Kuzuia Mikutano ya Kisiasa: CCM wataumia zaidi ya Upinzani

Elli

Platinum Member
Mar 17, 2008
55,520
86,081
Waswahili walisema kuwa "Kumpiga chura teke ni kumuongezea mwendo". Ni kweli ataumia kidogo kwa sababu utakua umemshtua ila ukweli ni kwamba umemuongezea mwendo. CCM wanafurahi wapinzani kukamatwa ovyo tena wakiwa kwenye vikao vya ndani, wapinzani kuzuiliwa kufanya Mikutano yao ili tu asikike mtu mmoja/chama kimoja kwa manufaa ya mtu au chama.

Kampeni zilizopita CCM walipata muda kabla ya kampeni kupinga au kujibu baadhi ya hoja za wapinzani na hivyo kuzidhoofisha kwa kiasi kikubwa kabla ya Uchaguzi Mkuu. Wapinzani wa leo hii ambao hawana mahali pa kuikosoa CCM na CCM ambao pia watakosa cha kujibu kwakuwa Upinzani umezuiliwa kusema itakua pigo kubwa sana sana kwa CCM kuja kujibu hoja/kashfa/tuhuma zitakazoibuliwa na Upinzani wakati wa uchaguzi na hivyo kuiweka CCM upande mbaya zaidi kuliko hata ilivyo sasa.

Ombi langu, CCM waendelee kuzuia mikutano ya Upinzani ila wahakikishe wana majibu ya kutosha ya kuja kujibu wakati Wapinzani watakaposema. Upinzani nao wataendelea kukusanya evidence za madudu ya CCM halafu watakuja kukutana ulingoni wakati ukifika, yaani CCM watajikuta wanajibu hoja/kashfa za upinzani badala ya kueleza waliyoyafanya na watakayoyafanya.

Twende kazi​
 
Umewaeleza ukweli tatizo hawa kiburi cha vyombo vya dola kimewajaa, na siku zote ashupazaye shingo mwisho wake shingo huvunjika.
 
Mitandao ya kijamii ni 'platform' tosha ya kujinadi.
Wanachofanya upinzani ni kupata media attention kubwa yenye kuwafanya waonewe huruma kuliko CCM.
 
Serekali ya awamu ya tano chini ya uongozi wa Mheshimiwa,Mtukufu Dr John Pombe Magufuli inakiuka misingi ya sheria mama yaani katiba ambayo Rais aliitumia kuapa kuilinda na kuhifadhi.

Ninachokiona sasa ni kuitumia katiba katika namna wanayoona inawakinga watawala.
 
CCM hatuwezi kuumia kwa sababu wananchi wote ni sehemu ya chama chetu
Naamini umenielewa ila umejibu tu ulivyojibu kwakuwa hukua na namna nyingine, asante Mpwa ila TAKUKURU wanakuja kwako pia
 
Serekali ya awamu ya tano chini ya uongozi wa Mheshimiwa,Mtukufu Dr John Pombe Magufuli inakiuka misingi ya sheria mama yaani katiba ambayo Rais aliitumia kuapa kuilinda na kuhifadhi.

Ninachokiona sasa ni kuitumia katiba katika namna wanayoona inawakinga watawala.
Ni kweli na wazi kabisa
 
Serekali ya awamu ya tano chini ya uongozi wa Mheshimiwa,Mtukufu Dr John Pombe Magufuli inakiuka misingi ya sheria mama yaani katiba ambayo Rais aliitumia kuapa kuilinda na kuhifadhi.

Ninachokiona sasa ni kuitumia katiba katika namna wanayoona inawakinga watawala.
Ynawageukia sasa, wameshindwa kujibu hoja wanaleta viroja, we said in 2016
 
Uzi ulikosa Hadi wachangiaji. Imebaki Tume ambayo Kwa kiasi kikubwa imeshaibeba CCM kwenye Wabunge WA bila kupingwa.Kinachofanyika ni ushenzi. wala sio democrasia.
 
Back
Top Bottom