Tangu chama cha Demokrasia na maendeleo kifanye mkutano wa kuhamasisha wananchi kuwawajibisha Viongozi/watawala wao, kuna wengine wametumia mwanya huo kufanya ndivyo sivyo. Hali hii imeleta mtafaruku kati ya jamii na baadhi ya asasi pamoja na watawala.
Kwanza niseme wazi kuwa mwananchi kufanya mawasiliano na mtawala wake kwa njia yoyote ile ni haki yake ya msingi, hivyo CDM kugawa namba ya viongozi hao haikuwa dhambi ukizingatia kuwa namba za mawasiliano yao zilikuwa wazi katika mitandao na kwenye ofisi zao hata kabla ya mikutano hiyo ya CHADEMA kufanyika. Hivyo kitu cha msingi hapa ni kulaumu watu waliotumia namba hizo kwa matumizi mengine na si yale ambayo yalikusudiwa.
Makinda na Ndugai kama binadamu wengine wanaweza kukosea katika maamzi yao, na pale walengwa wanapoona kuwa hawajatendewa haki wanayo sababu ya kupaza sauti ya kudai haki yao (Ila si kwa njia ya matusi kama ilivyotokea). Nina imani Viongozi wa CHADEMA waliwatuma watu wakapaze sauti zao au kuwauliza watawala wao kuwa haya mnayoyafanya ndiyo tuliyowatuma?!na si kuwatukana. Sasa kama kuna mtu amefikia hatua ya kutoa lugha za matusi au vitisho vya namna hiyo, sasa hiyo ni kazi ya vyombo vinavyohusika kuwafuatilia wahusika na kuwawajibisha kwa mjibu wa sheria za nchi.
Angalizo: katika suala hili, vyombo navyo vya habari vimejikuta vikitumbukia katika sakata hili na kuanza kulaumu CHADEMA kama vile ndicho kimesema watu wafanye hivyo. Hili suala linafaa kuangaliwa kwa kina ukizingatia kuwa hata vile vyombo ambavyo vimekuwa kipenzi cha wasikilizaji wengi, sasa vinatumiwa kama vyombo vya propaganda kwa watawala na serikali iliyopo madarakani.
TUKUMBUKE KUWA SEHEMU NYINGI ZIMEKUMBWA NA MACHAFUKO KUTOKANA NA SERIKALI TAWALA KUTUMIA VYOMBO VYA HABARI KUPOTOSHA UKWELI.
TUKUMBUKE KUWA: Maandiko yanasema kuwa atendaye mema hulakiwa kwa ndremo na vifijo, na Yule atendaye maovu huzomewa na hata asipate pa kuficha uso wake.
Tafakari.