Kwa nini CCM ikihofie CHADEMA?

Kwa nini CCM ikihofie CHADEMA?

Points of correction:
1;CCM haikuruhusu mfumo wa vyama vingi kwa matakwa yake.mfumo huu ni matokeo ya presha za wenye Dunia kama World bank na IMF.
2;Anguko la USSR pialilikuwa sababu tosha ya CCM kukubali kwa shingo upande mfumo huu.;

Tumeshazoea walalamikaji ambao jambo likiwa zuri basi wanadhani limetokea kwa bahati mbaya, lakini kikitokea kitu kibaya basi wako mstari wa mbele kulaumu.
Wewe ni mmoja wao, unadhani mfumo wa vyama vingi umetokea bila CCM kupenda, lakini umasikini wako umesababishwa na CCM.
Watu kama nyinyi kwenye jamii hamuepukiki.
 
Tumeshazoea walalamikaji ambao jambo likiwa zuri basi wanadhani limetokea kwa bahati mbaya, lakini kikitokea kitu kibaya basi wako mstari wa mbele kulaumu.
Wewe ni mmoja wao, unadhani mfumo wa vyama vingi umetokea bila CCM kupenda, lakini umasikini wako umesababishwa na CCM.
Watu kama nyinyi kwenye jamii hamuepukiki.

Hatupo hapa kuwasifia CCM tutawakimbiza mwanzo mwisho mpake mkae,Na sisi tunataka kuongoza Nchi vile vile kama nyinyi.
 
Viongozi wa vyama vya upinzani wanawalaghai wananchi kuwa wanaweza kuboresha maisha ya wananchi haraka haraka. Lakini wao kwa robo karne wameshindwa hata kuitoa CCM madarakani. Je, ipi ni kazi ngumu, kuboresha maisha ya watu au kuitoa CCM madarakani?

kweli nimeamini kuwa mshabiki wa ccm lazima ujitoe ufahamu, hv mechi inachezwa uwanjani refa ni wa ccm halafu ushinde uende cdm? 2010 cdm walishinda viti vingi vya ubunge na urais walishinda mbona hawakumtangaza cdm kuwa imeshinda?
 
Tumeshazoea walalamikaji ambao jambo likiwa zuri basi wanadhani limetokea kwa bahati mbaya, lakini kikitokea kitu kibaya basi wako mstari wa mbele kulaumu.
Wewe ni mmoja wao, unadhani mfumo wa vyama vingi umetokea bila CCM kupenda, lakini umasikini wako umesababishwa na CCM.
Watu kama nyinyi kwenye jamii hamuepukiki.
Sio kosa lako...kitendo chako cha kusoma magazeti ya udaku kila siku ndiko kunakokufanya usijue kwamba mfumo wa vyama vingi hakuja kwa hisani ya CCM.
 
Habari za jikoni zinasema kuanzia sasa cdm itapeleka elimu ya uraia nyumba hadi nyumba , 2015 ccm lazima ing'oke .
 
Kuuwawa kwa vibaka ni wananchi kukosa imani na vyombo vya dola, kuanzishwa kwa vikundi vya kujilinda ni ulegevu wa serikali na utumia upropaganda kwenye mambo ya msingi. wakati tukiongelea ushindi wa CCM tuongelee pia wizi, rushwa , vitisho na mauaji, ua katika siasa hakuna ubaya ili mradi ushinde kwasabau serikali haina dini?...kama kungekuwa na uchaguzi halali CCm isingekuwa madarakani...na kama unaakili timamu na tunatafuta kuikomboa tanzania yetu na kujitoa katika uchafu wa udini na vikundi basi CCM tuione ni adui mkubw kabisa wa kutafuta ukweli
 
Wewe akili yako ni ya kiwango cha bavicha. Nchi yoyote yenye chama kimoja chama hicho kinakuwa na asilimia 100 ya majimbo. Unapokuja mfumo wa vyama vingi ni LAZIMA majimbo hayo yapungue. Kwa vile wapinzani wako wengi basi walitakiwa kuwa na angalau asilimia 60 ya majimbo na CCM ibaki na asilimia 40. Hivi sasa CCM ina asilimia 70 ya majimbo. Kama akili yako ya bavicha inakudanganya kuwa CCM ni chama dhaifu basi tafuta mtu anayejua hesabu akufundishe tuition ili ujue kuwa CCM inashindana na vyama zaidi ya 10 na imefanikiwa kuwa juu kwa mbali sana kwa robo karne.
Kwa wizi wenu wa kura hiyo 60% inatoka wapi?...Juzi Shinyanga mkaiba bila aibu eti mbunge wenu akachukua kiti kwa tofauti ya kura moja.Shame on CCM!
 

TANGU kuanzishwa kwa vyama vingi nchini mwaka 1992, tayari chaguzi nne zinazoshirikisha vyama vingi zimefanyika.


Katika chaguzi hizo nne, Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimeendelea kushika dola kwa ushindi wa kishindo katika kiti cha urais, wabunge na madiwani.


Ushindi huu wa kishindo umeendelea kupungua kutoka ngazi ya ubunge na udiwani, ambapo wapinzani wamekuwa wakinyakua viti vya majimbo hata ambavyo vilikuwa vinatajwa kuwa ngome ya CCM.

Kupungua huko kwa viti vya ubunge na udiwani, ni kiashiria kuwahuenda kwa mara ya kwanza katika historia ya uchaguzi nchini, CCM itaenda katika uchaguzi mkuu mwaka 2015, kikiwa hakina uhakika wa kushinda.

Wapinzani wakuu wa CCM ni Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), ambacho kinashikilia rekodi ya pili kwa kuwa na viti vingi vya ubunge na udiwani nyuma ya CCM.

Nafasi ya ushindi katika uchaguzi huo, hasa katika ngazi ya urais imekumbwa na changamoto nyingi.

Wakati CCM imetimiza miaka 36 tangu kuzaliwa kwake, Chadema ina miaka 21 ambapo ndani ya miaka mitano kimeweza kujipambanua kwa Watanzania kama chama chenye sera madhubuti kinachotazamia kuchukua dola mwaka 2015.

Kwa nini CCM ikihofie Chadema na si vyama vingine? Ni mipango na mikakati ya muda mrefu, baada ya kuusoma mchezo wa CCM na kutumia udhaifu wake kujijenga.

CCM imewasahau wananchi wa kawaida na kukumbatia matajiri, Chadema ikaona hao ndio wanafaa na kuwafanya mtaji wao.

Ni ukweli ulio wazi kuwa mtaji wa chama chochote kile ni watu ambao ni wanachama hai.

Kitendo cha Chadema kutetea viti vyake vinne vya udiwani kwenye uchaguzi mdogo wa wiki iliyopita mkoani Arusha, ni hatua kubwa waliyopiga ambayo imekifanya chama hicho kufikisha idadi ya viti 15 kwenye Baraza la Madiwani, wakati CCM kimebakiwa kuwa na viti 12.

Mbio za Chadema kuifukuzia dola kwa kusimama na miguu yake yenyewe katika uchaguzi mkuu wa tatu ulioshirikisha vyama vingi mwaka 2005, baada ya kuwa msindikizaji kwa mihula miwili ambapo ilimsimamisha Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe wakati CCM ilimsimamisha Rais Jakaya Kikwete kwa mara ya kwanza.

Katika uchaguzi wa kwanza wa mwaka 1995, Chadema ilishiriki uchaguzi huo bila ya kuweka mgombea urais, ambapo walikubaliana kumuunga mkono mgombea wa chama cha NCCR-Mageuzi, Augustino Mrema ambaye alikuwa anakubalika sana wakati huo.

Uchaguzi mkuu wa mwaka 2000, Chadema ilishiriki tena uchaguzi huo kama mwanzo bila kusimamisha mgombea urais na safari hii ushirika ulihamia kwa CUF ambapo walimuunga mkono mgombea wake, Profesa Ibrahim Lipumba.

Mwaka huo, Chadema kilipata asilimia tatu ya kura za wabunge na jumla ya wabunge wanne na kushika nafasi ya nne katika vyama vya upinzani baada ya vyama vya CUF, TLP na UDP.

Baada ya kuchoka kuwa msindikizaji, Chadema ilijisuka upya na kumsimamisha Mbowe, ambaye alishindwa katika uchaguzi huo na hiyo ikawa kama changamoto kwa Chadema.

Chadema wakati huo ikaona ni wakati muafaka kujipambanua kwa wananchi, ambapo ilijieneza nchi nzima hata sehemu ambazo ilikuwa haikubaliki na kuvuna wanachama wengi zaidi.

Katika miaka yote hiyo CCM ilikuwa inaingia kwenye uchaguzi ikiwa na uhakika wa asilimia nyingi tu ya kushinda urais na viti vingi vya ubunge na udiwani bila kuhofia vyama vya upinzani.

Imani hii ya ushindi wa kishindo, inaanza kuyeyuka taratibu baada ya mwaka 2010, Chadema kupata viti vingi vya ubunge na udiwani hata katika majimbo ambayo yalikuwa ngome ya CCM.

Hofu ya kupoteza viti vingi vya ubunge na udiwani si hofu pekee inayoikabili CCM, bali pia inahofia kiti cha urais, haina uhakika nacho.

Tofauti kati ya Chadema na CCM baada ya uchaguzi ni kwamba, CCM hubweteka kwa madai ya kufanya kazi waliyotumwa na wananchi, lakini Chadema wao huchochea moto kwa kufanya mikutano mikoani yenye kauli mbiu za kuvutia kwa wananchi wanaopenda kusikia wanayotaka kusikia.

Mikutano hii imesaidia kuizindua CCM, ambapo nao hutembea mikoa iliyopitiwa na Chadema kujitakasa na kukanusha baadhi ya mambo baada ya jina lake kutiwa doa na Chadema.

Chadema imekuwa ikifanya mavuno katika vyuo vikuu mbalimbali pamoja na kuongeza idadi ya wanachama wanaotoka vyama vingine, wengi wao wakiwa viongozi.

CCM imekuwa ikifanya hivyo, lakini sasa ni kama imejisahau na inaanza upya ilipoishia.

Kujisahau huko kwa CCM kumeipaisha Chadema ambapo sasa ni vigumu kwa kijana wa kawaida kumueleza mambo hasi kuhusu Chadema.

Hii ni changamoto kwa CCM kushtuka na kuwakumbuka wananchi ambao kila uchao wanalalamikia ugumu wa maisha umeletwa na chama hicho.

Ni changamoto pia kwa Chadema kutobweteka kwa kuridhika na mafanikio madogo waliyo nayo.

KWA NINI CCM IKIHOFIE CHADEMA?? - MPEKUZI HURU

chadema ni chma cha kigaidi kwa hiyo lazima kihofiwe kwa sababu kinaua watu ambao hawana hatia.
 
Kuuwawa kwa vibaka ni wananchi kukosa imani na vyombo vya dola, kuanzishwa kwa vikundi vya kujilinda ni ulegevu wa serikali na utumia upropaganda kwenye mambo ya msingi. wakati tukiongelea ushindi wa CCM tuongelee pia wizi, rushwa , vitisho na mauaji, ua katika siasa hakuna ubaya ili mradi ushinde kwasabau serikali haina dini?...kama kungekuwa na uchaguzi halali CCm isingekuwa madarakani...na kama unaakili timamu na tunatafuta kuikomboa tanzania yetu na kujitoa katika uchafu wa udini na vikundi basi CCM tuione ni adui mkubw kabisa wa kutafuta ukweli

mbona unachekesha sasa nyie na chama chenu cha kihaini mnaanzisha kikundi cha waasi halafu mnasingizia kuwa umeshindwa kulindwa lakini majibu mtayapata tu watoto wa kiume wapo kwa ajiri ya kuwa kabili.
 
Viongozi wa vyama vya upinzani wanawalaghai wananchi kuwa wanaweza kuboresha maisha ya wananchi haraka haraka. Lakini wao kwa robo karne wameshindwa hata kuitoa CCM madarakani. Je, ipi ni kazi ngumu, kuboresha maisha ya watu au kuitoa CCM madarakani?

Kuitoa ccm madarakani kwani imeshika sana fikra za watu kwa kuwanyima elimu.
Mfano ni Kenya kwa kuwa wana Elimu ilukuwa rahisi kuitoa KANU madarakani.
Kuwaletea watu maisha mazuri ni kuwajenga ktk elimu bora ili waweze kubadilisha RASILIMALI ZAO KUWA MAENDELEO HALISI WALA SIO UCHAWI AU UGUMU KAMA CCM ILIVYOKUAMINISHA WEWE.
 
Wewe akili yako ni ya kiwango cha bavicha. Nchi yoyote yenye chama kimoja chama hicho kinakuwa na asilimia 100 ya majimbo. Unapokuja mfumo wa vyama vingi ni LAZIMA majimbo hayo yapungue. Kwa vile wapinzani wako wengi basi walitakiwa kuwa na angalau asilimia 60 ya majimbo na CCM ibaki na asilimia 40. Hivi sasa CCM ina asilimia 70 ya majimbo. Kama akili yako ya bavicha inakudanganya kuwa CCM ni chama dhaifu basi tafuta mtu anayejua hesabu akufundishe tuition ili ujue kuwa CCM inashindana na vyama zaidi ya 10 na imefanikiwa kuwa juu kwa mbali sana kwa robo karne.
Achane kushindana kwa kuiba na kutumia jeshi kupiga na kuuwa raia ambao hawana hatia tuone kama CCM mtapata viti 20%. Pia undeni tume huru ya uchaguzi na mtoe wazee kama Tendwa kwenye usajili wa vyama muone kama mtatoka. Mkifanya hivyo halafu mkashinda nahama nchi ndugu yangu.
 
chadema ni chma cha kigaidi kwa hiyo lazima kihofiwe kwa sababu kinaua watu ambao hawana hatia.
Kweli wewe ni chinemba la ukweli. Hivi magaidi ni kina nani? pole ndugu yangu. Hivi mbona hata haumuogopi wakati wakuandika vitu vya aibu kama hivi? Hata mtoto wa Makinda na Ndugai wanajua gaidi kwenye hii nchi na CCM na Green guards
 
Ccm bwana wajinga kweli. Eti wameingiza kodi ya cm card halafu wanarudi nyuma wanadai hawajaikubali. Loh. Mijinga sana hii mizee
 
mbona unachekesha sasa nyie na chama chenu cha kihaini mnaanzisha kikundi cha waasi halafu mnasingizia kuwa umeshindwa kulindwa lakini majibu mtayapata tu watoto wa kiume wapo kwa ajiri ya kuwa kabili.
wewe kaziyako ni kujibizana na ubishi, lakini ukinisoma vizuri ucngejibu hii pumba, ulegevu wa serikali ndiyo unaleta utaarab katika mambo ya msingi, nchi nyingine za watu ucngesikia upuuuzi kama huu wa watu kutupiana mpira, Ref: kwa ulimboka na Mwangosi, mnachojua ni kufungia magazeti kwa jibu la uongo rti wameandika kuhusu jeshi, kwa mtu mwenye akili hii ni aibu kubwa kwa kiongozi wa serikali kutokujua nini anongea, lakini usiwe na shaka 2015 itawapa majibu, Arusha itakuwa cha mtoto
 
Wakati CCM inaruhusu mfumo wa vyama vingi ilijua kuwa kutakuwa na changamoto kwenye kushika dola. CCM ingekuwa inaogopa upinzani isingeruhusu uwepo.

Kuweza kushika dola miaka zaidi ya 20 tangu upinzani uanzishwe ni mafanikio makubwa. CCM imeweka rekodi ya kudumu madarakani zaidi ya robo karne tangu kuanzisha upinzani!

Kwahiyo wapinzani Tanzania kwa robo karne wameshindwa kuwaconvince wananchi waisahau CCM. Hiyo ndio hali halisi iliyopo hivi sasa.

Masuala ya mwaka 2015 tusubiri 2015, mpira dakika 90 ingawa muda wa nyongeza kwenye fainali upo na ikibidi penati...


haikuruhusu ,bali ililazimika kukubali kutokana na kubadilika kwa mfumo wa dunia nzima.
 
viongozi wa vyama vya upinzani wanawalaghai wananchi kuwa wanaweza kuboresha maisha ya wananchi haraka haraka. Lakini wao kwa robo karne wameshindwa hata kuitoa ccm madarakani. Je, ipi ni kazi ngumu, kuboresha maisha ya watu au kuitoa ccm madarakani?

una maana gani kusema kuwa wameshindwa kutoa ccm madarakani kwa robo karne? Kwani hujui kuwa ccm inaiba kura na kubadilisha matokeo?! Na mtu wa kwanza kuisaidia ccm isitoke madarakani alikuwa hayati jkn? Si ndiye aliyesema matokeo ya zanzibar yabadilishwe haraka sana baada ya maalim seif kumshinda salmin! Na kuanzia hapo ccm ikajua mchezo huo ndio utakaofanywa hata bara?! Na kweli ndivyo ilivyofanywa? Hata kama mrema asingeshinda, kura zake nyingi ziliteketezwa, mkapa pengine angepita kwa kiwango kidogo sana au asingefikisha kura vilevile.
Na matokeo yake mchezo wa kuiba na kubadili kura umekua order of a day kwa ccm kwa kila uchaguzi? Sasa ndio vyama vya upinzani vimeshtuka na vinakula sambamba na hiyo mbinu, ndio maana unaona sehemu nyingine ccm inashindwa kabisa wakishabanwa.
Kwa hiyo ukiniambia eti kwa kuiba kura na kubadilisha ndio inamaanisha ccm bado inapendwa nashangaa sana, mnadanganya nani zaidi ya kujidanganya wenyewe?!
 
Nchi yetu ina fursa nyingi sana. Kila mwenye macho anaziona na kila mwenye akili ananufaika nazo.
Wapo watu wamekaa chini ya kivuli na vibarazani wanagoja siku kije chama fulani kuboresha maisha yao. Watu hao ni kama vile wamejiingiza kwenye puto la disappointment, its just a matter of time kabla puto hilo halijapasuka.

Kwa mtanzania mwenye bidii, for personal progress, Tanzania has more opportunities than any Europen country can offer. Only USA can compete with Tanzania in terms of opportunies of personal progress.
Mkuu ZeMarcopolo Tanzania hakuna kitu chochote

Wafadhili wanakusaidieni kisha munawapa ardhi yenu kuna Madini wanaiba Dhahabu,Almasi, na Madini yote wanakuacheni na njaa yenu

nyie mumelala usingizi amkeni Wa-Tanzania. Viongozi wenu wanaweka mikataba ya miaka 100 kwa wafanya biashara toka nje ya nchi

kwanini iwe miaka mingi mikataba ya kuuza nchi hiyo?Wizi mtupu huo nchi ina mafuta,Gesi, na Madini lakini bado ni Masikini na omba

omba mpaka lini tutategemea misaada toka nje?wakati tuna utajiri tunaukalia wenyewe ? tujiulize kwanini tunakuwa Masikini?
 
Mkuu ZeMarcopolo Tanzania hakuna kitu chochote Wafadhili wanakusaiieni kisha munawapa ardhi yenu kuna Madini wanaiba Dhahabu,Almasi, na Madini yote wanakuacheni na njaa yenu nyie mumelala usingizi amkeni Wa-Tanzania. Viongozi wenu wanaweka mikata ya miaka 100 kwa wafanya biashara toka nje ya nchi kwanini iwe miaka mingi mikataba ya kuuza nchi hiyo?Wizi mtupu huo nchi ina mafuta,Gesi, na Madini lakini bado ni Masikini na omba omba mpaka lini tutategemea misaada toka nje?wakati tuna utajiri tunaukalia wenyewe ? tujiulize kwanini tunakuwa Masikini?

da! mzizimkavu leo nimekukubali!
 
Last edited by a moderator:
da! mzizimkavu leo nimekukubali!
Mkuu Highlander mimi huwa sipendi kuzungumza mambo ya Siasa lakini nikiamuwa kuzungumza ninazungumza ukweli na huo ukweli kwa hapo kwetu Tanzania hautakiwi hata kidogo ukisema ukweli

wanakulimboka. Sasa kweli nchi yako na viongozi wa nchi yako hawataki useme ukweli utanyamaza mpaka lini?kila siku Umeme wa

mgao,Majisafi hakuna Mijini mpaka vijijini viongozi wetu wanatembea na Magari ya kifahari walala hoi ndio wanaoteseka inauma

sana.Viongozi wetu hawana huruma kwa wale walio wachaguwa kuongoza nchi yetu je kweli tutakuwa na maendeleo ya ukweli? Itabaki

hadithi tupu tuamkeni tuchague Viongozi wenye kuipenda nchi yetu na viongozi wenye kupenda Maendeleo ya walala hoi tuache

tofauti zetu za Udini.
 
Nchi yetu ina fursa nyingi sana. Kila mwenye macho anaziona na kila mwenye akili ananufaika nazo.
Wapo watu wamekaa chini ya kivuli na vibarazani wanagoja siku kije chama fulani kuboresha maisha yao. Watu hao ni kama vile wamejiingiza kwenye puto la disappointment, its just a matter of time kabla puto hilo halijapasuka.

Kwa mtanzania mwenye bidii, for personal progress, Tanzania has more opportunities than any Europen country can offer. Only USA can compete with Tanzania in terms of opportunies of personal progress.
Kama kuna fursa kama udaivyo wewe, CCM na serikali yake imeshindwa nini Kuifanya Dar iwe kama New York au L.A?CCM na serikali yake imeshindwa nini kupunguza vifo vya kinamama na watoto under 5,CCM na serkali yake imeshindwa nini kuwapatia watoto wote madawati na vitabu.Mpaka sasa 85% ya nchi haina umeme?Leo hii kila masika ikianza Dar na miji mingine TZ ni vipindupindu tu-halafu bila aibu unaifananisha Marekani na Tanzania!Fursa zilizopo Marekani hazijaja tu kwa kuota....zimetengenezwa na sera nzuri NA USIMAMIZI MADHUBUTI wa za serikali husika.Ulishasikia Wamarekani wanacheka na wansiasa/viongozi wazembe wasio na maadili na wala rushwa kama wafanyavyo ccm?Unakumbuka Bill Clinton alivyotiwa aibu ktk ishu yake ya umalaya na Monica Lewinski?Hapa bongo ni mara ngapi watu wamewapa wachumba zao ukuu wa wilaya,?Huko BOT ndo usiseme...its like a list of "Who is who" ya bongo politics!Wananchi wakianzisha vimigodi vyao ninyi mnavamia na kuwapa "wawekezaji"...nchi ambayo 48% ya bajeti yake inategemea wahisani..alafu eti unakuja kuongea about fursa....FURSA my foot!
 
Back
Top Bottom