Captain mopao
Senior Member
- Feb 25, 2021
- 133
- 379
Habari zenu wadau
Kuna wezi wameibuka hapa Dodoma wanapenda kutembea wawili wawili. Wapo wengi lakini hutembea kwa pair ya watu wawili
Hawa jamaa wanawaibia watu sana kwenye daladala na kama wana dawa kugundua ni ngumu sana.
Techinic wanayotumia kwanza wana maneno ya busara na ukarimu sana wanapanda daladala wote wanakaa siti moja ikishajaa mwizi mmoja anaangalia kati ya waliosimama yupi anaonekana ana pesa wakimuona ambae kidogo anaelekea mmoja ananyanyuka na kukuachia siti ukae yule wa pili ambae atabaki kakaa ndio atakayekuibia.
Huyu aliekaa unakuta ana koti ambalo kalininginiza kwenye bega na hilo koti limefunika mkono mmoja hauonekani huo ndio anatumia kuiba pale mkiwa mmebanana.
Na pia njia nyingine huwa mwizi aliyekaa anaangusha kitu chochote kwa upande wako pesa au simu ukiinama kumuokotea ni kitendo cha dakik 0 unakuwa umeshaibiwa.
Na wakishafanya uharifu huwa wanashuka gafla utasikia konda tuache hapa hapa.
Ukisikia hivo ujue wameshaiba kuna mzee juzi kaibiwa laki nane kwenye daladala, pia kuna siku nilikuwa natoka Nkuhungu waliiba simu ya mama mmoja wakashukia Bahi Road pale mama anakuja kugundua tunakaribia kufika.
Hawa jamaa identity yao ni wakarimu wana maneno mengi sana na mmoja nimemkalili ni mweupe ana upara na hereni sikio moja halafu kajichora tatuu mikononi
Huyo ni mmoja kati ya wengi
Maeneo yao ni Msalato siku za Jumamosi mnadani huwa hawakosi huwa wanapanda daladala wanakwenda na kurudi
Na soko la Job Ndugai nane nane mitaa ile hawakosi
Kuweni makini sana na mtu anayekuchangamkia na kukuachia siti
Kuna wezi wameibuka hapa Dodoma wanapenda kutembea wawili wawili. Wapo wengi lakini hutembea kwa pair ya watu wawili
Hawa jamaa wanawaibia watu sana kwenye daladala na kama wana dawa kugundua ni ngumu sana.
Techinic wanayotumia kwanza wana maneno ya busara na ukarimu sana wanapanda daladala wote wanakaa siti moja ikishajaa mwizi mmoja anaangalia kati ya waliosimama yupi anaonekana ana pesa wakimuona ambae kidogo anaelekea mmoja ananyanyuka na kukuachia siti ukae yule wa pili ambae atabaki kakaa ndio atakayekuibia.
Huyu aliekaa unakuta ana koti ambalo kalininginiza kwenye bega na hilo koti limefunika mkono mmoja hauonekani huo ndio anatumia kuiba pale mkiwa mmebanana.
Na pia njia nyingine huwa mwizi aliyekaa anaangusha kitu chochote kwa upande wako pesa au simu ukiinama kumuokotea ni kitendo cha dakik 0 unakuwa umeshaibiwa.
Na wakishafanya uharifu huwa wanashuka gafla utasikia konda tuache hapa hapa.
Ukisikia hivo ujue wameshaiba kuna mzee juzi kaibiwa laki nane kwenye daladala, pia kuna siku nilikuwa natoka Nkuhungu waliiba simu ya mama mmoja wakashukia Bahi Road pale mama anakuja kugundua tunakaribia kufika.
Hawa jamaa identity yao ni wakarimu wana maneno mengi sana na mmoja nimemkalili ni mweupe ana upara na hereni sikio moja halafu kajichora tatuu mikononi
Huyo ni mmoja kati ya wengi
Maeneo yao ni Msalato siku za Jumamosi mnadani huwa hawakosi huwa wanapanda daladala wanakwenda na kurudi
Na soko la Job Ndugai nane nane mitaa ile hawakosi
Kuweni makini sana na mtu anayekuchangamkia na kukuachia siti