Kwa kuwa sheria ya kunyongwa hadi kufa haitekelezwi, kwanini isifutwe?

sem2708

JF-Expert Member
Nov 4, 2010
5,204
4,211
Jana mkuu kasema hatatekeleza adhabu ya kunyongwa kwa watu walopewa hukumu hiyo, sasa nashauri sheria hii ifutwe badala ya kila anayekuja kuipotezea... ugumu uko wapi kuifuta sheria hii?
 
Amezuia utekelezaji wa sheria hiyo kwa kipindi chake lakini huenda labda atakaemfuatia akaitumia. Hivyo unaposema ifutwe sio sawa.
 
Jana mkuu kasema hatatekeleza adhabu ya kunyongwa kwa watu walopewa hukumu hiyo, sasa nashauri sheria hii ifutwe badala ya kila anayekuja kuipotezea... ugumu uko wapi kuifuta sheria hii?
Mimi hapo nyuma nimewahi kuuliza kuna umuhimu gani wa kuomba ridhaa Ikulu kwa hukumu iliyotolewa na mahakama?! Mahakama ikihukumu mtu kunyongwa kwanini sheria ilazimishe hadi idhini ya rais ndiyo hukumu itekelezwe? Huku si kuingilia uhuru wa mahakama?!

Hawa wahalifu wanaosubiri kunyongwa ni mzigo kwa taifa maana hawafanyi kazi yoyote gerezani. Ni kula na kulala.
 
Mimi hapo nyuma nimewahi kuuliza kuna umuhimu gani wa kuomba ridhaa Ikulu kwa hukumu iliyotolewa na mahakama?! Mahakama ikihukumu mtu kunyongwa kwanini sheria ilazimishe hadi idhini ya rais ndiyo hukumu itekelezwe? Huku si kuingilia uhuru wa mahakama?!

Hawa wahalifu wanaosubiri kunyongwa ni mzigo kwa taifa maana hawafanyi kazi yoyote gerezani. Ni kula na kulala.
Swali lako ni valid... ngoja wajuzi wa mambo watuelezee
 
Back
Top Bottom