Kwa Mzee wa Upako ni magari tu?

Kwa Mzee wa Upako ni magari tu?

ZINDIKO

Member
Joined
May 14, 2014
Posts
24
Reaction score
6
Nimekuwa nikiangalia mahubiri ya mzee wa upako,kila muumini anaye kwenda kutoa ushuhuda utasikia '' Mimi nilikuja hapa sina gari ila sasa na magari matatu na nyumba mbili''

Sijapata kusikia muumini hata mmoja aliyesema ''Mimi Nilikuwa na kabiashara cha kuuza mchicha kwa kutembeza kwa miguu ila sasa namshukuru Mzee wa upako kwa maombi yake nimepata baiskeli walau naweza kutembeza biashara sehemu nyingi tofauti na mwanzo,"

Hayo magari na nyumba ndani miezi mitatu tu ???

"Tafakari chukua hatua "
 
Wajinga ndio waliwao, magari yapo hata Lushoto, Mwahanuzi, Somalia, Darfur, Gamboshi na kwingineko ambako hakuna Mzee wa upako. Kuwa na gari kunategemea juhudi kazini, kipato na vipaumbele vyako kwenye maisha.

Magari yanaongeza foleni, yanaleta ajali, yanaharibu mazingira, yanatumika kufanya uhalifu, yanatumia hela za matumizi mengine kama chakula, ada za shule, n.k. Hivyo gari sio deal na wala haliwezi kutumiwa kama kigezo cha mafanikio.

Kule Marekani vijana wengi wana magari ya mikopo lakini hawana pa kulala wala ada ya kujisomesha. Wanalala ndani ya magari hayo, huku ni kuwapumbaza vijana wasione umuhimu wa kusoma na kufanya kazi kwa bidii na kuzingatia vipaumbele vyao kwenye maisha.
 
Mimi sijawahi kumsikia mtu anasema 'zamani nilikuwa siwezi kulala bila kuzini ila siku hizi namshukuru Mungu amenishindia hii dhambi'
Hiyo utasikia Emmanuel TV tu na sio kwa mzee wa upaku.
Kule kuna ushuhuda hadi wa kuweza kusoma biblia bila kusinzia. Kuanza kuheshimu wazazi kwa watoto watukutu.
 
Wajinga ndio waliwao, magari yapo hata Lushoto, Mwahanuzi, Somalia, Darfur, Gamboshi na kwingineko ambako hakuna Mzee wa upako.

Shangaa na wewe mkuu...hivi gari ndio maendeleo?
 
Kati ya watu ambao roho yangu hainishawishi KUWAAMINI huyu ni mmoja wapo!
 
Sasa hivi anawafool watu eti huwezi barikiwa kama hujatoa sadaka. This means to encourage "malofa"/waumini wake watoe awaombee. mwizi mkubwa.

Watu wana shida za uzazi, familia, wanaume mahanithi wote hao wanatafuta faraja, anawadanganya muhuni mkubwa. Masikini kwa vile wana shida wanatafuta wapi watapata majibu ya shida zao.

This is deep rooted belief which is difficult to uproot. Anakuombea upate gari at the same time anapokea shilingi shilingi za hawa masikini.
 
Naamini muujiza wa mtu uko popote na katika lolote. Sidhani kama Mungu anafanya miujiza kwa wenye kujiweza na kupungukiwa na magari na nyumba tu. WaPo wengine kwenye mahitaji ya kazi, ndoa, amani ya ndoa, walioshindikana kusoma, wazinzi, walevi. Lakini Leo ushuhuda mkuu ni magari na nyumba na hii hasa ni katika hayo makanisa ya kinabii na kitume.

Bora Tubaki katika imani zetu, naamini miujiza kama ni ya magari na nyumba itatukuta hukuhuku!!
 
Na anadai hana upendeleo katika kugawa magari!!
 
Anacheza Na Kiwango Chetu Kikubwa Cha USHAMBA na UJINGA Hivyo Acheni tu Ajipigie Na Bado Watamkoma Zaidi.
 
Pale kuna upako wa magari tu na kukosoa watumishi wengine ila hakuna Injili ya kupeleka watu Mbinguni.
Kuwatambua hawa jamaa unahitaji Neema ya Mungu.
 
Haha sijawahi kumsikia huyo jamaa anakemea dhambi wala kuhubiri real gospel ya kupeleka watu mbinguni haya Acha watu wapate magari na kusahau ufalme wa Mungu huyo jamaa sio Mtume wa Mungu prosperity Gospel hamfurahishi Mungu Bali Salvation Gospel ndo ya kumfurahisha Mungu

Kaeni chonjo

kuzimu kumekekwa Bond

Ni nyakati za mwisho
 
Back
Top Bottom