Kisoda2
JF-Expert Member
- May 30, 2008
- 2,475
- 747
Siku moja umerudi na mning'ining'io(hanover) wako ongeza na usingizi mkali wa kukesha yapata kama saa tisa unusu ama kumi ndo umeingia kulala.
Yapata majira ya saa moja asubuhi mtu anakugongea mlango kwa nguvu(fujo/kero).
Unaamka ili kwenda fungua upate kujua nani huyo, unajikwaa kidole cha mwisho cha mguu kwenye mfumbati wa kitanda, kisha kwa mawenge ya kilichotokea tena unagonga ndoo ya maji nayo inamwagika.
Unafungua mlango unakutana na jamaa anakwambia nauza VOCHA za simu tena kakukenulia meno eti pozi la biashara!!
Yapata majira ya saa moja asubuhi mtu anakugongea mlango kwa nguvu(fujo/kero).
Unaamka ili kwenda fungua upate kujua nani huyo, unajikwaa kidole cha mwisho cha mguu kwenye mfumbati wa kitanda, kisha kwa mawenge ya kilichotokea tena unagonga ndoo ya maji nayo inamwagika.
Unafungua mlango unakutana na jamaa anakwambia nauza VOCHA za simu tena kakukenulia meno eti pozi la biashara!!
Utafanya nini? Kwa ninavyokujua wewe!!:whistle::whistle::whistle: