kwa mfano huu kuna bado kuna mtu atatetea ujamaa?

Sexer

JF-Expert Member
Oct 22, 2014
8,216
7,907
Profesa wa Uchumi wa Chuo Kikuu kimoja alizungumza darasani kwamba hakuwahi kufelisha mwanafunzi hata mmoja, hata hivyo wakati huu Darasa zima lilikua limefeli.

Darasa lilikua limejibu mtihani kuwa Ujamaa ni itikadi muafaka ya kichumu ya kuleta usawa, chini ya ujamaa hakuna tajiri wala masikini.

Profesa akataka darasa lizijaribu kanuni za kijamaa kwenye mtihani.

Kwamba alama watakazopata wanadarasa wote zitagawiwa kwa usawa baina yao; hakuna atakaefeli wala hakuna atakae pata alama 'A'.

Baada ya mtihani kila mwanafunzi alipata alama 'B'.
Waliojiandaa sana na mtihani walichukia, wakati ambao walijiandaa kiasi tu walifurahi.

Mtihani wa pili ulipokuja wale waliojiandaa kidogo wakajiandaa kidogo zaidi na wale ambao awali walijiandaa sana, wakati huu hawakujiandaa vilivyo kwani nao hawakutaka kujisumbua.

Matokeo ya wastani yakawa alama 'D'. Na hakuna aliyefurahia!

Ulipokuja mtihani wa 3 matokeo yakawa 'F'

Jaribio lilivyoendelea na matokeo yakawa mabaya zaidi, wanafunzi wakalaumina na kuitana majina mabaya. Hakuna aliekua tayari kusoma kwa faida ya mwingine.

Kwa Mshangao mkubwa wote wakafeli, na profesa akawaambia hatimaye Ujamaa pia utafeli kwakua pale malipo yanapokua makubwa na jitihada za kufanikiwa zinaongezeka. Lakini pale ambapo Serikali inafuta malipo yote hakuna atakae jaribu kufanikiwa.

Pengine hizi ndio sentensi 5 zinazotawala jaribio hili.

1. Huwezi wafikisha masikini kwenye mafanikio kwa kuwaondoa matajiri kwenye mafanikio.

2. Kile ambacho mtu analipwa bila kukifanyia kazi, kuna mtu amekifanyia kazi bila kulipwa.

3. Serikali haiwezi kumlipa mtu kitu, ambacho serikali hiyo haijampora kitu hicho mtu mwingine.

4. Huwezi uzidisha utajiri kwa kuugawanya.

5. Pale ambapo nusu ya watu wanaona hakuna haja ya kufanya kazi kwakua kuna nusu ya watu wanafanya kazi kwa ajili yao. Na pale wanaofanya kazi wakiona kwamba hawana sababu ya kufanya kazi kwakua watu wengine watafaidika na kazi zao; huo ndio unakua mwanzo wa mwisho wa Taifa.
 
  • Thanks
Reactions: wax
Profesa wa Uchumi wa Chuo Kikuu kimoja alizungumza darasani kwamba hakuwahi kufelisha mwanafunzi hata mmoja, hata hivyo wakati huu Darasa zima lilikua limefeli.

Darasa lilikua limejibu mtihani kuwa Ujamaa ni itikadi muafaka ya kichumu ya kuleta usawa, chini ya ujamaa hakuna tajiri wala masikini.

Profesa akataka darasa lizijaribu kanuni za kijamaa kwenye mtihani.

Kwamba alama watakazopata wanadarasa wote zitagawiwa kwa usawa baina yao; hakuna atakaefeli wala hakuna atakae pata alama 'A'.

Baada ya mtihani kila mwanafunzi alipata alama 'B'.
Waliojiandaa sana na mtihani walichukia, wakati ambao walijiandaa kiasi tu walifurahi.

Mtihani wa pili ulipokuja wale waliojiandaa kidogo wakajiandaa kidogo zaidi na wale ambao awali walijiandaa sana, wakati huu hawakujiandaa vilivyo kwani nao hawakutaka kujisumbua.

Matokeo ya wastani yakawa alama 'D'. Na hakuna aliyefurahia!

Ulipokuja mtihani wa 3 matokeo yakawa 'F'

Jaribio lilivyoendelea na matokeo yakawa mabaya zaidi, wanafunzi wakalaumina na kuitana majina mabaya. Hakuna aliekua tayari kusoma kwa faida ya mwingine.

Kwa Mshangao mkubwa wote wakafeli, na profesa akawaambia hatimaye Ujamaa pia utafeli kwakua pale malipo yanapokua makubwa na jitihada za kufanikiwa zinaongezeka. Lakini pale ambapo Serikali inafuta malipo yote hakuna atakae jaribu kufanikiwa.

Pengine hizi ndio sentensi 5 zinazotawala jaribio hili.

1. Huwezi wafikisha masikini kwenye mafanikio kwa kuwaondoa matajiri kwenye mafanikio.

2. Kile ambacho mtu analipwa bila kukifanyia kazi, kuna mtu amekifanyia kazi bila kulipwa.

3. Serikali haiwezi kumlipa mtu kitu, ambacho serikali hiyo haijampora kitu hicho mtu mwingine.

4. Huwezi uzidisha utajiri kwa kuugawanya.

5. Pale ambapo nusu ya watu wanaona hakuna haja ya kufanya kazi kwakua kuna nusu ya watu wanafanya kazi kwa ajili yao. Na pale wanaofanya kazi wakiona kwamba hawana sababu ya kufanya kazi kwakua watu wengine watafaidika na kazi zao; huo ndio unakua mwanzo wa mwisho wa Taifa.
Mwenyezi Mungu alimpa Ibrahim mali nyingi na mifugo mingi.
 
Back
Top Bottom