Kiranga
Platinum Member
- Jan 29, 2009
- 87,509
- 151,756
Hahahaa,Claude Shanon amekuteka
Claude Shannon umemjulia wapi wewe mchizi?
Hahahaa,Claude Shanon amekuteka
Hata Mimi nashangaa Jua kuning'inia juu kwa juu bila kuanguka , mtasema mambo ya gravity, na hiyo nguvu nani kaiweka ? Please!! What's the first cause? Also who caused the first cause ??
Haya mambo ukijua kusoma Kiingereza wala hayashangazi.brother hata Mimi nilikua blind,kupitia mabandiko yako yenye fact na nondo zilizoshiba niliamua kua free minded nikaanza kuona mambo kwa jicho la tatu na niaanza kuishika elimu na kusoma mambo yenye logic na contradictions kiujumla,
Kiufipi kipindi nilipo ingia secondary tu nilianza kua mtu mwenye kuhoji mambo magumu Kama hayo sikupata majibu
Nilikua nashangaza sana mbaka Kuna baadhi ya watu wakasema nimechizika ila misimamo yangu haikuwahi kuyumbishwa
Sio hivyo tu hata kifamilia niliahawahi kalishwa kikao na wafia dini fulani nikanushe maneno yangu nikawaambia walete uthibitisho juu ya huyo wanaesema yupo wakapoteana vikabaki vitisho tu!
Big up mkuu
Siku ukinipa usahihi wa mantiki katika kuhoji au kuujua ukweli,sitajadiliana tena wewe kuhusu hii kadhia.Hoja ya "first cause" inatokana na ushamba wetu wa kufikiri kwamba mambo yote yapo sawa na mambo ya dunia tunayoiona.
Mara nyingi watu wanaoamini uwepo wa Mungu hutumia hoja ya "ulimwengu usioonekana" kujenga hoja ya kuwepo kwa Mungu, kwa hadithi tu ambazo hazithibitishiki.
Na hutumia hoja ya "first cause" kulazimisha lazima kuwe na first cause, na hiyo first cause ni lazima iwe Mungu.
Mpaka hapo, hata ukiwakubalia kwamba lazima kuwe na first cause, hoja yao ina makosa ambayo kilatini yanaitwa "non sequitur".
Unaelewa kwamba hata kuandika hapa umetumia mantiki?Siku ukinipa usahihi wa mantiki katika kuhoji au kuujua ukweli,sitajadiliana tena wewe kuhusu hii kadhia.
Ila sababu najua fika huwezi jambo hili,sidi huwa tuna vunja misingi ya mantiki. Kati ya uhalisia na mantiki kipi kilianza...? Sababu mantiki ni matokeo ya namna ya ufikiriaji wa kimakosa wa kina Aristoto.
Ukiweza kuthibitisha ukweli juu ya uchunguzi huu,kadhalika utarejea nilichokiandika hapo juu. Mtu mwenye akili timamu hawezi kusema haya kisha akiombwa ushahidi na kueleze mchakato wa hadithi hizi na utungwaji wake ulianzaje na ilikuwaje unashindwa. Hapa ndipo unaona madhara ys kuhoji mambo kwa misingi ya mantiki.Ukichunguza sana utaona hizi ni hadithi za kutungwa na watu tu, huyo Mungu anayesemwa hayupo.
Sijatumia mantiki yoyote sababu uandishi ulikuwepo kabla ya kuwepo mantiki,mantiki ni fani kama zilivyo fani nyingine kama uhandisi umeme,ujenzi,uchawi,ushairi. Laiti kama ungekaa siku na kujiuliza imekuwaje hizi fani zikawepo,hui ujinga wa Mantiki usingekuwa marejeo yako.Unaelewa kwamba hata kuandika hapa umetumia mantiki?
Si kweli sababu,hapa naandika uhalisia,na mantiki inajiweka mbali sana na uhalisia kwa namna yake ya kuhoji na kuhitimisha,kama ulivyo fanya hapa,yaani huwa hamgusi hakika ya hoja bali mnaipitia juu juu,ndiyo maana maisha yenu yote mnaishi katika makosa.Kwa hivyo kama mantiki ni namna ya ufikiriaji wa kimakosa, na haya uliyoandika hapa ni makosa pia?
Kauli hii inakuwa batili sababu haina uthibitisho. Mathalani nikikwambia fulano hayupo. Kuna njia nyingi za kuonyesha hayupo.Swali dogo tu la kuthibitisha kwamba Mungu yupo linapokuwa halijibiwi kimantiki, na linapigwa danadana za longolongo nyingi sana, linaonesha huyo
Matumizi ya tamko "nge" katika uhojaji,huonyesha dhana,na dhana ambayo iko chini ya asilimia hamsini pasi na kuungwa mkono na shahidi hii haifanyiwi kazi sababu inakuwa ni UONGO.Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote angekuwepo asingekuwa mkatili hivyo ajifiche sana, watu wauane katika vita za kidini wakibishana kumtafuta.
Umejuaje hili ?Mungu huyo angekuwepo ingekuwa kila mtu anazaliwa akimjua kwa urahisi tu, bila kuhubiriwa, bila kuhitaji kitabu, bila ya watu tofauti kumjua kiutofauti
Kwa uthibitisho gani ? Hizi dhana za "nge" ? Inakuaje unaikosea adabu akili uliyo pewa bure ?Mpaka hapo tu utaona huyu Mungu anayesemwa na watu katungwa tu na watu.
Nikiliangalia gari au mfumo mzima wa gari , na kuwa siamini kama mwanadamu ndo ameanzisha huu ufahamu, wazungu kuna kitu wanatuficha.Kama mechanism ya gari ilikua haiwezekani ku imagine kua ipo tu na haina mtengenezaji basi hapo utakubali kua kila kitu ambacho kwako kinakustaajabisha kwa ufanisi wake ni lazima kiwe na chanzo
Gari lina chanzo ambacho ni mtu na mtu actually mtu anaweza kuthibitishika hilo halina ubishi, lakini naye huyo mtu umempachika chanzo chake kua ni "Mungu" je unaweza kuthibitisha?
Je hicho chanzo cha mtu (Mungu) nini kimesababisha chanzo hicho kikawepo? ( chanzo cha mungu)
Itakua ni ujinga kusema gari linamtengenezaji mtengenezaji wa gari anamtengenezaji ila aliyemtengeneza mtengeneza gari hajatengenezwa (hana chanzo)
Mtu anaye kubali chanzo cha mtu (Mungu) kua hakina chanzo, mtu huyo anakua hana tofauti na yule anayesema gari ulimwengu hauna chanzo
Mimi mchawi. I know that which thou know notHahahaa,
Claude Shannon umemjulia wapi wewe mchizi?
I wonder how they know this, mfumo wa engine ni wakushangaza Sana, na si engine tu vitu vingi sana vilivyoundwa na mwanadamu vinashangaza , unajiuliza wamepata wapi hii knowledge ya kutengeneza haya mavitu ,
Wazungu kuna vitu wanavijua na wametuficha sisi maniga.
This knowledge is beyond human thinking capacity, there is someone who transfer this knowledge to white people.
Sent using Jamii Forums mobile app
Isaac Newton THE FATHER OF PHYSICS anakubali Mungu yupo. Kiranga et al wanasema hayupo. Kazi kweli kweli.Elimu ya kumjua Mungu ipo katika realm tofauti na hii casual realm, hii ni sawa katika physics kuna Classical physics na modern physics, kuna mambo huwezi kuyatanzua kupitia classical physics ila lazima upitie modern physics halikadhalika kumjua Mungu kuna njia zake alizotuwekea na wala sio hizi njia za crude-casual analysis ambazo watu wasiojua wamejitungia kulingana upeo wa akili zao.
Kumjua Mungu yataka unyenyekevu mbele yake ili ajidhihirishe kwako na sio Egos za nafsi kwani Mungu ni Supreme.
Kama mtu hajui kucheza mchezo fulani kwanini uulaumu huo mchezo kuwa ni mbaya na asilaumu uwezo wake mdogo wa kuweza kucheza mchezo huo??? Ndio hivyo kutokumjua kwako Mungu usihitimishe kwamba Mungu hayupo bali kagua uwezo wako kiakili uliofanya ushindwe kumjua Mungu, ni mambo Mengi katika Mazingira yetu bali ndani yetu sisi wenyewe yanayotosha kwa mwenye akili kujua kwamba kuna A Conscious Supreme creator.
Wenye busara hutafakari na kuomba msaada ili Mungu azidi kuwaongoza na milango ya perceptions za utambuzi wao izidi beyond the 5 senses.
Swali dogo tu la kuthibitisha kwamba Mungu yupo linapokuwa halijibiwi kimantiki, na linapigwa danadana za longolongo nyingi sana, linaonesha huyo Mungu hayupo, katungwa na watu tu.
Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote angekuwepo asingekuwa mkatili hivyo ajifiche sana, watu wauane katika vita za kidini wakibishana kumtafuta.
Mungu huyo angekuwepo ingekuwa kila mtu anazaliwa akimjua kwa urahisi tu, bila kuhubiriwa, bila kuhitaji kitabu, bila ya watu tofauti kumjua kiutofauti.
Mungu huyo kuwa na utata mwingi kujulikana kwa watu wa dunia nzima, ni ukatili wa hali ya juu, kitu ambacho kina contradict upendo wote anaosemwa kuwa nao Mungu huyo.
Mpaka hapo tu utaona huyu Mungu anayesemwa na watu katungwa tu na watu.
Ndiyo maana utasikia wanampa tabia za watu. Mara Mungu kakaa kwenye kiti cha enzi, sasa Mungu anakaa kwenye kiti anaogopa kuanguka?
Mara Mungu kakasirika, hivi huyu Mungu hana control ya hasira zake? Mungu anayejua kila kitu kitakachotokea anaanzaje kukasirika?
Mara Mungu kaona watu hawamfuati kawaua kwa gharika, ina maana alivyoumba hakujua hawatamfuata?
Mara Mungu ataunguza mabilioni ya watu kwenye moto wa milele.Hivi huyu Mungu anawanyima watu neema ya kumjua, wengine hata kusoma vitabu vyake hawawezi, halafu watu hao awachome motoni milele? Huyu ndiye Mungu mwenye upendo wote kweli jamani?
Ukichunguza sana utaona hizi ni hadithi za kutungwa na watu tu, huyo Mungu anayesemwa hayupo.
Uhakika wa logical consistency.Ww una uhakika gani Mungu hayupo?