Kwa hili la DP World, Wabunge wetu wametusaliti sana

Mchokoo

JF-Expert Member
Jul 28, 2015
1,179
1,579
Hawa jamaa wamejisahau mpaka wamepitiliza!

Hawajui hapo walipo ni kwa niaba ya wananchi ili kutetea maslahi ya nchi. Wanalipwa mishahara minono pamoja na posho mbalimbali kwa pesa (kodi) tunazokatwa kwenye mafuta, mishahara, mazao, madini, tozo, na ushuru mbalimbali kwa kila bidhaa inayopita mikononi mwetu.

Yote hayo tumeyakubali ili wasimamie maslahi yetu sisi wananchi. Lakini wenzetu hawa, pamoja na spika wao ambaye ni mwanasheria, wanagawa lango kuu la uchumi wetu bila hata kuonesha kwamba sisi watanzani tunapata nini cha ziada kuliko sasa?

Kwa namna wanasheria wetu wasomi na nguli; wanavyoendelea kuuchambua mkataba huo wa kinyonyaji.

Sasa natambua kwamba kwa mkataba huu wa bandari, wabunge wetu wametusaliti kwenye maeneo yafuatayo;

Mosi, kwenye uhuru wetu wa maamuzi kama nchi. Pili, Katiba yetu imesiginwa vibaya. Tatu, Kuhafifisha madaraka ya rais wa nchi aliyokabiziwa na watanzania. Nne, wametudharirisha kwamba watanzania ni watu wajinga sana. Lakini sijui watafanya kama vile msaliti mkongwe alivyofanya au vinginevyo?

"Kisha Yuda, Yule mwenye kumsaliti, alipoona ya kuwa amekwisha kuhukumiwa, alijuta, akawarudishia wakuu wa makuhani na wazee vile vipande thelathini vya fedha, akasema; nalikosa nilipoisaliti damu isiyo na hatia. (Mathayo 27:3)

Hakuna namna wabunge wetu wafuate nyayo za Yuda Iskariote aliyemsaliti Bwana Yesu, ili kulinusuru taifa.

Mungu ibariki Tanzania.
 
very sad, mbunge wangu amekaa kilofa sana na wala sina shaka naye...akili hana na ni mtu mwenye majivuno na hasira... sijui kama wanajua kuwa ipo siku tutaitaka nchi yetu kwa machozi na damu...
 
Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa

1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)

2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine yeyote anaweza kuja kufanya uwekezaji kwenye bandari za Tanganyika bila udalali wa DPW, je, ukiritimba huu ni kwa faida ya nani?

3.) Ni kwa faida ya nani, DPW apewe haki ya kudai kipande chochote cha ardhi yenye ukubwa wowote anaoutaka yeye ndani ya ‘Territory’ ya Tanganyika na sisi tumpe ardhi hiyo kwa kuondoa watu na miradi yote ndani ya eneo alilolitaka, na tumpatie bire kabisa kwa gharama zetu sisi, hata fidia tulipe sisi ili kuondoa watu kumpisha, huu uwendawazimu ni kwa faida ya nani?

4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

5.) Ni kwa faida ya nani, kwamba mkataba unahusisha bandari za Tanganyika tu na sio za Zanzibar, ilihali bandari ni suala la Muungano? Je, Zanzibar haitaki kunufaika au yenyewe haitaki matunda ya mkataba huu? Ukizingatia walioongia huu mkataba wote ni waZanzibari, kuanzia Samiah Suluhu Hassan, Makame Mbarawah, Hamza Johari na wenzao, kwamba hawataki Zanzibar yao ipate matunda mazuri ya mkataba huu?!

6.) Ni kwa faida ya nani kusema kwamba, hata DPW akavunja mkataba na kukiuka kanuni na taratibu zote zinazotambulika kimataifa, bado hatutaweza kuvunja , kuusema vibaya au kujitoa kwenye mkataba, milele! Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

7.) Ni kwa faida ya nani kwamba pamoja na kuwa DPW watachukua 100% ya faida, bado tena faida hiyo watapewa Msamaha wa kodi kwa 100%, yaani hata hicho wanachovuna nacho hatuchukui kodi, na wakti huo huo tunakamuliwa kodi za miamala, uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?
Eti hawajibu hoja, badala yake wanaleta viroja!
 
Mlishangilia wapinzani walipoambulia Jimbo Moja tu nchi nzima mkasema wanachelewesha maendeleo. Haya ndio matunda ya bunge la wazalendo alilochagua JPM!!
 
Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa

1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)

2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine yeyote anaweza kuja kufanya uwekezaji kwenye bandari za Tanganyika bila udalali wa DPW, je, ukiritimba huu ni kwa faida ya nani?

3.) Ni kwa faida ya nani, DPW apewe haki ya kudai kipande chochote cha ardhi yenye ukubwa wowote anaoutaka yeye ndani ya ‘Territory’ ya Tanganyika na sisi tumpe ardhi hiyo kwa kuondoa watu na miradi yote ndani ya eneo alilolitaka, na tumpatie bire kabisa kwa gharama zetu sisi, hata fidia tulipe sisi ili kuondoa watu kumpisha, huu uwendawazimu ni kwa faida ya nani?

4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

5.) Ni kwa faida ya nani, kwamba mkataba unahusisha bandari za Tanganyika tu na sio za Zanzibar, ilihali bandari ni suala la Muungano? Je, Zanzibar haitaki kunufaika au yenyewe haitaki matunda ya mkataba huu? Ukizingatia walioongia huu mkataba wote ni waZanzibari, kuanzia Samiah Suluhu Hassan, Makame Mbarawah, Hamza Johari na wenzao, kwamba hawataki Zanzibar yao ipate matunda mazuri ya mkataba huu?!

6.) Ni kwa faida ya nani kusema kwamba, hata DPW akavunja mkataba na kukiuka kanuni na taratibu zote zinazotambulika kimataifa, bado hatutaweza kuvunja , kuusema vibaya au kujitoa kwenye mkataba, milele! Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

7.) Ni kwa faida ya nani kwamba pamoja na kuwa DPW watachukua 100% ya faida, bado tena faida hiyo watapewa Msamaha wa kodi kwa 100%, yaani hata hicho wanachovuna nacho hatuchukui kodi, na wakti huo huo tunakamuliwa kodi za miamala, uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

Haya hawawezi kukueleza watakujibu kwa terms za IGA na HGA, akili kisoda
 
Hawa jamaa wamejisahau mpaka wamepitiliza!

Hawajui hapo walipo ni kwa niaba ya wananchi ili kutetea maslahi ya nchi. Wanalipwa mishahara minono pamoja na posho mbalimbali kwa pesa (kodi) tunazokatwa kwenye mafuta, mishahara, mazao, madini, tozo, na ushuru mbalimbali kwa kila bidhaa inayopita mikononi mwetu.

Yote hayo tumeyakubali ili wasimamie maslahi yetu sisi wananchi. Lakini wenzetu hawa, pamoja na spika wao ambaye ni mwanasheria, wanagawa lango kuu la uchumi wetu bila hata kuonesha kwamba sisi watanzani tunapata nini cha ziada kuliko sasa?

Kwa namna wanasheria wetu wasomi na nguli; wanavyoendelea kuuchambua mkataba huo wa kinyonyaji.

Sasa natambua kwamba kwa mkataba huu wa bandari, wabunge wetu wametusaliti kwenye maeneo yafuatayo;

Mosi, kwenye uhuru wetu wa maamuzi kama nchi. Pili, Katiba yetu imesiginwa vibaya. Tatu, Kuhafifisha madaraka ya rais wa nchi aliyokabiziwa na watanzania. Nne, wametudharirisha kwamba watanzania ni watu wajinga sana. Lakini sijui watafanya kama vile msaliti mkongwe alivyofanya au vinginevyo?

"Kisha Yuda, Yule mwenye kumsaliti, alipoona ya kuwa amekwisha kuhukumiwa, alijuta, akawarudishia wakuu wa makuhani na wazee vile vipande thelathini vya fedha, akasema; nalikosa nilipoisaliti damu isiyo na hatia. (Mathayo 27:3)

Hakuna namna wabunge wetu wafuate nyayo za Yuda Iskariote aliyemsaliti Bwana Yesu, ili kulinusuru taifa.

Mungu ibariki Tanzania.
Hivi kwel mnakaa kbs kusubir kauli za wabunge na kutegemea waende against gavoo? Mpo nyuma sana ya muda!!
 
Hawa jamaa wamejisahau mpaka wamepitiliza!

Hawajui hapo walipo ni kwa niaba ya wananchi ili kutetea maslahi ya nchi. Wanalipwa mishahara minono pamoja na posho mbalimbali kwa pesa (kodi) tunazokatwa kwenye mafuta, mishahara, mazao, madini, tozo, na ushuru mbalimbali kwa kila bidhaa inayopita mikononi mwetu.

Yote hayo tumeyakubali ili wasimamie maslahi yetu sisi wananchi. Lakini wenzetu hawa, pamoja na spika wao ambaye ni mwanasheria, wanagawa lango kuu la uchumi wetu bila hata kuonesha kwamba sisi watanzani tunapata nini cha ziada kuliko sasa?

Kwa namna wanasheria wetu wasomi na nguli; wanavyoendelea kuuchambua mkataba huo wa kinyonyaji.

Sasa natambua kwamba kwa mkataba huu wa bandari, wabunge wetu wametusaliti kwenye maeneo yafuatayo;

Mosi, kwenye uhuru wetu wa maamuzi kama nchi. Pili, Katiba yetu imesiginwa vibaya. Tatu, Kuhafifisha madaraka ya rais wa nchi aliyokabiziwa na watanzania. Nne, wametudharirisha kwamba watanzania ni watu wajinga sana. Lakini sijui watafanya kama vile msaliti mkongwe alivyofanya au vinginevyo?

"Kisha Yuda, Yule mwenye kumsaliti, alipoona ya kuwa amekwisha kuhukumiwa, alijuta, akawarudishia wakuu wa makuhani na wazee vile vipande thelathini vya fedha, akasema; nalikosa nilipoisaliti damu isiyo na hatia. (Mathayo 27:3)

Hakuna namna wabunge wetu wafuate nyayo za Yuda Iskariote aliyemsaliti Bwana Yesu, ili kulinusuru taifa.

Mungu ibariki Tanzania.
Kwani ni lini wabunge washawahi kua upande wa wananchi na maslahi ya Taifa?
 
Hawa jamaa wamejisahau mpaka wamepitiliza!

Hawajui hapo walipo ni kwa niaba ya wananchi ili kutetea maslahi ya nchi. Wanalipwa mishahara minono pamoja na posho mbalimbali kwa pesa (kodi) tunazokatwa kwenye mafuta, mishahara, mazao, madini, tozo, na ushuru mbalimbali kwa kila bidhaa inayopita mikononi mwetu.

Yote hayo tumeyakubali ili wasimamie maslahi yetu sisi wananchi. Lakini wenzetu hawa, pamoja na spika wao ambaye ni mwanasheria, wanagawa lango kuu la uchumi wetu bila hata kuonesha kwamba sisi watanzani tunapata nini cha ziada kuliko sasa?

Kwa namna wanasheria wetu wasomi na nguli; wanavyoendelea kuuchambua mkataba huo wa kinyonyaji.

Sasa natambua kwamba kwa mkataba huu wa bandari, wabunge wetu wametusaliti kwenye maeneo yafuatayo;

Mosi, kwenye uhuru wetu wa maamuzi kama nchi. Pili, Katiba yetu imesiginwa vibaya. Tatu, Kuhafifisha madaraka ya rais wa nchi aliyokabiziwa na watanzania. Nne, wametudharirisha kwamba watanzania ni watu wajinga sana. Lakini sijui watafanya kama vile msaliti mkongwe alivyofanya au vinginevyo?

"Kisha Yuda, Yule mwenye kumsaliti, alipoona ya kuwa amekwisha kuhukumiwa, alijuta, akawarudishia wakuu wa makuhani na wazee vile vipande thelathini vya fedha, akasema; nalikosa nilipoisaliti damu isiyo na hatia. (Mathayo 27:3)

Hakuna namna wabunge wetu wafuate nyayo za Yuda Iskariote aliyemsaliti Bwana Yesu, ili kulinusuru taifa.

Mungu ibariki Tanzania.
Hakuna cku CCM itakua na uchungu na rasilimali za nchi hii.

Wao wapate ubunge waishi maisha mazuri na familia zao Basi , mengine hayawahusu.

Lile siyo bunge asidhani.
 
Back
Top Bottom