muzi
JF-Expert Member
- Jun 17, 2016
- 1,038
- 1,448
NILIWAHI KUSEMA MAREKANI IKIPIGA CHAFYA DUNIA INAUGUA MAFUA
Pole Paul Makonda!
Kwa uamzi huu wa kumfungia Paul Makonda kuingia Marekani sasa ni rasmi hawezi kuwa rais wa Tanzania, waziri mkuu, waziri wa mambo ya nje wala balozi katika nchi yoyote ya Ulaya. (Nitafafanua).
Wakati wa matamko ya mataifa makubwa duniani kuhusu kuteteleka kwa haki za binadamu na demokrasia nchini kwetu nilitaadharisha kwamba sisi hatuna ubavu hata kidogo wa kutunishiana kifua na Marekani. Kama kawaida team KUSIFIA walikuja juu kwamba sisi ni nchi huru na hatupangiwi cha kufanya na nchi yoyote.
Sasa Makonda yamemkuta! Nimesema hapo juu nafasi ambazo hawezi kuzigusa tokana na uamzi huu wa Marekani.
Makonda hawezi kuwa rais tena kwa sababu huwezi kuwa na rais wa nchi asiyeweza kukanyaga New York (Umoja wa Mataifa) kwa sababu New York ni ardhi ya Marekani.
Makonda hawezi kuwa Waziri Mkuu kwa sababu huwezi kuwa na Waziri Mkuu asiyeweza kufika Umoja wa Mataifa. Wala huwezi kuwa na waziri wa mambo ya nje asiyefika Umoja wa mataifa. Lakini pia hawezi kuwa balozi kwenye nchi yoyote inayofuata misingi ya kidemokrasia hasa nchi za Ulaya.
Makonda pia hajapona kupelekwa mahakama ya kimataifa ya haki za binadamu ikiwa Marekani wakiamua kupeleka ushaidi wanaosema wanao.
Hii issue siyo ndogo kama watu wanavyojaribu kubeza kwa kutumia cheap propaganda. Kwa Afrika mashariki ni watu watatu tu wamechukuliwa hatua kama hizo. Mkuu wa polisi wa zamani wa Uganda Kale Kaihula na mwanasheria mkuu wa zamani wa Kenya Amos Wako. Lakini hawa wawili wana nafuu kwa sababu tuhuma zao ni za ufisadi na siyo ukiukaji wa haki za binadamu
From Edward Mpaka
Pole Paul Makonda!
Kwa uamzi huu wa kumfungia Paul Makonda kuingia Marekani sasa ni rasmi hawezi kuwa rais wa Tanzania, waziri mkuu, waziri wa mambo ya nje wala balozi katika nchi yoyote ya Ulaya. (Nitafafanua).
Wakati wa matamko ya mataifa makubwa duniani kuhusu kuteteleka kwa haki za binadamu na demokrasia nchini kwetu nilitaadharisha kwamba sisi hatuna ubavu hata kidogo wa kutunishiana kifua na Marekani. Kama kawaida team KUSIFIA walikuja juu kwamba sisi ni nchi huru na hatupangiwi cha kufanya na nchi yoyote.
Sasa Makonda yamemkuta! Nimesema hapo juu nafasi ambazo hawezi kuzigusa tokana na uamzi huu wa Marekani.
Makonda hawezi kuwa rais tena kwa sababu huwezi kuwa na rais wa nchi asiyeweza kukanyaga New York (Umoja wa Mataifa) kwa sababu New York ni ardhi ya Marekani.
Makonda hawezi kuwa Waziri Mkuu kwa sababu huwezi kuwa na Waziri Mkuu asiyeweza kufika Umoja wa Mataifa. Wala huwezi kuwa na waziri wa mambo ya nje asiyefika Umoja wa mataifa. Lakini pia hawezi kuwa balozi kwenye nchi yoyote inayofuata misingi ya kidemokrasia hasa nchi za Ulaya.
Makonda pia hajapona kupelekwa mahakama ya kimataifa ya haki za binadamu ikiwa Marekani wakiamua kupeleka ushaidi wanaosema wanao.
Hii issue siyo ndogo kama watu wanavyojaribu kubeza kwa kutumia cheap propaganda. Kwa Afrika mashariki ni watu watatu tu wamechukuliwa hatua kama hizo. Mkuu wa polisi wa zamani wa Uganda Kale Kaihula na mwanasheria mkuu wa zamani wa Kenya Amos Wako. Lakini hawa wawili wana nafuu kwa sababu tuhuma zao ni za ufisadi na siyo ukiukaji wa haki za binadamu
From Edward Mpaka