only83
JF-Expert Member
- Oct 15, 2010
- 5,343
- 2,525
...........Tangu bunge la bajeti lilipoanza nilikuwa nasubiri kwa hamu bajeti ya wizara ya utumishi wa umma,na jana bila kusita wala kuona aibu waziri wetu ambaye natilia shaka uwezo wake wa kuwa kiongozi kutokana na namana anavyowasilisha mada pamoja na kuongea kama waziri Ndugu Hawa Ghasia aliwasilisha bajeti hiyo.Kilichoniuma na kinachoniuma ni kutosikia ongezeko la mishahara kwa sisi wapiga nyundo.Wakati wenzetu wanakula posho mpaka za nguo,sisi wapiga nyundo tunaendelea kuumia kwa viela vichache.Na kilichoniumiza zaidi ni pale alipoulizwa kuhusu ongezeko la mishahara,akadai hilo ni siri kati yao na wawakilishi wa wafanyakazi.............Jamani mimi ni mtumishi wa umma lakini sijawai pata taarifa kuwa tunaongezewa shs ngapi,sasa Je,Mgaya,Mkoba na TUCTA mnawawakilisha akina nani wakati mimi mtumishi wa umma sina taarifa hiyo? Na Je,hapa hakuna ajenda ya siri kati yenu TUCTA na serikali ya JK? Na naanza kupata maana ya yale maneno aliyosema JK wakati wa mei mosi namnukuu "Ndugu wakipatana wewe kashike jembe ukalime" na "waliokuwa wanawaombea mabaya wajue kuwa tumepatana" Jamani watumishi wenzangu ndugu wamepatana tushike majembe tukalime tuendelee kupigwa na jua kwa mwaka mwingine...Huku tukianza na mafuta ya taa bei juu lol!!!!