Kwa mshahara huu kweli nitaweza kujenga nyumba?

Kwa mshahara huu kweli nitaweza kujenga nyumba?

Hujategea mshahara na haupo dsm.
Ingetakiwa uwe na ghorofa bas

Ni kweli kabisa ndugu yangu ila nilikua na majukumu sana nilikua nawasaidia wadogo zangu ambao kwa sasa mmoja yupo Sudan kikazi jeshini na mwingine yupo Barclay bank na mimi kwa sasa namalizia master hapa dar University na pia nimenunua kiwanja kigamboni eneo la tungi.
 
Kaka huo mshahara ni mkubwa sana maisha ni mipango mimi nalipwa laki saba na kwa sasa nina nyumba ya room nne sebule iliogawanyishwa sehemu ya sitting room na dining vyoo viwili cha kwenye master na kimoja cha public na gari aina ya Toyota raum na nyumba nimepiga ukuta bado sijamalizia tu electricity fence ya mizunguko saba ya waya jipange fresh utaweza kaka

mmh mmhhhh wewe kweli unatenda muujiza..
 
Kaka huo mshahara ni mkubwa sana maisha ni mipango mimi nalipwa laki saba na kwa sasa nina nyumba ya room nne sebule iliogawanyishwa sehemu ya sitting room na dining vyoo viwili cha kwenye master na kimoja cha public na gari aina ya Toyota raum na nyumba nimepiga ukuta bado sijamalizia tu electricity fence ya mizunguko saba ya waya jipange fresh utaweza kaka

Lisilowezekana kwa mtanzania kwa fisadi lawezekana.michango lukuki msshuleni ni ya nani?
 
UMESEMA UNALIPWA:

mshahara 600,000/- (am assuming hii ndo take home)

MATUMIZI:

kodi 100,000/-
chakula 200,000/-
umeme 25,000/-
nauli 30,000/-

JUMLA: 355,000/-

BAKI MFUKONI KWAKO KWA ANASA NA KUHONGA TSH. 245,000/- (Hizi ukizitumia vyema unaweza kujenga bro)

HAKUNA uchawi wala ndumba... #inawezekana #anzaKubadilika wewe kwanza...
Huwezi kwa kujenga nyumba ya vyumba vinne na ukuta na gari kwa hiyo serving! I hiyo ni matofali 2,500, maximum, kila tofali 1000/-, cement mifuko 80, kila mfuko 12,000/- bati za mchina na roofing ni kama milion 15! Milango na mbao, grill na madirisha ya alminium ni kama milion 8, rangi kama milion 1, umeme installation na kuhonga tanesco mpaka ukufikie ni kama milion 2.5, kuchimba maji ya miundombinu yake ni kama 5 milion, chemba za maji taka na miundombinu yake, kama 1.6 milion, tiles kama decorations zingine!

Mkuu huwezi kujenge kwa hiyo salary... never on earth. Labda ka unaishi nje ya jiji na unakaa kwa wazazi, unaweza kujibana kwa miaka kadhaa ukapata kibanda, but not dream house....
 
Tunajenga, tunasomesha tena c st. Kayumba shule za ukweli, tunakula, na mke pia na magari tunakopea huo huo mshahara bila kusahau vistuli virefu every jioni.
 
Lisilowezekana kwa mtanzania kwa fisadi lawezekana.michango lukuki msshuleni ni ya nani?

Sasa mimi ukiniuliza kuhusu michango mashuleni sijui nikujibu nini maana mimi nilichukua bachelor ya wildlife na ndio naendelea na master yake ndugu yangu msshuleni michango sijui ni ya nani
 
Kaka huo mshahara ni mkubwa sana maisha ni mipango mimi nalipwa laki saba na kwa sasa nina nyumba ya room nne sebule iliogawanyishwa sehemu ya sitting room na dining vyoo viwili cha kwenye master na kimoja cha public na gari aina ya Toyota raum na nyumba nimepiga ukuta bado sijamalizia tu electricity fence ya mizunguko saba ya waya jipange fresh utaweza kaka

Ngastukaa, Machale kundesaa!
1. Lazima una chanzo kingine cha pesa AU....
2. Bado unakaa kwa ndugu AU...
3. Hivyo vitu umerithi AU...
4. unatumia usafiri wa UNGO kwenda kazini AU...
5. Chuma ulete!
 
Sasa mimi ukiniuliza kuhusu michango mashuleni sijui nikujibu nini maana mimi nilichukua bachelor ya wildlife na ndio naendelea na master yake ndugu yangu msshuleni michango sijui ni ya nani

Nilihofu isije ikawa wewe ni mnufaika wa hiyo miradi ndugu yangu.Hongera endelea kukaza buti.
 
Tumia pesa kutengeneza pesa hakikisha unakua risk taker ndugu yangu wekeza kwenye vitu vingine kama mimi nimekuambia nalima kilimo cha kisasa, na Solon za kike mbili na duka kubwa lenye mpesa pia na nagari la kutembelea na nipo kazini hakuna miujiza wala ushirikina usiudumaze upongo wako ndugu jishugulishe ndio maisha yalivyo
 
Kikwete ameshusha cement toka 16,000 mpaka 8000..Magufuli atashusha bei ya nondo, matofali, mabati, mbao, misumari....utajenga nyumbayako ndani ya mwaka kwa huohuo mshahara
 
Kikwete ameshusha cement toka 16,000 mpaka 8000..Magufuli atashusha bei ya nondo, matofali, mabati, mbao, misumari....utajenga nyumbayako ndani ya mwaka kwa huohuo mshahara

Jaman hii nitaipata wapi ya 8000!
I real need it jaman niko mbeya kwa sasa!
Msaada mkuu!
 
Mkuu ili ujenge inatakiwa ujitahidi kuanzisha vyanzo mbadala vya kujiongezea kipato,mf.ufugaji,kilimo cha bustani za mbogamboga,biashara ndogondogo,n.k.
 
Tunajenga, tunasomesha tena c st. Kayumba shule za ukweli, tunakula, na mke pia na magari tunakopea huo huo mshahara bila kusahau vistuli virefu every jioni.

Kweli mkuu jambo la msingi ni kuishi kwa bajeti ili uweze kufikia malengo.
 
ni kwel maisha ni mipango unaweka angalau kwa mwaka nimalize msingi mwaka mwigine nifikie lenta mdogo mdogo
 
Kaka huo mshahara ni mkubwa sana maisha ni mipango mimi nalipwa laki saba na kwa sasa nina nyumba ya room nne sebule iliogawanyishwa sehemu ya sitting room na dining vyoo viwili cha kwenye master na kimoja cha public na gari aina ya Toyota raum na nyumba nimepiga ukuta bado sijamalizia tu electricity fence ya mizunguko saba ya waya jipange fresh utaweza kaka

Acha porojo, sema unaweza kutumia mshahara kupata mikopo, sio mshahara per se ufanye hayo! Sema una bishara unafanya, sio mshahara per se ufanye hayo uliyoyasema
 
lazima utakuwa mwizi...halafu ooohh lowasa fisadi!!!

Mwizi wewe usiyejua kujipanga, mimi nimejenga nyumba kama hiyo na mshahara wa laki tatu kwa mwezi, tena kwenye kampuni ya wahindi ambapo ni wagumu huwezi iba hata mia
 
Back
Top Bottom