Kwa taarifa hii ya waangalizi wa uchaguzi pateni picha halisi ya ccm, nec na zec

Mwanamageuko

JF-Expert Member
Oct 31, 2010
8,602
5,569
MKUU wa kundi la waangalizi wa Umoja wa Ulaya, David Martin, jana ametoa taarifa yake ya awali kuhusu mchakato wa uchaguzi mkuu ulivyokwenda visiwani Zanzibar. Wakati huo huo Kamati ya waangalizi wa uchaguzi Tanzania TEMCO, nayo pia imetoa ripoti juu ya uchaguzi huo.
Katika taarifa yake kuhusu uchaguzi, mkuu wa waangalizi wa Umioja wa Ulaya David Martin, alisema kwa ujumla uchaguzi ulifanyika katika hali ya amani na utulivu, lakini akataja dosari zilizotokeza na ambazo zinatia wasiwasi katika mchakato mzima.
Alisema kuharibika kwa zaidi ya kura 10,000 (kama ni kweli hapo)ni moja wapo ya shaka hizo ambapo inaonesha kwamba elimu ya uraia ilikosekana na ndio sababu kubwa ya wananchi wengi kuharibu kura zao bila ya kujua.
Hali kadhalika alitaja juu ya kasoro zilizojitokeza katika upande wa utoaji nafasi katika vyombo vya habari vinavyomilikiwa na serikali kwa kuwa vimejiegemeza na kukibeba chama tawala cha CCM ambapo kimepewa nafasi kubwa mno na vile vya upinzani kuekewa vikwazo katika kutolewa taarifa zao.
Aidha kuhusu Tume alieleza kwamba, kulikuweko na uwazi lakini anasikitika na kukataliwa kwa wawakilishi wa vyama vya kisiasa na waangalizi wa ndani na wa kimataifa kuingia katika ukumbi wa kujumuisha matokeo ya kura na hivyo zoezi hilo kufanywa bila ya kushuhudiwa na waangalizi ambapo ni kinyume na makubaliano waliokubaliana. Mkuu huyo wa waangalizi alisema serikali na Tume ilishindwa kutekeleza ahadi nyingi zilizotolewa kabla ya waangalizi hao kufika nchini na akasisitiza kwamba litakua jambo la busara kuhakikisha mambo kama hayo yanarekebishwa katika uchaguzi wa siku zijazo. Na kupendekeza kuruhusiwa kuwepo kwa wagombea wakujitegemea, akiitaja kuwa ni haki ya kila raia.
Kutolewa kwa ripoti ya Umoja wa Ulaya hii leo ni hatua ya kwanza na ya awali kabla ya kutolewa ripoti kamili baadae mwezi huu. Wakati huo huo Kamati ya waangalizi wa uchaguzi Tanzania (TEMCO) nayo imetoa ripoti yake Zanzibar kuhusu uchaguzi huo na ikipongeza utulivu na amani ulioshuhudiwa wakati wa kampeni na siku ya uchaguzi, pamoja na hayo ilitaja juu ya dosari kadhaa upande wa mawakala wa tume na pia kunyimwa kwa chama cha upinzani nafasi ya kufanya mkutano katika jimbo la Donge.
Mhadhiri mwandamizi wa chuo kikuu cha dare s salaam, Bashiru Ali aliwaambia waandishi wa habari katika ukumbi wa Eacrotanal kwamba ameshangazwa kuwa Tume ilishindwa kuchukua hatua yoyote wakati chama cha CUF kuilipokataliwa kufanya mkutano wake katika jimbo la Donge na akawasifu viongozi wa CUF kwa kuwashawishi wanachama wao na kuepusha shari.
"Nilikuwepo katika mkutano uliofanyiak Jangombe Maalim Seif na Jussa walitumia nusu saa nzima kuwashawishi wanachama wao waachane na mkutano wa Donge, hata hivyo vyombo vya ulinzi na usalama vilikwenda kule Donge kuweka ulinzi vikidhani CUF watakwenda kwa nguvu…kwa kweli kuna tatizo kubwa katika utoaji wa viwanja vya kufanyia kampeni hata kama hili halijalalmikiwa lakini tatizo hilo lipo…" alisema Mratibu huyo wa TEMCO.

Nadhani picha imepatikana hapo

Nimeanza kumpa ushahidi yule ndugu yangu anaesema WACHAKACHUAJI HAWACHAKACHUI:sad:
 
Waangalizi wa Uchaguzi msitishike na mkwara wa Membe leo tarehe 10/09/2015.Tafadhali tumieni weledi wenu ili haki na demokrasia zitawale.

Hali ya nchi yetu ipo hivi na wananchi wameichoka CCM...... "Ni jamii iliyochoka na kuchakaa; ni jamii iliyooza na kuchoma pua kwa harufu ya uvundo wa rushwa na kujaza nzi wakubwa wa rangi ya Kijani, Ni jamii yenye ufisadi na ukandamizaji; ni jamii isiyojua mbele wala nyuma, ni jamii iliyokosa dira". Bunge lipo kwa jina tu kwa sababu limewekwa kwapani na watawala; Madaraka ya Rais ni makubwa kwa kiwango cha kupora demokrasia: Utajiri wa nchi upo mikononi mwa kikundi kidogo cha "wateule" na watawala kilichowageuza wananchi wadunda kazi wasiofaidi jasho lao. Na pale maandamano ya wanawake, wanaume na vijana wenye njaa yanapopita karibu na Makazi ya Wenye nacho,Malodilofa husimama ghorofani, wakawatazama na kuuliza, "kulikoni?". Na walipoambiwa kwamba yalikuwa ya "malofa" wenye njaa waliokosa mkate wa kila siku, wao walijibu: "Kama ni hivyo, kwa nini wasile nyasi na mihogo?"Vijana wanaangamia kwa kukosa maarifa mashuleni na wanaishia kubwia "unga" ambao ni biashara pendwa ya Malodilofa,vijana wasanii wenye vipaji mbalimbali wanageuka ombaomba na wakati wa Kampeni wanakuwa "lulu" kwa kutumika kujaza "nyomi" katika mikutano,wakulima wanazeeka kwa kazi ngumu mashambani na kukosa pembejeo za kisasa na mazao yao yanaishia kukopwa kwa bei ndogo ajabu,wavuvi wanachomewa nyavu zao walizonunua kwa wafanyabiashara wajanja wenye meno,wawindaji wa vitoweo wanaambiwa ni majangili huku tembo wakiuwawa kwa tama ya meno yao na twiga wakipandishwa ndege kwenda ulaya na Asia..Dah! wagonjwa wanakufa huku wamelala mzungu wanne sakafuni mahospitalini kwa kukosa madawa,wakina mama wanajifungulia vichochoroni kwa ubovu wa barabara, Na wanapoona malofa wanawapigia kelele kwa madai yao sahihi wanaamuru majeshi ya ndugu zao wanyonge wawapige mabomu ya machozi na kuwaua na kuwasababishia vilema vya maisha na kuwatesa waandishi wa habari zao za kilofa.Watawala wetu hivi leo wanatuhumiwa kumiliki mabilioni ya fedha wanayomiliki huku wakiyaita ni "vijisenti", au "fedha ya mboga", wakati kipato cha Watanzania walio wengi ni chini ya shilingi mia nane kwa siku. Wananchi wanapopiga kelele kugugumia bei kubwa ya kivuko wanaambiwa "Wapige mbizi" na pale ndege ya Rais na rada chakavu inaponunuliwa kwa pesa nyingi zenye asilimia kumi za wajanja wanaambiwa "Ni heri wale nyasi"…Pamoja na mikakati mikubwa na yakutumia fedha na rasilimali nyingi za walala hoi kwa ajili ya kuvuruga "Mabadiliko" kwa kuwanunua wanasiasa uchwara na kuwakashfu kuwa ni "wapumbavu,amlofa na mbumbumbu". Wakati umefika,chama kilichokuwa na dhamana ya haya yote kipumzishwe,ili kijitafakari,kitakapokuja kwa mara nyingine (MUNGU akikijaalia) kije kikiwa kamili....Kwa wakati huu,nathubutu kusema,Naichagua UKAWA,...sio kwa sababu za uimara wa CDM,CUF,NLD,NCCR MAGEUZI ama Uimara wa UKAWA la hasha!!Ila ni kwa sababu ya udhaifu wa CCM na ahadi ilizoshindwa kuzitekeleza kwa miaka 54 mfululizo."ALUTA Continua, Victoria Ascerta".... "The Struggle Continues, Victory is Certain"; ...Mapambano yanaendelea, Ushindi unakuja!! ≠HapaNimakwenziTu!!
 
Back
Top Bottom