Mary Chuwa
Senior Member
- Feb 24, 2011
- 177
- 40
Imekuwa ni kawaida kusikia ugomvi baina ya wamama na wake za watoto wao wa kiume(wakwe zao)
Hii ni kutokana na wamama wengi kutotambua nafasi yao pindi watoto wao wanapopata wake.
Kwani kabla ya kuoa nafasi hiyo hushikiliwa na mama,na pindi mwanaume anapooa huwa ni ya mke.
Lakini wamama wengi hawaridhiki na kuiacha nafasi hiyo,bali huwa ni kama mashindano kuonesha ubora,
Mfano:mama huona kama mtoto wake wa kiume haudumiwi vizuri,nguo hazifuliwi zikatakata,hapikiwi chakula kama alichokuwa anakiandaa yeye na mengineyo.
Anaona haudumiwi yeye bali ni mkwewe hivyo kujenga wivu na chuki.
Kwa wababa nafasi ya mume hushikiliwa na baba na baada ya binti kuolewa ni nafasi ya mume,
Nawapongeza wababa kwa kutambua kuwa sasa nafasi hiyo si yao tena na kupunguza mgogoro baina yao na wakwe zao,kwa hili nawapongeza sana na ni vyema mkasaidiana ili wakina mama watambue nafasi hiyo si yao tena na kupunguza mgogoro wa kugombana baina yao na wakwe zao.
Hii ni kutokana na wamama wengi kutotambua nafasi yao pindi watoto wao wanapopata wake.
Kwani kabla ya kuoa nafasi hiyo hushikiliwa na mama,na pindi mwanaume anapooa huwa ni ya mke.
Lakini wamama wengi hawaridhiki na kuiacha nafasi hiyo,bali huwa ni kama mashindano kuonesha ubora,
Mfano:mama huona kama mtoto wake wa kiume haudumiwi vizuri,nguo hazifuliwi zikatakata,hapikiwi chakula kama alichokuwa anakiandaa yeye na mengineyo.
Anaona haudumiwi yeye bali ni mkwewe hivyo kujenga wivu na chuki.
Kwa wababa nafasi ya mume hushikiliwa na baba na baada ya binti kuolewa ni nafasi ya mume,
Nawapongeza wababa kwa kutambua kuwa sasa nafasi hiyo si yao tena na kupunguza mgogoro baina yao na wakwe zao,kwa hili nawapongeza sana na ni vyema mkasaidiana ili wakina mama watambue nafasi hiyo si yao tena na kupunguza mgogoro wa kugombana baina yao na wakwe zao.