Kuwa na akili nyingi kama Mzee Bishanga sio kuwa tajiri!

Mtambuzi

Platinum Member
Oct 29, 2008
8,810
15,398

Hata mimi nilikuwa nikiamini katika jambo hili, kwamba watu wenye uwezo mkubwa kiakili huwa na mafanikio katika maisha. Nilikuwa nikiamini hivyo kwa sababu nilikuwa nikijua kwamba ni wale wenye uwezo mkubwa darasani ndio pekee wenye uwezo wa kufanikiwa katika maisha, lakini hivi karibuni baada ya kusoma tafiti kadhaa na kuangalia maisha ya wale niliosoma nao ambao darasani walikuwa wakituburuza kwa kupata maksi za juu na kufaulu sasa hivi maisha yao ni ya kawaida kabisa na wengine wameshindwa kabisa katika maisha wamebaki kubaingaiza tu mitaani.

Wale ambao tulikuwa tukiwaita mbumbumbu, ambao hawakuwa na uwezo kabisa darasani na wengine walishindwa kabisa kuendelea na masomo wakiwa hata hawajafika darasa la tano, ndio ambao wamefanikiwa na kumudu kuwa na kipato cha kuridhisha na wengine wakiwa wanamiliki biashara kubwa kubwa. Na ndio maana kuna wakati unashangaa sana kusikia watu wakisema, ‘fulani alikuwa bomu kabisa darasani, hata la nne hakumudu kumaliza, lakini sasa ana fedha kama nini!' Kwa nini kauli kama hizi zimebeba mshangao mkubwa? Ni kwa sababu, tumefanywa kuamini kwamba, uwezo wa kiakili, ndiyo unaoamua mtu apate fedha kiasi gani maishani mwake.
Diamond2.jpg

Ninavyojua mimi ni kwamba, kuna watu kwa mamilioni ambao wana akili sana, kuanzia za darasani na zile za nje ya darasa. Lakini, ukiangalia kipato chao, kila siku ni kile cha kubangaiza. Ukweli ni kwamba, hakuna uhusiano kati ya akili nyingi na upataji wa fedha. Watu wenye uwezo wa kawaida kiakili wanaweza kuwa na mali sawa na wenye uwezo mkubwa. Haijalishi uwezo wako wa kiakili linapokuja suala la mafanikio ya kiuchumi. Kama una mtazamo chanya na unahitaji mafanikio kiuchumi, haihitaji uwezo mkubwa kiakili kuvipata hivyo.

Hata hivyo imebainika kwamba watu wenye uwezo mkubwa sana kiakili pia wana matatizo kiuchumi kiasi cha kushindwa kabisa kulipia bili na za vitu kama umeme, maji, simu na vingine hata vidogo zaidi. Matatizo kiuchumi yanaweza kuhusishwa na uwezo mdogo wa kutunza pesa. Tafiti za nyuma zilionesha kwamba, uwezo wa kiakili huathiri pato au pesa ambayo mtu hutengeneza kwa mwaka. Watu wenye uwezo mkubwa kiakili huwa na mafanikio ya juu kielimu, kicheo na hii hutokea mara nyingi. Hata Ruth Spinks, mwanasayansi wa neva (neuroscientist) anathibitisha jambo hilo na kusema, halina majadala. Na anasema, kwenye pato la kifedha, akili kubwa haina nafasi kubwa.
ray.jpg

Lakini pia mtu kuwa na kazi inayomlipa vizuri haimaanishi kuwa ni tajiri. Mtu anaweza kuwa na mshahara mzuri sana kwa sababu ya elimu na cheo chake, lakini je, umeshawahi kujiuliza kuhusu namna watu hawa wanavyodaiwa? Wanadaiwa sana, kwa sababu hata kutunza fedha, kwao ni shughuli pevu.
Kwa mfano,, ingawa wanasayansi waliogundua roketi walikuwa wakipata mapato makubwa haikumaanisha kwamba wao ni matajiri kwani hawakuwa na akiba ya kutosha kulidhihirisha hilo.

Utafiti mpya wa Zagorsky unaonesha kwamba watu wenye uwezo mkubwa sana kiakili huwa hawana tabia ya kutunza pesa nyingi. Wengi wanaonekana kujali zaidi sifa za kiakili kuliko zile za kifedha. Ndiyo maana, ni vigumu kukuta wanataaluma wakiwa ndiyo matajiri katika jamii.
 
Bishanga nakuomba sana usichangie huu uzi.
Lakini unaweza kuchungulia na kusalimia ukipenda.......................LOL
 
Najua kuna watu watakuja humu na kutoa povu mdomoni wakinibishia......
Natabiri mwanangu mwenyewe tena wa kumzaa King'asti atakuwa wa kwanza....................LOL
 
Last edited by a moderator:
Mimi pia hili jambo nimeliona wale waliokuwa wanaongoza darasani wengi wao wanaishia kuwa just employees for the rest of their life ikizidi sana kipato cha kujitosheleza. Nafikiri ni kuwa wengi wasiokuwa na elimu ya zaidi huwa ni risk takers, they don't real take into account what if......haya mambo ya wasomi ya kufanya toooooo many planning ndio yanaishia kuwarudisha nyuma.
 
I beg to differ with this analysis. Mbona watu wanaotumia sana pesa ndo wanazipata zaidi???sisi wabahili wala hatupati zaidi???
 
Bishanga ni babu jinga. Ana mipesa lakini akili hana! Kila siku analiwa mihela yake na vibinti vi tinieja.
 
Last edited by a moderator:

Hata mimi nilikuwa nikiamini katika jambo hili, kwamba watu wenye uwezo mkubwa kiakili huwa na mafanikio katika maisha. Nilikuwa nikiamini hivyo kwa sababu nilikuwa nikijua kwamba ni wale wenye uwezo mkubwa darasani ndio pekee wenye uwezo wa kufanikiwa katika maisha, lakini hivi karibuni baada ya kusoma tafiti kadhaa na kuangalia maisha ya wale niliosoma nao ambao darasani walikuwa wakituburuza kwa kupata maksi za juu na kufaulu sasa hivi maisha yao ni ya kawaida kabisa na wengine wameshindwa kabisa katika maisha wamebaki kubaingaiza tu mitaani.

Wale ambao tulikuwa tukiwaita mbumbumbu, ambao hawakuwa na uwezo kabisa darasani na wengine walishindwa kabisa kuendelea na masomo wakiwa hata hawajafika darasa la tano, ndio ambao wamefanikiwa na kumudu kuwa na kipato cha kuridhisha na wengine wakiwa wanamiliki biashara kubwa kubwa. Na ndio maana kuna wakati unashangaa sana kusikia watu wakisema, ‘fulani alikuwa bomu kabisa darasani, hata la nne hakumudu kumaliza, lakini sasa ana fedha kama nini!’ Kwa nini kauli kama hizi zimebeba mshangao mkubwa? Ni kwa sababu, tumefanywa kuamini kwamba, uwezo wa kiakili, ndiyo unaoamua mtu apate fedha kiasi gani maishani mwake.
Diamond2.jpg

Ninavyojua mimi ni kwamba, kuna watu kwa mamilioni ambao wana akili sana, kuanzia za darasani na zile za nje ya darasa. Lakini, ukiangalia kipato chao, kila siku ni kile cha kubangaiza. Ukweli ni kwamba, hakuna uhusiano kati ya akili nyingi na upataji wa fedha. Watu wenye uwezo wa kawaida kiakili wanaweza kuwa na mali sawa na wenye uwezo mkubwa. Haijalishi uwezo wako wa kiakili linapokuja suala la mafanikio ya kiuchumi. Kama una mtazamo chanya na unahitaji mafanikio kiuchumi, haihitaji uwezo mkubwa kiakili kuvipata hivyo.

Hata hivyo imebainika kwamba watu wenye uwezo mkubwa sana kiakili pia wana matatizo kiuchumi kiasi cha kushindwa kabisa kulipia bili na za vitu kama umeme, maji, simu na vingine hata vidogo zaidi. Matatizo kiuchumi yanaweza kuhusishwa na uwezo mdogo wa kutunza pesa. Tafiti za nyuma zilionesha kwamba, uwezo wa kiakili huathiri pato au pesa ambayo mtu hutengeneza kwa mwaka. Watu wenye uwezo mkubwa kiakili huwa na mafanikio ya juu kielimu, kicheo na hii hutokea mara nyingi. Hata Ruth Spinks, mwanasayansi wa neva (neuroscientist) anathibitisha jambo hilo na kusema, halina majadala. Na anasema, kwenye pato la kifedha, akili kubwa haina nafasi kubwa.
ray.jpg

Lakini pia mtu kuwa na kazi inayomlipa vizuri haimaanishi kuwa ni tajiri. Mtu anaweza kuwa na mshahara mzuri sana kwa sababu ya elimu na cheo chake, lakini je, umeshawahi kujiuliza kuhusu namna watu hawa wanavyodaiwa? Wanadaiwa sana, kwa sababu hata kutunza fedha, kwao ni shughuli pevu.
Kwa mfano,, ingawa wanasayansi waliogundua roketi walikuwa wakipata mapato makubwa haikumaanisha kwamba wao ni matajiri kwani hawakuwa na akiba ya kutosha kulidhihirisha hilo.

Utafiti mpya wa Zagorsky unaonesha kwamba watu wenye uwezo mkubwa sana kiakili huwa hawana tabia ya kutunza pesa nyingi. Wengi wanaonekana kujali zaidi sifa za kiakili kuliko zile za kifedha. Ndiyo maana, ni vigumu kukuta wanataaluma wakiwa ndiyo matajiri katika jamii.
Naamini na wengi wanaamini kuwa wafanyabiashara wengi elimu yao si kivile na hao hao wamewapita wengi wenye masters au wenye akili sana mfano fanya research kwa wafanyabiashara wengi wa Kariakoo,Dar yote,Mwanza,Mbeya utagundua wengi elimu si kubwa sana ila income,assets huwagusi
 
wenye akili wengi sio marisk takers,kila kitu wanakifanyia analysis weeeeeeeeeeeh! mwishowe wanaamua kukiacha !
 
Wacha nimwage povu langu. Hiyo analysis ya Mtambuzi ina kasoro. Kushinda mitihani siyo sifa pekee ya kusema mtu ana akili nyingi. Akili nyingi ziko katika nyanja mbali mbali. Michael Jackson alikuwa na akili nyingi katika muziki wa pop. Albert Einstein alikuwa na akili nyingi katika hesabu na fizikia. Julius Nyerere alikuwa na akili nyingi katika siasa. Usain Bolt ana akili nyingi katika riadha hasa mbio fupi. Wapo na wengine wengi. Je watu hao niliowataja unaweza kuwaita watu ambao hawakufanikiwa? Mafanikio siyo kuwa na pesa nyingi. Kuna watu ambao kwa nature zao pesa kwao siyo "motivator". Motivators kwao zinaweza kuwa ni vitu kama kushinda Nobel Prize, Kushinda Grammy, kupewa sifa kama 'Sir' kwa Waingereza, n.k.. Lakini kwa misingi ya nadharia ya mtaalam Maslow inayoitwa "Hierarchy of Needs" siyo ajabu kwa watu wa dunia ya tatu (maskini wa kutupwa) kupima mafanikio kwa kigezo cha pesa tu. Bado mahitaji yetu ni yale ya chini (ya msingi).
 
Mimi pia hili jambo nimeliona wale waliokuwa wanaongoza darasani wengi wao wanaishia kuwa just employees for the rest of their life ikizidi sana kipato cha kujitosheleza. Nafikiri ni kuwa wengi wasiokuwa na elimu ya zaidi huwa ni risk takers, they don't real take into account what if......haya mambo ya wasomi ya kufanya toooooo many planning ndio yanaishia kuwarudisha nyuma.

Exactly MadameX, this is what i wanted to say
 
Wacha nimwage povu langu. Hiyo analysis ya Mtambuzi ina kasoro. Kushinda mitihani siyo sifa pekee ya kusema mtu ana akili nyingi. Akili nyingi ziko katika nyanja mbali mbali. Michael Jackson alikuwa na akili nyingi katika muziki wa pop. Albert Einstein alikuwa na akili nyingi katika hesabu na fizikia. Julius Nyerere alikuwa na akili nyingi katika siasa. Usain Bolt ana akili nyingi katika riadha hasa mbio fupi. Wapo na wengine wengi. Je watu hao niliowataja unaweza kuwaita watu ambao hawakufanikiwa? Mafanikio siyo kuwa na pesa nyingi. Kuna watu ambao kwa nature zao pesa kwao siyo "motivator". Motivators kwao zinaweza kuwa ni vitu kama kushinda Nobel Prize, Kushinda Grammy, kupewa sifa kama 'Sir' kwa Waingereza, n.k.. Lakini kwa misingi ya nadharia ya mtaalam Maslow inayoitwa "Hierarchy of Needs" siyo ajabu kwa watu wa dunia ya tatu (maskini wa kutupwa) kupima mafanikio kwa kigezo cha pesa tu. Bado mahitaji yetu ni yale ya chini (ya msingi).

Naandaa uzi kukujibu very soon...............
 
Back
Top Bottom