Kwa Mzee wa Upako ni magari tu?

Kwa Mzee wa Upako ni magari tu?

Kwa upande wa pili, idadi ya watu wanaokwenda kwenye nyumba za ibada kuutafuta "ufalme wa dunia" - majumba, magari vyeo, kufanikiwa kibiashara, kufaulu mitihani, afya njema ya mwili, kuoa/kuolewa, kupata watoto, n.k. bila kwanza kutaka usafi wa roho, imeongezeka sana. Tena wanataka kupata vitu hivyo haraka sana kwa miujiza ya chapchap. Hii imekuwa kivutio kikubwa kwa "watumishi" kuandaa na kuwasilisha "huduma" zinazokidhi mahitaji ya "wateja" wengi badala ya kuweka msisitizo katika kuutafuta Ufalme wa Mbinguni.
 
Kwa upande wa pili, idadi ya watu wanaokwenda kwenye nyumba za ibada kuutafuta "ufalme wa dunia" - majumba, magari vyeo, kufanikiwa kibiashara, kufaulu mitihani, afya njema ya mwili, kuoa/kuolewa, kupata watoto, n.k. bila kwanza kutaka usafi wa roho, imeongezeka sana. Tena wanataka kupata vitu hivyo haraka sana kwa miujiza ya chapchap. Hii imekuwa kivutio kikubwa kwa "watumishi" kuandaa na kuwasilisha "huduma" zinazokidhi mahitaji ya "wateja" wengi badala ya kuweka msisitizo katika kuutafuta Ufalme wa Mbinguni.

..swali kubwa hapa ni je kweli wanafanikiwa?kama jibu ni ndio then haina haja ya kumwita tapeli...ni ukweli usiopingika kuwa mafanikio ya kiimami hayapimwi tu kwa magari na majumba,lakini ni moja ya baraka za MUNGU.
 
Neno linasema "Utafuteni kwanza Ufalme wa Mbinguni na Haki Yake ..." Mathayo 6:33. Huo ndio msingi wa Ukristo ninaouamini. Watoto, majumba, magari, vyeo, n.k. ni matokeo tu na vielelezo vya aina ya baraka nyingi anazoweza kutoa Mwenyenzi Mungu ila si uthibitisho wa ubora wa Mkristo. Hata wasioamini huwa navyo tele tena wengine (wengi) huvipata katika matendo ya dhambi. Hivyo, kuvitanguliza vitu hivyo ni kugeuza Ibada kuwa biashara au aina ya ushirikina. I have no flexibility on that stance.
 
tulikua nanawacheka waislam wanaodanganywa kujilipua wende mbinguni wakapewe wake wazur wenye masikio makubwa kama vikombe huku wale wanaowatuma hawana huo mpango kama osama sasa na cc yametukuta sasa injiri ya utajiri tu na sio toba hapa kazi tunayo
 
wazungu watupite hadi kwenye mahubiri... haha, wahubiri wao hawasemi njoo upate gari, wanasema njoo umuabudu Mungu.. duh! bongo ujinga ni excess umejaa hadi unaflow
 
Hiyo utasikia Emmanuel TV tu na sio kwa mzee wa upaku.
Kule kuna ushuhuda hadi wa kuweza kusoma biblia bila kusinzia. Kuanza kuheshimu wazazi kwa watoto watukutu.

Mmh kaunga nyuzi za hivi hauwezi kukosa , nilipokuwa na fungua thread hii nikajua utakuwepo page za awali tu
 
huyu ni mmoja kati ya maelfu ambao walitabiriwa kuja kwa njia za kilaghai,bado mamilioni wenine kama yeye wanakuja ...wanastahili hukumu yetu hawa
 
huyu ni mmoja kati ya maelfu ambao walitabiriwa kuja kwa njia za kilaghai,bado mamilioni wenine kama yeye wanakuja .....!,?wanastahili hukumu yetu hawa
 
Mungu wa mzee wa Upako ni material God,ni pesa kwa kwenda mbele
 
tulikua nanawacheka waislam wanaodanganywa kujilipua wende mbinguni wakapewe wake wazur wenye masikio makubwa kama vikombe huku wale wanaowatuma hawana huo mpango kama osama sasa na cc yametukuta sasa injiri ya utajiri tu na sio toba hapa kazi tunayo
Injili.
 
Kwa upande wa pili, [size=+2][idadi ya watu wanaokwenda kwenye nyumba za ibada kuutafuta "ufalme wa dunia" - majumba, magari vyeo, kufanikiwa kibiashara, kufaulu mitihani, afya njema ya mwili, kuoa/kuolewa, kupata watoto, n.k. bila kwanza kutaka usafi wa roho, imeongezeka sana.[/size] Tena wanataka kupata vitu hivyo haraka sana kwa miujiza ya chapchap[/I]. Hii imekuwa kivutio kikubwa kwa "watumishi" kuandaa na kuwasilisha "huduma" zinazokidhi mahitaji ya "wateja" wengi badala ya kuweka msisitizo katika kuutafuta Ufalme wa Mbinguni.

Ni kweli mkuu!
 
Nimekuwa nikiangalia mahubiri ya mzee wa upako,kila muumini anaye kwenda kutoa ushuhuda utasikia '' Mimi nilikuja

hapa sina gari ila sasa na magari matatu na nyumba mbili'' Sijapata kusikia muumini hata mmoja aliyesema ''Mimi

nilikuwa nakabiashara cha kuuza mchicha kwa kutembeza kwa miguu ila sasa namshukuru Mzee wa upako kwa maombi

yake nimepata baiskeli walau naweza kutembeza biashara sehemu nyingi tofauti na mwanzo,

Hayo magari na nyumba ndani miezi mitatu tu ??? ""Tafakari chukua hatua "

Bila shaka wewe siomfuatiliaji mzuri wa vipindi vyake vya shuhuda, vipi uponyaji hujaona?
 
Pia tumeambiwa tuzipime roho maana si zote zinatoka kwa Mungu. Kumbuka kuna counterfeit miracles. Musa alitupa fimbo yake chini na wale wachawi wamisri walitupa zao zikageuka nyoka ila nyoka wa musa akawala wale counterfeit nyokas. Tusikimbilie miujiza. Neno la Mungu linasema tafuta sana ufalme wa Mungu na mengine yote utazidishiwa. Nilichoelewa katika mada hii ni huo msisitizo wa mali badala ya kuokoa roho za watu. Mtumishi wa Mungu huwa anaweka emphasis kwenye kuokoa roho za watu. Usemi wako ni wa kweli maana Mungu alimwadhibu Miriamu dada yake Musa kwa kumsema mtumishi wake Musa kuhusu wifi yake (Mke wa Musa ambaye hakuwa myahudi). Lakini "pima roho dont believe every so called preacher"
Imeandikwa usimseme vibaya mtumishi wa bwana
 
Mungu wa mzee wa Upako ni material God,ni pesa kwa kwenda mbele

Tena Mungu wake anaenda na wakati...anajua watx wengi wanahitaji nini kwa sasa ni magari na nyumba fullstop...

Mambo Mengine Baadaye!!
 
nikiwa kama Mkristo niliyeokoka nina wasiwasi na uwezo wa Mzee wa Upako.

Mungu ni wa ajabu sana,baada ya kumwokoa mtu anampa nafasi ya kujijengea uwezo wa kuelewa maandiko ndani ya Biblia,nashangaa sana Mungu hapendi kuingilia maamuzi ya mtu yeyote hata kama ni Mtumishi wake.

Jamani ndugu zangu magari ni matatizoooooooo,naombeni sana siyo lazima kuwa na gari,hivi kama unaishi Dar na kuna public transport ambayo ni well arranged kuna haja ya kulazimisha kununua gari?

Jamani tuache hayo mambo bana kwani lazima uwe na gari?

Hivi unajua gharama ya ku-maintain gari?

nimeshamiliki magari mengi na sasa hivi sioni haja ya kuwa na gari ni matatizo mara mechanical problem mara mafuta mara umegonga gari la mtu,sasa hayo ndipo unapojiongezea majaribu na kufanya wokovu wako kuwa mgumu zaidi.

Kama unaweza kwenda kazini au kwenye shughuli zako na public transport kwa nini ujitafutie matatizo?kwani nani alisema baraka ni kuwa na gari?

Amani mioyoni mwetu ndiyo baraka kuu,Mzee wa Upako nisamehe hapo umeonyesha uwezo mdogo sana.
 
Mimi sijawahi kumsikia mtu anasema 'zamani nilikuwa siwezi kulala bila kuzini ila siku hizi namshukuru Mungu amenishindia hii dhambi'
Nilitaka nikugongee 'like', nikagundua kwamba kumbe sijalogin !!
 
Wewe ndo unakosea. Mm sijaona sehemu ambayo mzee wa upako anakosea. Kwan humfuta mtu mkono na kusema nakuombea upate gari?? Bali kwa anaetaka kuwa na gari na watu huenda.kama yamekushinda hayo ya kwako peke yako.
 
Wewe ndo unakosea. Mm sijaona sehemu ambayo mzee wa upako anakosea. Kwan humfuta mtu mkono na kusema nakuombea upate gari?? Bali kwa anaetaka kuwa na gari na watu huenda.kama yamekushinda hayo ya kwako peke yako.

Kesi ya nyani......kwa tumbili . Oh ni wale wale. Tajiri na ufalme wa Mungu.
 
Back
Top Bottom