Kwa namna hii kuna haja ya kuwa na marafiki kweli?

TheMnyonge

JF-Expert Member
Mar 25, 2022
739
1,871
Ndugu zangu, naandika nikiwa very down yaani, na kila nikifikiria nashindwa kujua what kind of friends do I have?

Nimekuwa na marafiki kadhaa ambao kwa mtazamo wangu nimekuwa nikidhani tunafaana, ila kumbe mimi ndo nawafaa wao tu.

Kumekuwa na hizi mambo ambazo baada ya kufikiria kwa kina naona hakuna haja ya kuwa na marafiki kabisa.

Kila wakiazima pesa jamaa zangu hawa HAWARUDISHI, wengine wanaazima then wanaanza kurudisha kidogo kidogo, naanza na hizi tatu za karibuni...

1. Jamaa alipatwa na bonge la dharura akiwa nje ya jiji, akaniomba nimuwekee 400,000/= akirudi anakuja ku-clear, (Mimi nafanya biashara ya miamala ya kifedha) nikamtumia jamaa a solve tatizo lake, siku mbili baadaye jamaa alirudi ila hakuwa anazungumzia chochote kuhusu pesa yangu, Mara wiki ikakata, nikamkumbusha kuwa ile ni pesa ya biashara na ipo kwenye mzunguko akasema "soon ntakurekebishia" ila kimya...(huyu ni mtu nimesoma naye, anafanya kazi na pesa najua anayo ila dhamira ya kurudisha hana!)

2. Hii imetokea mwezi mmoja uliopita, jamaa tupo naye kazini na ni rafiki yangu wa karibu kabisa, ghafla ulitokea msiba wa baba yake huko mkoani, Bahati mbaya hakuwa vizuri, kwa kuwa anajua kaofisi ka miamala hakapo vibaya sana akanifuata na kuomba nimpe 350,000/= then soon angenirejeshea, nikamsisitiza sana kwamba pesa ni ya biashara, aka-declear kwamba ile pesa ya mkono wa pole kutoka ofisini (ambayo ni 500,000) nitachuku 350,000 then inayobaki ndo atumiwe (maana hii pesa huwa inatolewa immediately inapotokea dharura ya aina yake)

Cha ajabu nilipokwenda kwa muhasibu kumwambia anipe hiyo 350,000 nikaambiwa jamaa aliitaka yote na wameshamtumia tayari, nikanyamaza, jamaa alirudi job, lakini pesa yangu haizungumzii kabisa, nikamkumbusha akaniambia atanipa mwisho wa mwezi, imefika mwisho wa mwezi akanipa 100,000/= kirahisi kabisa akaniambia nyingine mwezi ujao, nilishikwa hasira sana nikaondoka.

Jamaa wa tatu aliipata janga la kuunguliwa na vitu, katika kutafuta namna ya kusimama upya akaniomba 450,000/= katika hiyo alirudisha 250,000/= nyingine mpaka leo kimyaaa, sasa najiuliza aina huu ya urafiki wa kurudishana nyuma kuna ulazima wa kuendelea nao kweli?

Naombeni mbinu za kuishi bila interaction na marafiki, maana inafika mahali naona kama wanafanya makusudi kunikwamisha tu, na kwanini marafiki ndo wanakuwa wa kwanza kutuangusha?

Najiuliza kwani hawa jamaa wananionaje?
 
Sometimes I have been so sympathetic, ikiwa ni tatizo kubwa nikimuangalia rafiki yangu naona ngoja nimsaidie kwa muda then atarudisha pesa na circle ya biashara itaendelea, ila matokeo yake ndiyo hivyo tens...
Kukopa harusi kulipa matanga
 
Sio wanakuonaje ni hiviii. Hakuna urafiki kwenye pesa, Hakuna undugu kwenye pesa, Hakuna huruma kwenye pesa. Pesa huvunja urafiki, undugu na hata amani yako ya moyo.

Hivyo kama unahitaji kuutunza urafiki, undugu na amani ya moyo wako bas achana na habari za kukopesha pesa kwa watu wakaribu yako kwani marejesho ni ugomvi.

Kama mtu anashida msaidie na sahau habari za kukopesha
 
Sio wanakuonaje ni hiviii.....Hakuna urafiki kwenye pesa, Hakuna undugu kwenye pesa, Hakuna huruma kwenye pesa. Pesa huvunja urafiki, undugu na hata amani yako ya moyo. Hivyo kama unahitaji kuutunza urafiki, undugu na amani ya moyo wako bas achana na habari za kukopesha pesa kwa watu wakaribu yako kwani marejesho ni ugomvi
kama mtu anashida msaidie na sahau habari za kukopesha
Nakubaliana na wewe kabisa, ila marafiki wanapokuja wakiwa na shida nzito na wanajua kabisa uwezo wa kuwasaidia kusolve matatizo kwa dharura, ila kwanini hawawezi kufikiria kwa utu tu na kurudisha kwa uaminifuuuu?
 
Neno sina hela,hali mbaya hakuna biashara ndio huwa zipo kwenye midomo ya mfanyabiashara wa kweli,na ikitokea unamkopesha mtu inabidi umtafute mtu fake kwamba ndio atamkopesha pesa sio wewe kwa hivyo hapo dhamana itahusika na asipolipa kwa wakati unapiga mnada dhamana,hii itakuondolea hasara za kipumbavu
 
Ikiwa mtu anaona pesa unayo na unamwambia huna urafiki utabaki kweli?

That is why nimefikiria kuachana na urafiki wa aina hii, ili iwe clear kwamba sisi si marafiki tena baaas...

Ukiwa na rafiki anakukopa kopa kimbia
Mi nishagundua ukiwa mwenyewe kwanza unafanikiwa vitu vingi ,marafiki iwe kwa simu tu
Japo wapo wachache wa ukweli lakin wengi ni hovyo
 
Ikiwa mtu anaona pesa unayo na unamwambia huna urafiki utabaki kweli?

That is why nimefikiria kuachana na urafiki wa aina hii, ili iwe clear kwamba sisi si marafiki tena baaas...
Anaonaje hela unayo?punguza show off, jifunze pia kutenganisha biashara na mambo yako binafsi, wewe na biashara ni vitu viwili tofauti na iwe hivyo kwa sababu kama ungekuwa na hela kama anavyoona, ungetoa kwenye mfuko wako umpe na ndivyo inavyotakiwa kufanyika, la sivyo hata biashara yako itakufa, urafiki na undugu utakufa...ndipo utaelewa maana ya maneno "sina hela"...hii haimaanishi usisaidie watu wakiwa na shida, ila toa mfukoni kwako
 
Ndugu zangu, naandika nikiwa very down yaani, na kila nikifikiria nashindwa kujua what kind of friends do I have???

Nimekuwa na marafiki kadhaa ambao kwa mtazamo wangu nimekuwa nikidhani tunafaana, ila kumbe mimi ndo nawafaa wao tu...

Kumekuwa na hizi mambo ambazo baada ya kufikiria kwa kina naona hakuna haja ya kuwa na marafiki kabisa...

Kila wakiazima pesa jamaa zangu hawa HAWARUDISHI, wengine wanaazima then wanaanza kurudisha kidogo kidogo...naanza na hizi tatu za karibuni...

1. Jamaa alipatwa na bonge la dharura akiwa nje ya jiji, akaniomba nimuwekee 400,000/= akirudi anakuja ku-clear, (Mimi nafanya biashara ya miamala ya kifedha) nikamtumia jamaa a solve tatizo lake, siku mbili baadaye jamaa alirudi ila hakuwa anazungumzia chochote kuhusu pesa yangu, Mara wiki ikakata, nikamkumbusha kuwa ile ni pesa ya biashara na ipo kwenye mzunguko akasema "soon ntakurekebishia" ila kimya...(huyu ni mtu nimesoma naye, anafanya kazi na pesa najua anayo ila dhamira ya kurudisha hana!)

2. Hii imetokea mwezi mmoja uliopita, jamaa tupo naye kazini na ni rafiki yangu wa karibu kabisa, ghafla ulitokea msiba wa baba yake huko mkoani, Bahati mbaya hakuwa vizuri, kwa kuwa anajua kaofisi ka miamala hakapo vibaya sana akanifuata na kuomba nimpe 350,000/= then soon angenirejeshea, nikamsisitiza sana kwamba pesa ni ya biashara, aka-declear kwamba ile pesa ya mkono wa pole kutoka ofisini (ambayo ni 500,000) nitachuku 350,000 then inayobaki ndo atumiwe (maana hii pesa huwa inatolewa immediately inapotokea dharura ya aina yake)

Cha ajabu nilipokwenda kwa muhasibu kumwambia anipe hiyo 350,000 nikaambiwa jamaa aliitaka yote na wameshamtumia tayari, nikanyamaza, jamaa alirudi job, lakini pesa yangu haizungumzii kabisa, nikamkumbusha akaniambia atanipa mwisho wa mwezi, imefika mwisho wa mwezi akanipa 100,000/= kirahisi kabisa akaniambia nyingine mwezi ujao, nilishikwa hasira sana nikaondoka...

Jamaa wa tatu aliipata janga la kuunguliwa na vitu, katika kutafuta namna ya kusimama upya akaniomba 450,000/= katika hiyo alirudisha 250,000/= nyingine mpaka leo kimyaaa, sasa najiuliza aina huu ya urafiki wa kurudishana nyuma kuna ulazima wa kuendelea nao kweli???

Naombeni mbinu za kuishi bila interaction na marafiki, maana inafika mahali naona kama wanafanya makusudi kunikwamisha tu, na kwanini marafiki ndo wanakuwa wa kwanza kutuangusha???

Najiuliza kwani hawa jamaa wananionaje?
Ww ujengewe sanamu kubwa hapo ofcin unapofanyia kazi kisha waweke bango kubwa linalosomeka MTAKATIFU WA KUSINI au nasema uongo ndugu zangu
 
Back
Top Bottom