Kwa mwendo anaokwenda nao Rais Magufuli, upinzani unakufa kifo kitakatifu.

waliondoka watu wenye influence kama akina slaa, zitto ila chama kiliendelea kuwa imara hawa bavicha kwanza mi binafsi nilikuwa siwajui, kafulila nilijua yupogo shamban...

anaimarisha upinzan bila kujua....
 
Wanabodi,

Hili ni bandiko la swali, kufuatia hii hama hama ya wapinzani kuhamia CCM, Jee rais Magufuli Anaimarisha CCM kwa kujenga CCM imara, Au Anaua Upinzani na kulifanya taifa tunaelekea Nchi ya Chama Kimoja?. Nini Mustakabali wa Upinzani TZ?.

Naendelea kutafakari hii hama hama ya wanachama wa upinzani kuhamia CCM, jee hama hama hii ni kwa sababu rais Magufuli anajenga CCM imara, au CCM ni ile ile, kinachofanyika ni Magufuli kuua upinzani, kwa viongozi wa upinzani kumkubali sana Magufuli, hadi kuamua kuachana na vyama vyao na kujiunga na CCM, kumfuata Magufuli, ili wamsaidie kutimiza azma yake kuiletea Tanzania maendeleo?, ama ni kweli kuna fedha zinatembea kuwanunua viongozi wa upinzani wenye njaa, hivyo kulielekeza taifa letu kurejea kwenye mfumo wa chama kimoja kwa mlango wa nyuma?.

  1. Jee CCM imara, ina maana gani kwa mustakabali wa upinzani Tanzania?.
  2. Jee kuna uukweli kuwa rais Magufuli hana nia njema na upinzani Tanzania, ndio maana alisema kamwe hatateua wapinzani kwenye serekali yake?.
  3. Uteuzi wa Mama Anna na Prof. Kitila, ni uteuzi wa hongo ili kuisambaratisha ACT, na sasa kazi kuisambaratisha Chadema, ndio imeanza?.
  4. Jee ni kweli Viongozi wa upinzani wanaohamia Chadema, wamenunuliwa?.
  5. Jee katazo la rais Magufuli kuzuia maandamano na mikutano ya kisiasa ya kitaifa, inawezekana halina nia njema na upinzani?.
  6. Jee ni kweli rais Magufuli, anaendelea kutumia rasilimali za taifa kuitangaza CCM katika mikutano ya kiserikali, au ya kichama inayofanyikia kwenye venue za serikali, hivyo kugharimiwa kwa fedha za umma?.
  7. Kama katiba ya nchi, rais Magufuli aliyoapa kuilinda, inaruhusu mikutano ya kisiasa, lile katazo lake kuzuia mikutano hiyo, lina maana gani kwa mustakabali wa upinzani Tanzania.
  8. What does Mhe. rais Magufuli stand to loose kama ataruhusu shughuli za kisiasa nchini kuendeshwa kwa mujibu wa katiba?. Yaani anapata nini kuzuia mikutano?.
  9. Kwa watu wenye uwezo wa kosoma nia njema iliyoko ndani ya moyo wa mtu kupitia facial expressions mtu anapozungumza, jee kuna nia jema kuhusu upinzani nchi Tanzania katika awamu hii?.
  10. Kwa vile upinzani nchini Tanzania, upo kwa mujibu wa katiba, jee mtu yoyote mwenye nia ya kuudhoofisha upinzani nchini Tanzania, ana nia njema kweli na taifa hili?. Inawezekana kwa mtu kuwa na nia njema na maendeleo ya taifa, at the same time, ukafifisha demokrasia kwa kudhoofisha upinzani?.
My Take.
Kazi ya upinzani Zaidi ya kutaka kwenda ikulu, pia kuisimamia serikali kule bungeni kupitia mawaziri mbadala, kusimamia matumizi ya fedha za umma kupitia oversight committee, ili kujihakikishia serikali inasimamiwa ipasavyo, Tanzania tunahitaji kuwa na upinzani imara, kama juhudi za rais Magufuli katika vita dhidi ya rushwa, uzembe, ubadhirifu na ufisadi, matokeo yake ni kuua upinzani, kwa wapinzani kukosa hoja za kuendelea kuwa wapinzani, hivyo kuamua kujiunga na CCM kumsaidia Magufuli, jee ni nini mustakabali wa Tanzania yenye upinzani hafifu?.

Jee Tumeanza safari ya kuelekea nchi ya chama kimoja cha siasa?, na uchaguzi wa rais 2020, utakuwa ni uchaguzi wa rais kweli au litakuwa ni igizo tuu la uchaguzi, lakini rais wa Tanzania hadi 2025, ni Dr. John Pombe Joseph Magufuli?. If this is case for 2020, kwa umasikini wetu nchini Tanzania, do we real need to spend so much kufanya igizo hili?. Kwa Kasi hii ya Magufuli, kuna haja Kufanya Uchaguzi wa Rais 2020 ...

Wasalaam.

Paskali
upinzani unajiua wenyewe kwa kudakia mambo yasio ya msingi kipindi cha kikwete sio kweli kuwa upinzani ulifanya vizuri bali perfomance ya serikali ya JK kutokuwa sirias hasa kwenye swala la rushwa .na ndo kilichofsnya ccm ichokwe kila kona
 
Kinachofanyika sasa ni kuiporomosha demokrasia Na ni uoga wa ccm Na pia uoga wa baadhi ya viongoz Na makada wa mpinzani. Kivipi ni uoga wa ccm ni Kwa sababu wanatumia nguvu kubwa sana kuwarudisha nyuma upinzan Kwa kutumia jeshi la police fursa za uongozi serikali Na mamlaka zote za serikali.mfano wa kwanza utaona namna serikali ilivyozuia wigo sawa wa Kufanya siasa Kwa kuzuia mikutano ya siasa hadi uchaguzi Na Kama unavyojua jukwaa pekee la Kufanya siasa Kwa wapinzani ni mikutano ya hadhara. Pili kuzuia vyombo vya habari kuwapa coverage wapinzani.tatu ukiangalia bungeni namna wabunge wa upinzan wanavyotendewa ni Kama wahalifu au watu wasio Na maana ingawa wamechaguliwa Na wananchi kuwawakilisha bungeni. Na ukija ktk upande wa pili wa vyama vya upinzan ni kwamba baadhi ya viongoz wao ama wanaojiita makada ni watu ambao hawana ule wito wa siasa ni watu wanaofanya siasa ili wapate jukwaa la kuonekana kisha waweze kutimiza malengo yao ya kujikusanyia fursa za maisha Na vyeo serikalini .njia moja ya ccm kuzika vyama vya upinzan ni kutoa huduma za kijamii Bora Na kuboresha miundombinu afya Na elimu kinyume chake ni kwamba unajitekenya mwenyewe Na kucheka mwenyewe sawa viongoz Na makada wanatuangusha ama kwa kukata tamaa au kutetea maslahi yao but uchumi wa nchi utaonyesha Kwa wananchi nn serikali imefanya sasa hapo ndyo balaa lake litakapoanza kwan Hali mbaya ya uchumi Na huduma mbovu za afya Na elimu ndizo zitapelekea wananchi kuingia barabaran sasa itakuwa vita ya wananchi wenyewe Na serikali yao hvyo vyama vya upinzan vitakaa pembeni Na kuangalia tu
 
pascal ndugu yangu ccm watatawala muda mrefu sana , hakuna chama chenye nguvu kuwatoa ccm
wapinzani awana msimamo wanaingia na kutoka kama wanaingia chooni

Unaweza kuwa sahihi, hata mm pengine naweza(kwa makosa kabisa kusema/kufikiri hivyo. Lakini nasutwa na swali hili, mpinzani ni nani huyo tunaemtegemea? Mimi ni upande wa upinzani, he nimefanya nn?, yatosha kutamani tu? Nani kama siyo mm?
Tatizo ni kubwa kuliko tunavodhani. Kila MTU anategemea Fulani afanye!
 
Haimarishi CCM na wala haui upinzani. Kifupi. Asilimia kubwa kama si wote wanaoenda CCM, ama wanashawishiwa kwa ahadi ya au pesa ama vyeo, na pengine kutaka kuhurumiwa katika shughuli afanyazo mtu. Sasa CCM haiwezi kujengwa kwa kuwapa asante wanaohamia huku kuna wanachama wengi ambao kwa muda mrefu wametumika chamani kwa bidii na uaminifu na bila kudai au kupewa malipo. Kuhusu upinzani hauwezi kuuawa kwa kuwarubuni wanachama ambao kwa kweli si kuwa wanarubunika kwa sera za CCM, bali kwa aina fulani ya rushwa, ambayo kwa maoni yao inawasaidia kutatua shida zao za kimaisha, ikiwamo njaa. Kwa wale wanaohamia upinzani, huwa hakuna ahadi ya kupewa chochote. Na hata kama ahadi itakuwepo, ni ile ya kupiga kazi bila malipo, ambayo kwa kweli ni wale tu wenye msimamo na maamuzi binafsi ndiyo wanao weza kuhamia upinzani. Kwa maoni yangu mimi, CCM lazima tu itakufa, kwa sababu zifatazo. Kwanza CCM haina sera. Ndiyo maana kila mwana CCM hawezi ongea kitu bila kumtaja Magufuli. Kwa hiyo CCM haina sera kwa sasa. Sera ni Magufuli. Pili Magufuli alishasema CCM kuna majizi hivyo hategamei CCM. Ndiyo maana hata wakati wa kampeni alijinadi kama Magufuli, na ndiyo maana hakuwa anatumia nembo ya chama, alikuwa na nembo yake "M" yenye mwenge katikati. Pia siku hizi ni nadra sana kusikia serikali ya CCM, si kwenye chama wa serikalini, wote wanasema serikali John Pombe Magufuli. Hivyo kwa maoni yangu, tofauti ya CCM na CHADEMA ni kuwa CCM ni Magufuli na CHDEMA ni Taasisi yenye sera ambayo ni wale tu wenye imani na sera ndiyo wanajiunga. Na kwa kuwa CHADEMA ni Taasisi, haiwezi kufa kamwe, japo kweli inaweza kuyumba, lakini ikaimarika zaidi.
 
Watu wanatamani bila kificho CCM ife, maswali kama vile haya huwa hayaulizwi pale akina Nyalandu wanapoipa kisogo CCM.

UPINZANI lazima uwe na mbinu mpya za kupambana na CCM mpya. Mbinu za kupambana na CCM ya JK haiwezi kutumika kwa JPM.

Kama vile Mrema na team yake ya NCCR walipoishiwa mikakati walisambaratishwa, the same will happen kwa team Mbowe.

They have to change with changes ELSE wanapotea

JPM nje ya urais wake yeye ni mwenyekiti wa ccm. Kama mkuu wa chama hawezi kuacha kukipambania chama chake eti kwa kisingizio kuwa ni rais, urais kwake ni advantage na ndio maana kila chama kinaingia gharama kubwa kuutafuta. Ccm kuwa na nguvu kubwa kwake JPM ni credit.

Si wajibu wa ccm kuufanya upinzani uwe na nguvu. Ni wajibu wa upinzani kuwa wabunifu kimkakati kujijengea nguvu.

Wanaoua upinzani ni viongozi wa kitaifa wa upinzani. Kwa sababu ya ubinafsi, upendeleo na kukosa dira.

Upinzani umekuwa na visingizio kila kukicha. Madiwani wao hawafanyi kazi, wabunge wao hawafanyi kazi uongozi wa chama ndo kabisaaa.

Wanasema rais hataki kukosolewa ila wao jaribu kuwakosoa uone. Sasa bado hawajashika dola hawaendi kukosolewa je wakiingia ikulu itakuwaje.

Upinzani huu wa sasa ni budi uondoke uje upinzani mpya. Vinginevyo lazima kuwe na mageuzi makubwa ndani ya upinzani. Hawa akina Mbowe walioshindana na awamu mbili zilizopita wakae pembeni wapishe wengine waanze na huyu wa awamu mpya ya tano. Vinginevyo tutaendelea na mbinu za mchangani kwenye uwanja wa nyasi. Matokeo ni kugaragazwa tu.
 
CCM walichanga karata zao vizuri mwaka 2015 na walizachanga kwa maslahi ya umma huku chadema wakichanga karata zao kwa maslahi ya chama na wanachama wachache.
 
Comrade Pascal Mayalla, kwa sasa Tanzania hakuna upinzani kilichobaki ni ubabaishaji tu. Mbowe anauliwa kisiasa na asipo angalia atajikuta yuko pekee akiwa na machungu na wewe pamoja na sie tusio na umuhimu kwake. Magufuli is killing them softly.
 
CCM wana Serikali na dola, wana ahadi ambazo wametoa kwa wananchi, kuimarika kwa CCM kutatokana na kuwaletea wananchi maendeleo na wala si maigizo ya kuhamisha baadhi ya watu kutoka upinzani, badala yake wanapaswa kushughulikia mambo ya msingi kama kuhuisha uchumi, huduma za afya na elimu.
 
hakuna wakuwatoa ccm madarakani never labda miaka 20 mingine kwa sasa hapana
wapinzani wana njaa , na hawana amani pia
 
Haimarishi CCM na wala haui upinzani. Kifupi. Asilimia kubwa kama si wote wanaoenda CCM, ama wanashawishiwa kwa ahadi ya au pesa ama vyeo, na pengine kutaka kuhurumiwa katika shughuli afanyazo mtu. Sasa CCM haiwezi kujengwa kwa kuwapa asante wanaohamia huku kuna wanachama wengi ambao kwa muda mrefu wametumika chamani kwa bidii na uaminifu na bila kudai au kupewa malipo. Kuhusu upinzani hauwezi kuuawa kwa kuwarubuni wanachama ambao kwa kweli si kuwa wanarubunika kwa sera za CCM, bali kwa aina fulani ya rushwa, ambayo kwa maoni yao inawasaidia kutatua shida zao za kimaisha, ikiwamo njaa. Kwa wale wanaohamia upinzani, huwa hakuna ahadi ya kupewa chochote. Na hata kama ahadi itakuwepo, ni ile ya kupiga kazi bila malipo, ambayo kwa kweli ni wale tu wenye msimamo na maamuzi binafsi ndiyo wanao weza kuhamia upinzani. Kwa maoni yangu mimi, CCM lazima tu itakufa, kwa sababu zifatazo. Kwanza CCM haina sera. Ndiyo maana kila mwana CCM hawezi ongea kitu bila kumtaja Magufuli. Kwa hiyo CCM haina sera kwa sasa. Sera ni Magufuli. Pili Magufuli alishasema CCM kuna majizi hivyo hategamei CCM. Ndiyo maana hata wakati wa kampeni alijinadi kama Magufuli, na ndiyo maana hakuwa anatumia nembo ya chama, alikuwa na nembo yake "M" yenye mwenge katikati. Pia siku hizi ni nadra sana kusikia serikali ya CCM, si kwenye chama wa serikalini, wote wanasema serikali John Pombe Magufuli. Hivyo kwa maoni yangu, tofauti ya CCM na CHADEMA ni kuwa CCM ni Magufuli na CHDEMA ni Taasisi yenye sera ambayo ni wale tu wenye imani na sera ndiyo wanajiunga. Na kwa kuwa CHADEMA ni Taasisi, haiwezi kufa kamwe, japo kweli inaweza kuyumba, lakini ikaimarika zaidi.
Ninakubaliana na wewe! Huwezi kuimarisha chama kwa kununua watu kwa pesa na ahadi za vyeo. Watu wakununua hawawezi kujenga chama imara wala nchi. Na hii ni aina mbaya kabisa ya rushwa! Wanaonunua wapinzani na wale wanaonunuliwa hawana maadili yoyote....both are crooked....hawawezi kujenga mifumo...wanajijenga wenyewe...kwa masilahi yao..siyo ya nchi!

Kwa upande mwingine walioko kwenye vyama vya upinzani ni watu ambao wamejitoa mhanga na sadaka kupigania wanachokiamini....hakuna pesa wala deal huko...it is pure sacrifice! Wengi ni watu wamaadili mema.
 
Magufuli anatumia formula ya Mchezo wa karata (Last Card)

Ukiomba mavi ,kopa, shupaza hakupi... Anachofanya anasimamisha mchezo kwa namba saba,..... Sasa wapinzani wakaona njia pekee ni kutoa jokeri mapemaa kumlambisha Baba wawa watu..

Kumbe wakati wanamlambisha JPM akakamilisha kadi nne special....... Akawa stopisha, akatoa kopa, akaita akaita last card.... Wapinzani wakakosea tena wakaomba mavi, JPM akatoa kadi nne special mchezo ukaisha
 
Hata awanunuwe wote... Ila hali halisi ya Maisha ya Watanzania..... Na kuzidi kuzorota kwa uchumi..... Ndicho kitu pekee kinacho tufanya watanzania tuione CCM ni mavi.
 
Bora chama ki moja on China anavyoipeleka Mbio dunia kiuchumi, lakini watu kila siku wanailaumu haifuati utawala bora wa kuwatetea wezi wa Mali za umma.
kwani wanaoibia taifa ni upinzani?viongozi ndio wezi, china hakuna kulindana kama hapa kiongozi mwizi,lzm hatua zichukuliwe ndiyo maana wanaenda ingawa wezi wapo lkn wanashughurikiwa, ingekuwa china huyo nani visenti na wenzie wangeshakula kamba siku nyingi tu.
 
Nadhani kuna mpango unasukwa kwa sababu maalum.

Tusibeze tu, kunakitu.

Swali namba 5 ndio jibu. Mtumwenye nianjema lazma angefikiri kuhusu katiba maana ndio jamboambalo lingeweka kumbukumbu nzuri kwa vizazi.

Ngoja tu subiri kuona.
 
Back
Top Bottom