Tuko
JF-Expert Member
- Jul 29, 2010
- 11,178
- 7,319
Naomba kutumia jukwaa hili kuwapongeza sana wanawake makini ambao naamini ndio waliojaa JF. Kwa kawaida miaka 2-3 baada ya harusi, vile vijizawadi; jiko, sufuria, glasi, sahani, microwave, sijui rice cooker, na hata friji, TV, deki, mashuka, nk.nk.nk, vinakuwa vimeshaanza kuchoka na kuisha.
Stori za Kijiweni zimenifanya nigundue kuwa kwa sisi wa kipato cha chini, vile vikikundi vya upatu vya akina mama vinazitoa sana familia katika manunuzi ya vitu kama hivi. Wakati mwingine unaweza kukuta mshahara wa wife ni almost nusu au pungufu zaidi ukilinganisha na wa baba, lakini visible impact yake pale ndani kubwa mno na huwezi kulinganisha. Mnajua tena wababa matumizi yetu sio editable, na laiti angepewa rungu Utoh kufanya ukaguzi siku moja, wengi tutaondoka na hati chafu, na tunaweza kulazimishwa kuji-Maige...
Big up wamama kwa kuendelea kuziweka juu familia zetu...
Stori za Kijiweni zimenifanya nigundue kuwa kwa sisi wa kipato cha chini, vile vikikundi vya upatu vya akina mama vinazitoa sana familia katika manunuzi ya vitu kama hivi. Wakati mwingine unaweza kukuta mshahara wa wife ni almost nusu au pungufu zaidi ukilinganisha na wa baba, lakini visible impact yake pale ndani kubwa mno na huwezi kulinganisha. Mnajua tena wababa matumizi yetu sio editable, na laiti angepewa rungu Utoh kufanya ukaguzi siku moja, wengi tutaondoka na hati chafu, na tunaweza kulazimishwa kuji-Maige...
Big up wamama kwa kuendelea kuziweka juu familia zetu...