Kwa heri bwana Martin Shigela

Kwa heri bwana Martin Shigela

Sr. Magdalena

JF-Expert Member
Joined
Aug 10, 2011
Posts
803
Reaction score
472
Aliyekuwa Kaimu Katibu Mkuu wa CCM mkoa wa Morogoro Bwana Sixtus Mapunda ameteuliwa kuchukua nafasi iliyokuwa inashikiliwa na Martine Shigela (Katibu Mkuu UVCCM), je vijana kuna lolote tulilojifunza kutoka kwa kaka Shigela na je bwana Mapunda ni kijana wa aina gani, je ataweza misukosuko ya siasa za leo?
 
Hakuna yeyote ndani ya CCM atakayechaguliwa akaleta tofauti,hembu tujikumbushe tambo za Mukama,akapita kimya hakuna alilofanya zaidi ya kutunisha account yake,akaja Mangula na Kinana waliingia kwa mbwembwe mpk sasa hakuna la maana zaidi ya style yao mpya ya kubambikia watu kesi.....hata huyo aliyeingia hakuna atakachobadilisha,zaidi sana atabadilika yeye kwa kunawiri na pesa za kifisadi.
 
Wakuu punguzeni jazba...naamini kuna kitu cha kujifunza kwenye kila jambo kiwe positive au negative ...tumejifunza nini kwa Shigela na tutarajie nini kwa Mapunda?
 
Aliyekuwa Kaimu Katibu Mkuu wa CCM mkoa wa Morogoro Bwana Sixtus Mapunda ameteuliwa kuchukua nafasi iliyokuwa inashikiliwa na Martine Shigela (Katibu Mkuu UVCCM), je vijana kuna lolote tulilojifunza kutoka kwa kaka Shigela na je bwana Mapunda ni kijana wa aina gani, je ataweza misukosuko ya siasa za leo?
Waacheni wafu wazike wafu wenzao, sababu ya mapanya kumtoa panya mwenzao nini ?
 
Wakuu punguzeni jazba...naamini kuna kitu cha kujifunza kwenye kila jambo kiwe positive au negative ...tumejifunza nini kwa Shigela na tutarajie nini kwa Mapunda?

Nilichojifunza ni kwamba huwezi kupata jambo jipya toka kwa watu wale wale wenye upeo ule ule, mtazamo ule ule, na wenye fikra zile zile(THE SAME LEVEL OF THINKING). Kwenye shamba la miwa usitegemee kuvuna mihogo.
 
Apeleke Ndevu Zake Zisizopangiliwa Hukooo!
 
Tutarajie mapunda kutengeneza vipunda vingine vidogo vyakusafirisha bidhaa mpya ya magamba.SEMBE
 
Shigela ataukwaa u-dc au u-rc

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom