Pole sana inaonekana hujui hata maana sahihi ya hayo maneno, 'tiini mamlaka'. Mungu huruhusu hata uwepo kwa utawala mbaya kwa makusudi maalumu. Mojawapo ni kwaajili ya kuwaadhibu waliokengeuka. Kunapokuwa na dalili hizo, wanadamu hutakiwa kutubu kwa dhamira ya ama Mungu awaondolee utawala dhalimu au amjalie mtawala hekima ili baraka za Mungu zipate kushuka juu ya nchi.
Kutubu kuna maana ya kuomba upatisho kwa Mungu. Mfalme akifitinika hulaanika yeye, utawala wake na wanaotawaliwa. Ndiyo maana ni muhimu kwa watawaliwa, wakati wote kutaka uwepo upatisho kati ya mtawala wao na Mungu ili neema ya Mungu ishuke kwa watu wote.