GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,551
- 108,888
Nikiwa na wao hujua GENTAMYCINE ni mwenzao (mwana Yanga SC) na bahati nzuri hawajui kuwa ndiyo mimi, hivyo huweza kupata mipango yao mingi ya siri na miovu dhidi ya Simba SC.
Taarifa niliyoipata na kuhakikishiwa kutoka Yanga SC ni kwamba, kwa kuona jinsi mchezaji Moses Phiri anavyokuja kasi na kuonekana ni tishio kwa ufungaji wameamua kumroga (kwa Kutumia Kitabu) kutoka kwa mtaalam (mganga wao mkubwa wa kisiwani Zanzibar) ili asifunge tena magoli na awe anakosa mno.
Na ni mganga huyu huyu ndiye aliyemuagua mshambuliaji wa Yanga SC Fiston Mayele msimu uliyopita katika mechi kadhaa alizokuwa na ukame wa magoli, baada ya Simba SC kumtumia mchezaji wa Namungo FC na mwana Simba SC lia lia Shizya Ramadhan Kichuya aibe jezi yake baada ya kumalizika kwa mechi yao pale Namungo mkoani Lindi msimu uliyoisha.
Taarifa za ndani (kutoka jikoni) kwa Yanga SC zinasema kuwa, kutokana na Simba SC kumuwahi kumtengeneza kindumba (kiuchawi) ili asidhurike na Yanga SC, mtaalam hatari wa Yanga SC kila akijaribu anadunda.
Sasa mchezaji tegemeo wa Simba SC Clatous Chota Chama ameandaliwa mkakati wa kuumizwa (kujeruhiwa) vibaya na timu pinzani ambazo zitahongwa na Yanga SC ili asicheze kabisa ligi, na Simba SC iweze kudhoofika pakubwa kwa kutokuwepo kwake.
Kama mwana Simba SC lia lia GENTAMYCINE, nauomba uongozi wa Simba SC uyachukue yote haya niliyoyaandika ya kuwahusu wachezaji muhimu raia wa Zambia Moses Phiri na Clatous Chama ili yote niliyoahidiwa kuwatokea yasitokee.
Na ikiwezekana upesi mno Phiri apelekwe kwa mtaalam wa Simba SC yule wa Morogoro (bibi) au aitwe Dar es Salaam yule wa Mkoani Rukwa, ili amuague vyema Phiri na ikiwezekana sasa awafanyie dawa ya kuwalinda wachezaji wote wa Simba SC dhidi ya kurogwa kwa kuhujumiwa na waganga wanaotumika na kutumwa na Yanga SC.
ONYO
Hakuna mahala popote pale GENTAMYCINE nimekulazimisha uusome huu uzi au uuamini, hivyo kama utaona kwako hauna maana tafadhali nakuomba pita tu na waachie watakaoulewa wachangie. Vinginevyo ukijipendekeza tu na kuwa na kiherehere tegemea majibu yangu umiza na chukizo, tena mubashara kabisa.
Nimemaliza.
Taarifa niliyoipata na kuhakikishiwa kutoka Yanga SC ni kwamba, kwa kuona jinsi mchezaji Moses Phiri anavyokuja kasi na kuonekana ni tishio kwa ufungaji wameamua kumroga (kwa Kutumia Kitabu) kutoka kwa mtaalam (mganga wao mkubwa wa kisiwani Zanzibar) ili asifunge tena magoli na awe anakosa mno.
Na ni mganga huyu huyu ndiye aliyemuagua mshambuliaji wa Yanga SC Fiston Mayele msimu uliyopita katika mechi kadhaa alizokuwa na ukame wa magoli, baada ya Simba SC kumtumia mchezaji wa Namungo FC na mwana Simba SC lia lia Shizya Ramadhan Kichuya aibe jezi yake baada ya kumalizika kwa mechi yao pale Namungo mkoani Lindi msimu uliyoisha.
Taarifa za ndani (kutoka jikoni) kwa Yanga SC zinasema kuwa, kutokana na Simba SC kumuwahi kumtengeneza kindumba (kiuchawi) ili asidhurike na Yanga SC, mtaalam hatari wa Yanga SC kila akijaribu anadunda.
Sasa mchezaji tegemeo wa Simba SC Clatous Chota Chama ameandaliwa mkakati wa kuumizwa (kujeruhiwa) vibaya na timu pinzani ambazo zitahongwa na Yanga SC ili asicheze kabisa ligi, na Simba SC iweze kudhoofika pakubwa kwa kutokuwepo kwake.
Kama mwana Simba SC lia lia GENTAMYCINE, nauomba uongozi wa Simba SC uyachukue yote haya niliyoyaandika ya kuwahusu wachezaji muhimu raia wa Zambia Moses Phiri na Clatous Chama ili yote niliyoahidiwa kuwatokea yasitokee.
Na ikiwezekana upesi mno Phiri apelekwe kwa mtaalam wa Simba SC yule wa Morogoro (bibi) au aitwe Dar es Salaam yule wa Mkoani Rukwa, ili amuague vyema Phiri na ikiwezekana sasa awafanyie dawa ya kuwalinda wachezaji wote wa Simba SC dhidi ya kurogwa kwa kuhujumiwa na waganga wanaotumika na kutumwa na Yanga SC.
ONYO
Hakuna mahala popote pale GENTAMYCINE nimekulazimisha uusome huu uzi au uuamini, hivyo kama utaona kwako hauna maana tafadhali nakuomba pita tu na waachie watakaoulewa wachangie. Vinginevyo ukijipendekeza tu na kuwa na kiherehere tegemea majibu yangu umiza na chukizo, tena mubashara kabisa.
Nimemaliza.