Kwa kumroga Phiri asifunge tena wamefanikiwa, sasa wanakamilisha la Chama kuumizwa ili Simba SC idhoofike

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,551
108,888
Nikiwa na wao hujua GENTAMYCINE ni mwenzao (mwana Yanga SC) na bahati nzuri hawajui kuwa ndiyo mimi, hivyo huweza kupata mipango yao mingi ya siri na miovu dhidi ya Simba SC.

Taarifa niliyoipata na kuhakikishiwa kutoka Yanga SC ni kwamba, kwa kuona jinsi mchezaji Moses Phiri anavyokuja kasi na kuonekana ni tishio kwa ufungaji wameamua kumroga (kwa Kutumia Kitabu) kutoka kwa mtaalam (mganga wao mkubwa wa kisiwani Zanzibar) ili asifunge tena magoli na awe anakosa mno.

Na ni mganga huyu huyu ndiye aliyemuagua mshambuliaji wa Yanga SC Fiston Mayele msimu uliyopita katika mechi kadhaa alizokuwa na ukame wa magoli, baada ya Simba SC kumtumia mchezaji wa Namungo FC na mwana Simba SC lia lia Shizya Ramadhan Kichuya aibe jezi yake baada ya kumalizika kwa mechi yao pale Namungo mkoani Lindi msimu uliyoisha.

Taarifa za ndani (kutoka jikoni) kwa Yanga SC zinasema kuwa, kutokana na Simba SC kumuwahi kumtengeneza kindumba (kiuchawi) ili asidhurike na Yanga SC, mtaalam hatari wa Yanga SC kila akijaribu anadunda.

Sasa mchezaji tegemeo wa Simba SC Clatous Chota Chama ameandaliwa mkakati wa kuumizwa (kujeruhiwa) vibaya na timu pinzani ambazo zitahongwa na Yanga SC ili asicheze kabisa ligi, na Simba SC iweze kudhoofika pakubwa kwa kutokuwepo kwake.

Kama mwana Simba SC lia lia GENTAMYCINE, nauomba uongozi wa Simba SC uyachukue yote haya niliyoyaandika ya kuwahusu wachezaji muhimu raia wa Zambia Moses Phiri na Clatous Chama ili yote niliyoahidiwa kuwatokea yasitokee.

Na ikiwezekana upesi mno Phiri apelekwe kwa mtaalam wa Simba SC yule wa Morogoro (bibi) au aitwe Dar es Salaam yule wa Mkoani Rukwa, ili amuague vyema Phiri na ikiwezekana sasa awafanyie dawa ya kuwalinda wachezaji wote wa Simba SC dhidi ya kurogwa kwa kuhujumiwa na waganga wanaotumika na kutumwa na Yanga SC.

ONYO
Hakuna mahala popote pale GENTAMYCINE nimekulazimisha uusome huu uzi au uuamini, hivyo kama utaona kwako hauna maana tafadhali nakuomba pita tu na waachie watakaoulewa wachangie. Vinginevyo ukijipendekeza tu na kuwa na kiherehere tegemea majibu yangu umiza na chukizo, tena mubashara kabisa.

Nimemaliza.
 
Nikiwa nao Wao hujua GENTAMYCINE ni Mwenzao ( mwana Yanga SC ) na bahati nzuri hawajui kuwa ndiyo Mimi hivyo huweza kupata Mipango yao mingi ya SIRI na MIOVU dhidi ya Simba SC.
I agree with u, shida ni viongozi wetu ukisema ya ukweli kama haya wanaona kama unaleta usanii wakati unaongea facts, Phiri angeondoka na mpira vs Ruvu lkn ukosaji wake mabao ulinifanya niamini kuwa he must be bewitched.
 
Huyo bibi wa mrogoro namjua ila sasa kwenye rozari tunakuwa naye
 
Huyo bibi wa mrogoro namjua ila sasa kwenye rozari tunakuwa naye
Huyo (Huyu) Bibi kwa sasa anatumiwa mno na Wachezaji wa Simba SC na Yanga SC watokao (wanaotoka) Mkoani Morogoro wakiongozwa na Mkali Wao Kipa wa Simba SC Aishi Manula na Kiungo Mzamiru Yassin huku kwa Yanga SC wakiwa ni Dickson Job ( Dogo wa Misufini Morogoro ) na Kibwana Shomary.
 
I agree with u, shida ni viongozi wetu ukisema ya ukweli kama haya wanaona kama unaleta usanii wakati unaongea facts, Phiri angeondoka na mpira vs Ruvu lkn ukosaji wake mabao ulinifanya niamini kuwa he must be bewitched.

Sent from my SM-F916B using JamiiForums mobile app
GENTAMYCINE huwa sileti Jambo la Uwongo au nisilo na uhakika nalo hivyo nakuomba amini na niamini tena kwa 100% zote haya niliyoyaandika hapa.

Mwisho nikuombe na niwaombeni tafadhalini Watumieni ( Share ) huu Uzi wangu na Viongozi Waandamizi wote wa Simba SC ili waupokee na waufanyie Kazi kwa haraka sana kwani ni Mipango iliyoko na imeshafanyika.
 
Kapombe umemsahau alisaidiwa sana na yule bibi
Shida Kubwa (Kuu) ya Beki Shomary Kapombe siyo Kurogwa kama anavyoamini na kutaka Kutulazimisha tuamini.

Ukweli ni kwamba Beki Shomary amedanganya Umri hivyo hata akiwa anapelekwa Kutibiwa hudanganya Umri wake hivyo kupewa Dawa zisiondana na Uhalisia Kamili wa Ujeba (Umri) wake mkubwa.

Na hata Kapteni Mstaafu wa JWTZ na mwana Simba SC lia lia na Mafia wa Soka la Tanzania na Afrika Marehemu Zacharia Hanspoppe 'Mapama' aliwahi Kumtolea Uvivu kwa Kumsema (Kumchana) juu ya tabia yake ya Kudanganya Umri iliyofanya awe anapewa Dawa zisizomfaa na Kuchelewa kupona Majeraha.
 
Sasa shida chama huwa ni ngumu kumuumiza..ukitaka kumvaa atakupa chenga mpaka uchanganyikiwe(kuna mchezaji wa ruvu juzi alikula chenga akajikuta chini, lengo lake lilikuwa ni kumvaa chama).

Na kwenye uchawi,naskia hawa wazambia ndio wenyewe,yaani hawa kina chama ni magwiji huko kwao Zambia.

Njia pekee ni kufika miguuni tu kwa chama,physical manake kiuchawi sijui kama watamuweza.
 
Mkuu we ni konyoniliangalia mechi ya simba na ruvu juzi nikawa nasubiri kwa hamu goli la phiri ila wapi!!!NILIJUA PALE KUNA KITU SIO BUREEE!!!nakukubali sana we mzee
Thanks for the sincere Credits Chief. Be blessed.
 
Nikiwa na wao hujua GENTAMYCINE ni mwenzao (mwana Yanga SC) na bahati nzuri hawajui kuwa ndiyo mimi, hivyo huweza kupata mipango yao mingi ya siri na miovu dhidi ya Simba SC.

Taarifa niliyoipata na kuhakikishiwa kutoka Yanga SC ni kwamba, kwa kuona jinsi mchezaji Moses Phiri anavyokuja kasi na kuonekana ni tishio kwa ufungaji wameamua kumroga (kwa Kutumia Kitabu) kutoka kwa mtaalam (mganga wao mkubwa wa kisiwani Zanzibar) ili asifunge tena magoli na awe anakosa mno.

Na ni mganga huyu huyu ndiye aliyemuagua mshambuliaji wa Yanga SC Fiston Mayele msimu uliyopita katika mechi kadhaa alizokuwa na ukame wa magoli, baada ya Simba SC kumtumia mchezaji wa Namungo FC na mwana Simba SC lia lia Shizya Ramadhan Kichuya aibe jezi yake baada ya kumalizika kwa mechi yao pale Namungo mkoani Lindi msimu uliyoisha.

Taarifa za ndani (kutoka jikoni) kwa Yanga SC zinasema kuwa, kutokana na Simba SC kumuwahi kumtengeneza kindumba (kiuchawi) ili asidhurike na Yanga SC, mtaalam hatari wa Yanga SC kila akijaribu anadunda.

Sasa mchezaji tegemeo wa Simba SC Clatous Chota Chama ameandaliwa mkakati wa kuumizwa (kujeruhiwa) vibaya na timu pinzani ambazo zitahongwa na Yanga SC ili asicheze kabisa ligi, na Simba SC iweze kudhoofika pakubwa kwa kutokuwepo kwake.

Kama mwana Simba SC lia lia GENTAMYCINE, nauomba uongozi wa Simba SC uyachukue yote haya niliyoyaandika ya kuwahusu wachezaji muhimu raia wa Zambia Moses Phiri na Clatous Chama ili yote niliyoahidiwa kuwatokea yasitokee.

Na ikiwezekana upesi mno Phiri apelekwe kwa mtaalam wa Simba SC yule wa Morogoro (bibi) au aitwe Dar es Salaam yule wa Mkoani Rukwa, ili amuague vyema Phiri na ikiwezekana sasa awafanyie dawa ya kuwalinda wachezaji wote wa Simba SC dhidi ya kurogwa kwa kuhujumiwa na waganga wanaotumika na kutumwa na Yanga SC.

ONYO
Hakuna mahala popote pale GENTAMYCINE nimekulazimisha uusome huu uzi au uuamini, hivyo kama utaona kwako hauna maana tafadhali nakuomba pita tu na waachie watakaoulewa wachangie. Vinginevyo ukijipendekeza tu na kuwa na kiherehere tegemea majibu yangu umiza na chukizo, tena mubashara kabisa.

Nimemaliza.
Sawa mkuu, natii onyo lako. Napita kimya.
 
Yanga siku Hizi wanamtumia Sana yule mganga wa Visiwani ,nimeshuhudia mechi za dabi Zote kipind hiki akifanya Mambo , hata ya Juzi hii ilikuwa Yanga afungwe 2-0 , ila zilifanyika harakati ,goli moja likahamishwa na kuwa 1-1

Ilikuwa Aziz Ki asisalimiane ,Simba afe, na huku Simba ilitakiwa hivo hivo kwa Chama, MMOJA angekiuka masharti tu ,Matokeo yangekuwa 2-0 .
 
Yanga siku Hizi wanamtumia Sana yule mganga wa Visiwani ,nimeshuhudia mechi za dabi Zote kipind hiki akifanya Mambo , hata ya Juzi hii ilikuwa Yanga afungwe 2-0 , ila zilifanyika harakati ,goli moja likahamishwa na kuwa 1-1

Ilikuwa Aziz Ki asisalimiane ,Simba afe, na huku Simba ilitakiwa hivo hivo kwa Chama, MMOJA angekiuka masharti tu ,Matokeo yangekuwa 2-0 .
😁😁😁 jf raha sanaaa
 
Back
Top Bottom