NostradamusEstrademe
JF-Expert Member
- Jul 1, 2017
- 3,840
- 5,097
Mimi sikubaliani na TIBIM kuwa eti mtu ukipanda miti ekari100 baada ya miaka15 mkivuna miti mnakuwa matajiri kuliko kupoteza miaka yako 15 ukisoma.Ataniwia radhi ni maoni tu.Elimu ni ufunguo wa maisha.Hakuna kitu kibaya ukiwa masikini halafu tena na elimu uwe huna.Hiyo habari ya kupanda miti ni mawazo tu unaweza kuta hata hiyo ekari100 huna na au ukapanda miti yote ikafa.Namnukuu mhe Flani raisi wetu awamu ya flani alipataga kusema ''Wazazi wa Maradhi ni Ujinga na Umasiki,Ujinga ni baba yao na Umasikini ni mama yao''(Mwisho wa kunukuu).
Ukiwa huna elimu kabisa kila kitu unafikiria umelogwa na unaendesha mambo yako kama meli isiyo na usukani matokeo yake maradhi na umasikini juu.Hivi unafikiri matajiri tulio nao Mfano Mzee wa IPP na kijana MOD hawana elimu?.Mzee wa IPP ana shahada ya udakitari na ni moja ya watu wachache wenye cheti cha charter cha wingereza hapa nchini.Kijana MODi ana shahada ya pili ya uchumi amesomea Marekani,Mzee wa watu wa Juice,Unga n.k anaweza kuwa hana elimu kubwa lakini amesomesha wanawe kwa elimu za juu sana kwa kuona umri wake mkubwa na wanawe wanamsaidia kupanua biashara na nyie mnaona.
Ni kweli wako matajiri walio na utajiri bila elimu ila ukiona wanavyoendesha mambo yao utasikitika sana.Unakuta mtu anaungulia ndani na pese kwenye magunia.Eleweni kuwa hata matajiri wakubwa wasio na elimu kuendesha mambo yao wanatafuta wasomi.Na walio wajanja wanaanza kusoma baada ya kugundua walichokosa maishani na wengine siwataji wameshafikia hata ngazi ya udaktari wa falsafa.Unakuta mtu ana ng'ombe 5000 lakini analala kwenye ngozi ya ngombe na hali nyama anachinja siku ngombe akifa au kukiwa na msiba.
Eleweni haiwezekani watu wote tukawa matajiri nani atamtuma mwenzake na nani atamuajiri mwenzake?.Matajiri mnao waona Marekani msije dhani hawana Elimu kama kina Trump na huyu tajiri wa Africa Aliko Dangote.Niwieni radhi kidogo nitataja mikoa yenye maendeleo mkoa flani wa kaskazini,mkoa flani wa kusini magharibe na na mkoa flani wa magharibi maendeleo yao japo hawana rasilimali yeyote ya kuwekeza au ardhi kubwa sana lakini wameendelea kutokana na Elimu sio maisha ya kubahatisha bahatisha.
Ili kuvunja CIRCLE ya umasikini kitu cha kwanza kabisa ni kutoa UJINGA kwa elimu mambo ya bahati yatafuatia hiyo ni mipango ya mungu sio kusema mbona fulani hajasoma lakini ana mali ni kujidanganya bahati ya mwenzio usilalie mlango wazi.
Kinachosababisha CIRCLE ya umasikini isikatike ni UJINGA(kukosa elimu) baba akiwa hajasoma kabisa akizaa mtoto naye anajiwa na ujinga wakusema mbona baba hajasoma mimi nisome nini sasa.Mtoto ana pass ujinga huo kwa wanawe na wanawe kisa mtasingizia laana au shetani SHETANI wetu ni ujinga wa kukosa elimu.Kwa ujinga mtu alio nao mtu anaoa wake wanne huku akijua ni masikini unategemea nini watoto wanazaliwa kwenye lindi la umasikini.Bahati mbaya baba akiondoka bado anaacha watoto kwenye lindi la umasikini kizazi na kizazi wanapasiana ujinga.
ELIMU inamkomboa mtu kutokuwa masikini wa kutupwa(ABJECT POVERTY) pia inamfanya mtu awe na uwezo wa kati sio chini sana wala juu sana.Sasa usiende shule kabisa utegee utakua kama flani utasubiri mpaka jua linazama.
Kitu kingine niwaase watanzania wenzangu.Kuna dhana imejengeka kuwa mtu anasoma ili aajiriwe.Hii pia ndio inachangia kuwafanya wasomi wasipige hatua kimaendele.Mtu unasoma ili uelimike upambane na hali yako serikali haina uwezo wa kuajiri kila mtu wa kila sekta na hata sekta binafsi imefikia hapo.Hiyvo chonde msikate tamaa kutokusoma kisa sitaajariwa afterall kuajiriwa ni utumwa.Tumia elimu na maarifa uliyopata kujiajiri mwenyewe.
Naomba kutoa hoja
Ukiwa huna elimu kabisa kila kitu unafikiria umelogwa na unaendesha mambo yako kama meli isiyo na usukani matokeo yake maradhi na umasikini juu.Hivi unafikiri matajiri tulio nao Mfano Mzee wa IPP na kijana MOD hawana elimu?.Mzee wa IPP ana shahada ya udakitari na ni moja ya watu wachache wenye cheti cha charter cha wingereza hapa nchini.Kijana MODi ana shahada ya pili ya uchumi amesomea Marekani,Mzee wa watu wa Juice,Unga n.k anaweza kuwa hana elimu kubwa lakini amesomesha wanawe kwa elimu za juu sana kwa kuona umri wake mkubwa na wanawe wanamsaidia kupanua biashara na nyie mnaona.
Ni kweli wako matajiri walio na utajiri bila elimu ila ukiona wanavyoendesha mambo yao utasikitika sana.Unakuta mtu anaungulia ndani na pese kwenye magunia.Eleweni kuwa hata matajiri wakubwa wasio na elimu kuendesha mambo yao wanatafuta wasomi.Na walio wajanja wanaanza kusoma baada ya kugundua walichokosa maishani na wengine siwataji wameshafikia hata ngazi ya udaktari wa falsafa.Unakuta mtu ana ng'ombe 5000 lakini analala kwenye ngozi ya ngombe na hali nyama anachinja siku ngombe akifa au kukiwa na msiba.
Eleweni haiwezekani watu wote tukawa matajiri nani atamtuma mwenzake na nani atamuajiri mwenzake?.Matajiri mnao waona Marekani msije dhani hawana Elimu kama kina Trump na huyu tajiri wa Africa Aliko Dangote.Niwieni radhi kidogo nitataja mikoa yenye maendeleo mkoa flani wa kaskazini,mkoa flani wa kusini magharibe na na mkoa flani wa magharibi maendeleo yao japo hawana rasilimali yeyote ya kuwekeza au ardhi kubwa sana lakini wameendelea kutokana na Elimu sio maisha ya kubahatisha bahatisha.
Ili kuvunja CIRCLE ya umasikini kitu cha kwanza kabisa ni kutoa UJINGA kwa elimu mambo ya bahati yatafuatia hiyo ni mipango ya mungu sio kusema mbona fulani hajasoma lakini ana mali ni kujidanganya bahati ya mwenzio usilalie mlango wazi.
Kinachosababisha CIRCLE ya umasikini isikatike ni UJINGA(kukosa elimu) baba akiwa hajasoma kabisa akizaa mtoto naye anajiwa na ujinga wakusema mbona baba hajasoma mimi nisome nini sasa.Mtoto ana pass ujinga huo kwa wanawe na wanawe kisa mtasingizia laana au shetani SHETANI wetu ni ujinga wa kukosa elimu.Kwa ujinga mtu alio nao mtu anaoa wake wanne huku akijua ni masikini unategemea nini watoto wanazaliwa kwenye lindi la umasikini.Bahati mbaya baba akiondoka bado anaacha watoto kwenye lindi la umasikini kizazi na kizazi wanapasiana ujinga.
ELIMU inamkomboa mtu kutokuwa masikini wa kutupwa(ABJECT POVERTY) pia inamfanya mtu awe na uwezo wa kati sio chini sana wala juu sana.Sasa usiende shule kabisa utegee utakua kama flani utasubiri mpaka jua linazama.
Kitu kingine niwaase watanzania wenzangu.Kuna dhana imejengeka kuwa mtu anasoma ili aajiriwe.Hii pia ndio inachangia kuwafanya wasomi wasipige hatua kimaendele.Mtu unasoma ili uelimike upambane na hali yako serikali haina uwezo wa kuajiri kila mtu wa kila sekta na hata sekta binafsi imefikia hapo.Hiyvo chonde msikate tamaa kutokusoma kisa sitaajariwa afterall kuajiriwa ni utumwa.Tumia elimu na maarifa uliyopata kujiajiri mwenyewe.
Naomba kutoa hoja
Last edited by a moderator: