Kwa mheshimiwa rais kikwete tu

Kwa mheshimiwa rais kikwete tu

Jumakidogo

R I P
Joined
Jul 16, 2009
Posts
1,851
Reaction score
427
Habari za kazi mheshimiwa Rais, pole sana na majukumu pamoja na visafari vya hapa na pale. Sielewi nikusalimie kwa salamu ipi, lakini bila shaka shikamoo itafaa zaidi. Mimi ninaye kuandikia barua hii ni raia wa kawaida sana. Ni mtu wa mtaani tu kama walivyo watanzania wengine.

Nimekuandikia kupitia hapa kwa sababu sina namna nyingine kufikisha ujumbe wangu kwako. Naamini kwa njia hii, maneno yangu yatakufikia huko uliko.

Mheshimwa, sidhani kama unatambua kuwa, hivi sasa watanzania tuna matatizo makubwa sana. Maisha yamekuwa magumu, ajira hakuna, thamani ya shilingi imeporomoka, maandamano kila kukicha, watu wasio na hatia wanaumizwa bila ya sababu, mfumuko wa bei kila baada ya masaa sita.

Imekuwa afadhali ya Zimbabwe na Somalia. Hata mishahara ya sisi walimu sasa imekuwa kama bahati nasibu. Hayo ni machache tu, lakini kuna mengi zaidi ambayo hayaandikiki. Pamoja na yote hayo, umekuwa kimya sana. Kimya kama kifaranga kilicho ndani ya yai.

Waswali wanasema; kukaa kimya ni namna moja nzuri ya kumpuuza anayekupigia kelele. Lakini kumbuka kuwa, kimya kingi, kina mshindo mkuu.

Moja ya mfano wa mshindo huo, ni kile kilichotokea Mbeya. Hata ukiwa kimya, ni imani yangu kuwa ujumbe na maneno ya watanzani unayasikia kwani hata mabango barabarani hayaongei, lakini watu wakisoma wanaelewa.

Wakati unaingia madarakani, mimi ni mmoja wa watu waliokupigia kura japo itikadi zetu kisiasa ni tofauti. Lakini mpaka sasa sijafaidika na chochote katika utawala wako. Labda cha maana nilichofaidika nacho ni kuacha pombe.

Nimeacha kwa sababu hali imekuwa ngumu na kulazimika kupunguza matumizi yasiyo ya lazima. Unajua kuwa umaarufu wako uliotuka sasa unabalika? Watu wanaona kuwa unawatesa sasa, wengi wanaona kuwa umewageuka.

Vijiweni jina lako limekuwa ndiyo agenda kuu kwa sasa. Naomba ujitokeze utupe japo maneno ya kutufariji tu ili mioyo yetu iburudike na kurejewa na matumaini.

Mengi yametokea, lakini binafsi napenda sana wanyama wa porini. Hivi ni nani aliyeswaga wale twiga kutoka porini na kuwapakia katika ile ndege?

Mpaka sasa waliohusika wamechukuliwa hatu gani? Halafu walikuwa twiga ndama au? Manaake nadhani kumswaga twiga mzee ni kazi kubwa sana.

Mwisho naomba ujue kuwa, wananchi hali zetu ni mbaya sana kwa sasa. Tunahitaji msaada. Nashukuru sana kwa ukarimu wako..Ni mimi raia mwema.

Naishi Mbezi hapa Dar es salaam.
 
Sikubaliani, kama ni msaada nenda kwa Cameroun anatoa lakini kuna masharti
 
atasoma lakini hawezi kuelewa'uwezo wa kuelewa hautokani na degree mkuu'
 
hayo malalmiko yako yote yana wizara zake. Peleka huko, usituletee unafiki hapa.
 
Uh,anaweza akataka kujua mbez bichi au ile ya m0ro rod?
 
Ukome kabisa, me kura yangu ckumpa huyo ndugu yake na cameroon, me nilizisoma alama za nyakati toka kipindi kile anagombea ukuu wa kaya, hahahahahahaha kumbe ka elimu kangu ka standard 7 kananisaidiaga kuona mbali? Thanx God.
 
mmmmh huyu jamaa hata tv sidhani kama anaangalia, je hii barua atasoma??
 
mmmmh huyu jamaa hata tv sidhani kama anaangalia, je hii barua atasoma??
Kwa Jk ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa ukitegemea ataelewa afurahi na kuanza kucheza!
 
ha ha ha ha haaaa pole sana ndgu yangu... kwamba faida uliyopata sana sana ni kuacha pombe kutokana na ugumu wa maisha
 
hayo malalmiko yako yote yana wizara zake. Peleka huko, usituletee unafiki hapa.
Omr unapotoa ushauri, inabidi umfahamishe maana hafahamu, kwa mfano ugumu wa maisha wa wananchi apeleke malalamiko wizara gani?

Unakumbuka kwamba Kikwete aliahidi maisha bora kwa kila Mtanzania? Kwanini hiyo kauli asiiachie Wizara husika? Omr Tanzania tupo katika wakati mgumu sana kutokana na kuwa na ombwe la uongozi hata kama wewe Omr binafsi unafaidika na hili Tatizo la uongozi usipende kujitokeza mbele kiasi hicho.

Kaa kimya kula bata kimya kimya kama Wahindi wanavyokula bata kariakoo kimya kimya kutokana na udhaifu wa ukusanyaji kodi hapa nchini.

Ni ushauri tuu.
 
Mkuu msg yako imetulia sana, nakushauri uipost kwenye baadhi ya magazeti ili watu wengi waione. Hlf nipe ruhusa niipeleke kwenye wall facebook yake maana ni friend of mine.
ASANTENI JAMANI NGOJA NIRUDI DARASANI NAONA TICHA ANAINGIA.
 
msg nzuri sana ila ni ngumu sana kuielewa kwa mtu jk,ufahamu wake sidhani km ataambulia kitu hapa,utaona km atakujibu!!!
mi nadhani ili kumvutia ungeongeza yafuatayo
-mialiko mingapi inatoka kwa cameroon
-obama anamuhitaji lini
-km kuna bembea mpya zimetengenezwa
-km babu seya ametoka jela
-uhusiano wa liyumba na vick-shika umeisha
-migodi mingapi inahitaji kukabidhiwa kwa marekani kwa ubia na yeye

tofauti na hapo sidhani km atakuelewa
 
Nyie wote wanafiki tu, mnasogeza muda siku iishe.
 
Back
Top Bottom