(PROSTATE DISORDERS) TEZI DUME NI NINI?
Tezi dume ni moja ya tezi la uzazi la kiume ambalo kila mwanaume anayo, tezi hili lipo chini ya kibofu cha mkojo na linazunguka njia ya mkojo toka kwenye kibofu kwenda kwenye uume. Kazi ya tenzi dume ni kutoa majimaji anayochanganyika na mbegu za kiume (sperms) kutengeneza manii (semen).
Jinsi umri unavyoongezeka tezi dume nalo huongezeka ukubwa ambao unaweza kuwa wa kawaida na kusababisha kufinya njia ya mkojo au saratani.
Kuna aina tatu za magonjwa ya tezi dume.
- Maambukizi ya Bakteria (Prostatitis).
- Kukua kwa tezi dume ambalo sio saratani (Benign Prostatic Hypertrophy-BPH).
- Saratani ya tezi dume.
Chanzo cha tatizo la tenzi dume ;maambukizi ya bacteria (Prostatitis) mbalimbali ambao wanaweza kuwa ni visababishi vya magonjwa mbalimbali ya zinaa mfano, kaswende, kisonono, pangusa n.k au bacteria wanao shambulia mfumo wa mkojo (UTI) wanaweza kupenya na kuifikia tezi dume na kuishambulia, vyanzo vingine ni kushuka kwa kinga za mwili na ajali zinazopelekea kuumia katika eneo ambalo tezi dume ipo na pia kunamazingira hatarishi yanayo pelekea mwanaume kuathirika na hili tatizo; Kama mwanaume alishawahi kuwa na hili tatizo na hakupata matibabu sahihi.
Pia kuwa na maambukizi katika kibofu cha mkojo au mrija unao tiririsha mkojo (urethra), Kutokunywa maji ya kutosha, Kuwa na wapenzi wengi na kushiriki tendo la ndoa na mpenzi mwenye maambukizi ya magonjwa ya zinaa na HIV/AIDS.
DALILI ZA HILI TATIZO
- Maumivu wakati wa kutoa haja ndogo au kuhisi kama mkojo ni wa moto na maumivu wakati wa kufika kileleni
- Kwenda haja ndogo mara kwa mara
- Mtiririko wa mkojo kuwa dhaifu
- Maumivu chini ya kitovu Na kiuno na chini ya mgongo
- Maumivu ya sehemu ambayo ipo katikati ya korodani na sehemu ya kutolea choo kubwa, Maumivu ya korodani na uume
- Mwanaume mwenye tatizo hili anaweza akawa na homa
Iwapo saratani ya tenzi dume imesambaa mwilini kiasi cha kuhusisha sehemu za jirani ya mwili, mgonjwa anaweza kuwa na
- Maumivu makali ya mifupa katika maeneo ya nyonga, mapajani na kiunoni
- Uume kushindwa kusimama (uhanithi)
- Aidha, mgonjwa huwa na dalili nyingine zinazoweza kumpata mgonjwa mwingine yeyote wa saratani kama vile kupungua uzito, kuhisi kichefuchefu, uchovu, kizunguzungu n.k
TIBA
Matibabu ni ghali na mara nyingi wagonjwa hushauriwa kufanyiwa upasuaji ambao huwa ni gharama. Matibabu yake yanaweza kujumuisha upasuaji wa kuondoa korodani, matumizi ya dawa za kupunguza kiwango cha homoni ya testosterone katika damu (hormonal therapy), au matumizi ya kemikali za kuua seli za saratani (chemotherapy).
Upasuaji
Upasuaji hufanyika kwa wagonjwa walio katika hatua za awali za ugonjwa (stage I na stage II) ingawa pia hufanywa kwa baadhi ya wagonjwa walio katika hatua za mwisho za ugonjwa huu yaani stage III na stage IV. Upasuaji unaofanywa ni ule wa kuondoa tezi dume pamoja na baadhi ya tishu zinazozunguka tezi hiyo.
Tiba ya Mionzi
Hii ni aina ya tiba inayotumia mionzi kuua seli zenye saratani. Tiba ya mionzi hutumika kutibu saratani ya tezi dume ambayo haijasambaa kwenye sehemu nyingine za mwili. Aidha inaweza pia kutumika kuua masalia ya tishu zenye saratani mara baada ya kufanyika kwa upasuaji.
Madhara anayoweza kupata mgonjwa kutokana na aina hii ya tiba ni pamoja na kushindwa kusimamisha uume au uhanithi, kukosa hamu ya kula, uchovu, ngozi kubabuka, kuharisha na kutoa mkojo uliochanganyika na damu.
Tiba ya Homoni
Hii ni aina ya tiba inayotumia dawa zinazopunguza kiwango au ufanyakazi wa homoni ya testosterone mwilini. Testosterone ni homoni ya kiume inayochochea ukuaji wa tezi dume, hivyo basi matumizi ya dawa hizi husaidia kupunguza ukuaji huu na kusambaa kwa seli za saratani. Tiba ya homoni hutolewa kwa wanaume walio katika hatua za mwisho za ugonjwa huu kwa nia ya kupunguza maumivu na kutibu dalili za ugonjwa. Dawa zinazotumika kwa tiba ya aina hii zimegawanyika katika makundi mawili, zile zinazochagiza uzalishaji wa homoni ya luteinizing (
luteinizing hormone-releasing hormones, LH-RH) kwa mfano goserelin, nafarelin na leprolide; na zile zinazozuia ufanyaji kazi wa homoni ya androgen kwa mfano flutamide, bicalutamide na nilutamide.
Lakini, ipo njia nyingine ya kukabiliana na tatizo hili ambayo ni
TIBA YA SELI SHINA AU CRYSTAL SELI. Crystal cell (stem cells) ni kirutubisho tiba chenye uwezo wa kuhisha seli zilizoharibiwa kwenye tenzi na kuzirekebisha na kusaidia kuchochea uzwalishaji wa seli mpya nzuri zenya afya na hivyo huboresha afya hatimaye kuokoa maisha ya wanaume wengi.
- Crystal cell husimamisha usambaaji wa saratani kwenye sehemu nyingine za mwili. Aidha husaidia kuhuisha na kuchochea uzalishwaji wa seli zilizokufa wakati wa mionzi au upasuaji.
- Crystal cell inasaidia thibiti, kuboresha na kubalance uzawalishwaji wa homoni ya testosterone katika ume inayochochea ukuaji wa tezi dume bila mpangilio kutoka na uhitaji wa mwili na hivyo hupelekea kupunguza ukuaji na kusambaa kwa seli za saratani
MADHARA ENDAPO MATIBABU YATACHELEWA
Madhara yanayoweza kusababishwa na utumiaji wa dawa hizi ni pamoja na kichefuchefu na kutapika, upungufu wa damu, kuongezeka uzito, uhanithi na kukosa hamu ya tendo la ngono, matatizo katika ini na matiti kuwa makubwa.
- Kusambaa kwa bacteria mbalimbali katika damu(bacteremia)
- Kuwa na jipu kwenye tezi dume(prostatic abscess)
- Ugumba kutokana na kuathirika kwa manii,mbegu za kiume
- Pia tatizo hili linaweza likasababisha kansa ya tezi dume(prostate cancer )
kwa ajili ya maswali,ushauri,na maelezo kuhusiana na crystal cell na hili tatizo na matatizo mengine