Kutoka Mwakyembe hadi Zitto Kabwe

Kutoka Mwakyembe hadi Zitto Kabwe

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Hii sasa ni zamu rasmi ya Zitto Kabwe. Zamu ya kuongea ukweli mchungu kwa wenye nyadhifa serikalini na kuwachomoa walipo. Kuwafanya wajiuzulu kwa kashfa za moja kwa moja au kuwajibika kwa pamoja kama si mkuu wa mahali fulani. Zitto amekabidhiwa penati ya mwisho ya ushindi au kushindwa.

Mwaka 2008 ilikuwa zamu ya Dr. Harrison Mwakyembe. Alilishughulikia ipasavyo suala la Richmond na kuwaangusha wahusika, akina Lowassa,Karamagi,Msabaha na wengineo. Dr. Mwakyembe,akisaidiwa na weledi wake wa sheria,alikusanya nyaraka na shahidi nyingine kuuambia umma ukweli na kusafisha serikali.

Mwaka 2013,ikawa zamu ya Ndugu yangu James Lembeli. Akaishughulikia ipasavyo kadhia ya Operesheni Tokomeza kwa ustadi mkubwa. Hatimaye,akina Mathayo,Nahodha na Kagasheki wakaacha nyadhifa zao. Serikali ikajivua gamba.

Zitto,ambaye kitaaluma ni mchumi,anapaswa kuvaa viatu vya Mwakyembe na Lembeli. Kuibuka na uthibitisho wa uharamu wa jambo husika na kusafisha serikali. Kiukweli, Zitto ana kazi ngumu mbele yake. Ushahidi,watuhumiwa na hatma yao.Vyote viwepo.

Kuna jambo halijulikani kwa wengi. Kwa kadhia kama hizi,mwenye nchi huwa na taarifa na amesharidhia la kusemwa lisemwe;la kutendwa litendwe. Hivyobasi,waongozaji kama Mwakyembe, Lembeli na Zitto "hulindwa".Na waongozaji wote huwa watu wa "mfumo".

Twende taratibu tujionee. Ni zamu ya Zitto

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
Ndio nini sasa? Unaamanisha kutoka CCJ hadi ACT Tanzania? Ninayo list ya walioficha fedha Uswis!
 
  • Thanks
Reactions: DSN
Kwa jinsi Hamasa ya huu mchezo ulivyo naona dhahiri Zitto Kabwe akipaisha hii penalt Au kuigongesha mwamba na ushindi uende pasipotarajiwa..........binafsi nimekaa moyo unadunda Zitto atatutoa kimasomaso Au kichwa ChiNi? Nasubiria hiyo Siku.
 
Mzee wa Lumumba kuna Uzi umeondolewa hapa haraka sana joni hii -ukizungumzia Balozi Sefue kuwapo Dodoma kuwasilisha Barua toka Magogoni sijui hilo linawezakuleta mkanganyiko kwenye kazi ya Kamati ya PAC

Kwa hali ilivyo,mjadala hauepukiki

Mzee Tupatupa
 
Kwa kinywa changu na bila kushawishiwa na mwanasihasa yeyote zito anauwezo mkubw naninaamini atawasimamia kooni wahusika
 
Kwahili "mfumo" upo upande wa wananchi ndio maana wahusika wanahaha usiku kucha....
 
aliyeshindwa kichuguu ( majina ya uswisi ) ataweza mlima ( escrow) ?
 
Zittod will do the best.. im proud of him, he is going to make it to the top patriotic leaders again......tumtie moyo, cha muhimu hiyo mijizi tuishkishe adabu ...... Mungu mwenyewe amtangulie Zitto...Brother, you have Full support from our side,.....
 
Kwa jinsi Hamasa ya huu mchezo ulivyo naona dhahiri Zitto Kabwe akipaisha hii penalt Au kuigongesha mwamba na ushindi uende pasipotarajiwa..........binafsi nimekaa moyo unadunda Zitto atatutoa kimasomaso Au kichwa ChiNi? Nasubiria hiyo Siku.

Mkuu Zitto huyu tunayemfahamu? Kama niyeye nakwambia atapaisha makusudi kwa sababu maslahi! Mana hana tofauti kwasasa nahao mafisadi ni sawa na ndege wanaofanana huruka pamoja,nyie subirini ndio mtamjua Zitto ninani!
 
Zito aitumie hii fursa itamrudisha kwenye chati. Ila akiendekeza bei tutajua pia.
 
aliyeshindwa kichuguu ( majina ya uswisi ) ataweza mlima ( escrow) ?

hivi jk sindio aliempa huyo zito hayo maraka sasa zito anaubavu gan wa kumzuru jk na pinda kisiasa ilihari ndio mabosi wake hiki ni kiinimacho
 
Hii sasa ni zamu rasmi ya Zitto Kabwe. Zamu ya kuongea ukweli mchungu kwa wenye nyadhifa serikalini na kuwachomoa walipo. Kuwafanya wajiuzulu kwa kashfa za moja kwa moja au kuwajibika kwa pamoja kama si mkuu wa mahali fulani. Zitto amekabidhiwa penati ya mwisho ya ushindi au kushindwa.

Mwaka 2008 ilikuwa zamu ya Dr. Harrison Mwakyembe. Alilishughulikia ipasavyo suala la Richmond na kuwaangusha wahusika, akina Lowassa,Karamagi,Msabaha na wengineo. Dr. Mwakyembe,akisaidiwa na weledi wake wa sheria,alikusanya nyaraka na shahidi nyingine kuuambia umma ukweli na kusafisha serikali.

Mwaka 2013,ikawa zamu ya Ndugu yangu James Lembeli. Akaishughulikia ipasavyo kadhia ya Operesheni Tokomeza kwa ustadi mkubwa. Hatimaye,akina Mathayo,Nahodha na Kagasheki wakaacha nyadhifa zao. Serikali ikajivua gamba.

Zitto,ambaye kitaaluma ni mchumi,anapaswa kuvaa viatu vya Mwakyembe na Lembeli. Kuibuka na uthibitisho wa uharamu wa jambo husika na kusafisha serikali. Kiukweli, Zitto ana kazi ngumu mbele yake. Ushahidi,watuhumiwa na hatma yao.Vyote viwepo.

Kuna jambo halijulikani kwa wengi. Kwa kadhia kama hizi,mwenye nchi huwa na taarifa na amesharidhia la kusemwa lisemwe;la kutendwa litendwe. Hivyobasi,waongozaji kama Mwakyembe, Lembeli na Zitto "hulindwa".Na waongozaji wote huwa watu wa "mfumo".

Twende taratibu tujionee. Ni zamu ya Zitto

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

Katika watu ambao nitawakumbuka katika maisha yangu yaliyobaki waliondani na waliowahi kuwapo CCM na wewe upo.Maana kwenye ukweli haukwepeshi,hauogopi unatanua tu kama kawa.Hongera.

Cha msingi tunatakiwa kuwa wamoja sasa kuliko siku nyingine zote.Ninauhakika ZItto walikosea hapo mwanzo sasa ni wakati wake kuirudisha ile hadhi yake ya awali.

Tumuombee awe na ujasiri na subira,Uzalendo na busara.
 
Zitto wa zamani si sawa na huyu wa sasa,mnaomshabikia mtatafuta pa kujificha baada ya kuwatosa na kulalia kwa mafisadi! Ameshakuwa sehemu ya mfumo fisadi na wala tusitarajie lolote zaidi ya kuwasafisha wezi
 
Back
Top Bottom