Kuwa wa kiroho (Spirituality)

Kuwa wa kiroho (Spirituality)

Surya

JF-Expert Member
Joined
Jun 7, 2015
Posts
9,759
Reaction score
15,567
Usipokuwa na maarifa ya kiroho basi upo hatarini sana sio tu kuwa masikini daima bali hata na kupotezwa kabisa.

Dunia ni uwanja wa vita, kati ya Ufalme wa Mungu mkuu na ufalme wa miungu.

Ipo nguvu isio onekana kwa Macho ya nyama inayoweza kutawala dunia na vilivyomo.

Roho, Nafsi, Mwili.
1. Mungu kaipa Roho mamlaka ya kutawala dunia na vilivyomo, nafsi au akili ya mtu hujikusanyia nguvu kutokea Ndani rohoni au nje mwilini.

2. Roho ya binadamu imeumbwa kwa mfano wa Mungu ndio maana ni roho yenye nguvu na mamlaka kuzidi roho ya Malaika na majini.

3. Binadamu akiongea kwa kinywa kusema jambo lolote maneno yake hutembea kama roho hai (words are spirit).
ndio maana kuna kitu tunaita manuizo.

4. Kutumia roho za malaika na majini sio kosa ni ruksa kwa kila mtu. Biblia na Quran vinathibitisha hili.

5. Nguvu ya uchawi hutumia roho kutekeleza jambo au kuendesha nafsi ya mtu mwingine (Maarifa na vigezo ni kuwa na Nguvu kubwa ya kiroho)

6. Nguvu za kiroho huongezeka kwa kujua kanuni za kiroho.

7. Ukiwa huna nguvu za kiroho, Mimea, ardhi, Maji na moto ambavyo ni Muhimu kwa mwili wa binadamu hutumika kiroho kumuathiri binadamu.

Kanuni baadhi za kichawi ili kuroga.

Maneno (Manuizo) + mti au majani + spirit zilizo ulimwenguni hutiii maneno ya miungu watu na kufanya jambo fulani

Maji + Manuizo + roho husika huja na kufanya jambo kulingana na maagizo.

8. Watu ni miungu kwani tumepewa vinywa vinavyoweza kutuma (kuamrisha) roho nyingi tofauti hapa ulimwenguni.
Roho hizo ukizijua tu zenyewe zinapenda na zinajua wajibu wake ni kumtii Adamu na uzao wake.

9. Unaweza kunyanyua vyuma kutanua misuri uwe na nguvu za mwili, lakini aliyetanua roho yake anaweza kuwa na nguvu kubwa zaidi supernatural power ya kufanya maajabu kama Samson.
Samson hakua na misuri mwilini ndio maana aliulizwa siri ya nguvu zako ni nini na hunyanyuagi vyuma spirit behind.

10. roho zinafanya kazi kwa maagano.
kwa kutumia maneno na kiumbe kama funza baada ya kukipa chakula fulani funza wanapokea nguvu ya kipepo na kuweza kwenda kumuingia mtu mwingine aise na nguvu za kiroho kwa kazi maalumu, hasa kuteka nafsi na kuigeuza isivyotaka.

11. Naongea kuhusu mambo ya kiroho
Ipo kanuni ya namna ya kujipa nguvu ya kimamlaka katika eneo fulani, zipo roho zinazotawala na kulinda mipaka na mataifa or territories.

12. Huwezi ukakuwa (to be great) tu na kuwa mkubwa na mkuu bila kutawala vitu fulani katika ulimwengu wa roho.

Pia inasemekana kuwa Kupitia mlezi wa mtoto mdogo Elon Musk, Elon Musk alikuwa na miungu ya jamii ya Misri katika chumba chake na alikuwa na roho fulani ambazo ni rafiki zake. bibi au mlezi huyo akiwa shahidi.

The spirit rule the World.

........

........

The spirit create the World
 
Iyo namba nne ime andikwa kwenye biblia mstarii gani....
Hapa ni Mungu katuma pepo kwa Manabii wa Mfalme.

2 Mambo ya Nyakati 18:18-20
18 Mikaya akasema, Sikieni basi neno la Bwana; Nalimwona Bwana ameketi katika kiti chake cha enzi na jeshi lote la mbinguni wamesimama mkono wake wa kuume na wa kushoto.

19 Bwana akasema, Ni nani atakayemdanganya Ahabu mfalme wa Israeli, ili akwee Ramoth-gileadi akaanguke? Basi huyu akasema hivi; na huyu hivi.

20 Akatoka pepo, akasimama mbele za Bwana, akasema, Mimi nitamdanganya. Bwana akamwambia, Jinsi gani?

Hapa ni Balaamu kapewa kazi ya kutupa roho za laana kwa Taifa la israel.

Hesabu 22:5-6
5 Basi akatuma wajumbe kwa Balaamu mwana wa Beori, hata Pethori, ulio kando ya Mto, mpaka nchi ya wana wa watu wake, kwenda kumwita, akisema, Tazama, kuna watu waliotoka Misri; tazama, wanaufunika uso wa nchi, tena wanakaa kunikabili mimi.

6 Basi, njoo wewe, nakusihi unilaanie watu hawa; maana wana nguvu kunishinda mimi. Labda nitawaweza, tupate kuwapiga, niwafukuze watoke katika nchi yangu, kwa maana najua ya kuwa yeye umbarikiye hubarikiwa, na yeye umlaaniye hulaaniwa.
 
Watu ama elimu iliyopo Kwenye jamii ni cheap mno, watu wamekaririshwa kufanya only physical exercise Ila mental, emotional and spiritual exercises hakuna na ndizo zenye nguvu kabisa kuliko hata mwili,

Ya kwanza ni spiritual, emotions,mental last ni physical energy/exercise Sasa dunia imesisitiziwa kufanya zoezi sehemu ya ubinadamu ambayo ni meaningless. Ni Kama watu walivyozoea kuoga na kujipaka mafuta/losheni sijui perfume ili wang'ae na wanukie ngozi yao ing'ae Ila wangejua hayo yote ni bure kabisa.
Watu wangedili mno na mambo ya kiroho..
Ujue hata Jesus alisema kabisa kuwa utafuteni ufalme wa mbinguni mengine mtapewa effortlessly Mana you're strong spiritually.
Na alisisitiza kuwa ufalme wa mbinguni upo ndani yako. Waisalmu wao ni elimu ahera kwanza elimu dunia baadaye,
 
Watu ama elimu iliyopo Kwenye jamii ni cheap mno, watu wamekaririshwa kufanya only physical exercise Ila mental, emotional and spiritual exercises hakuna na ndizo zenye nguvu kabisa kuliko hata mwili,

Ya kwanza ni spiritual, emotions,mental last ni physical energy/exercise Sasa dunia imesisitiziwa kufanya zoezi sehemu ya ubinadamu ambayo ni meaningless. Ni Kama watu walivyozoea kuoga na kujipaka mafuta/losheni sijui perfume ili wang'ae na wanukie ngozi yao ing'ae Ila wangejua hayo yote ni bure kabisa.
Watu wangedili mno na mambo ya kiroho..
Ujue hata Jesus alisema kabisa kuwa utafuteni ufalme wa mbinguni mengine mtapewa effortlessly Mana you're strong spiritually.
Na alisisitiza kuwa ufalme wa mbinguni upo ndani yako. Waisalmu wao ni elimu ahera kwanza elimu dunia baadaye,
Light
 

Attachments

  • images (7).jpeg
    images (7).jpeg
    17.4 KB · Views: 31
Back
Top Bottom