Wakuu kumepambazuka vema,
Viunga vya mahakama kuu vimetulia, watu wakiendelea kuwasili tayari kwa usikilizwaji wa pingamizi la Zitto Kabwe kutaka kamati kuu ya chadema isijadili utetezi wake,
Tumejiandaa vema kuwaletea kinachojiri na kuzuia upotoshaji mkubwa uliofanywa jana na kundi la wasaliti hawa wa mageuzi,
NB
Kamati kuu ya chadema inaanza kikao chake kama kawaida hivi punde na Zitto ataanza kutajwa ndani ya vikao hivyo baada ya saa tatu kamili asubuhi hii,
Pipoooooz!!!!!!!
UPDATES
Bado ukumbi wa kusikiliziwa shauri husika haujapangwa, nimeelezwa na mapokezi kuwa hivi punde watapanga na shauri litaanza kusomwa saa tatu,
Makamanda wengi wamashawasili, pikipiki zenye bendera za chadema zimetanda mahakamani,
Hali ya hewa ni nzuri ambapo nyuzi joto linakadiriwa kuwa 26 tu hivyo makamanda waliovalia suti wapo salama kabisa,
Tunaendelea .....
APDATES
Zitto yupo hapa mahakamani tangu saa 12 asubuhi, amejificha kwenye gari aina ya Carina no T564 CAS, anawalinzi wa nne wenye miili dhaifu (fizikali), kwakumuonyesha kuwa nimemuona, nimeenda kuengemea gari hiyo hiyo na huku napost updates,
Naaaam
Tumeruhusiwa kuingia ukumbini na kila mtu ametakiwa kuandika jina lale kwenye kitabu cha wageni wa mahakama,
Haya Zitto nae ameshushwa kwenye gari na wapambe wake wanne, anaingia sasa nae mahakamani,
Jambo lakufurahisha leo nikuwa Zitto amevaa mavazi ya SANDA,
Yaani meupe kama .....!
Wooooooooiiiiii Zitto anazomewaaaaaa CCMmmmmmmmmm, duuuuuh hii hatari ukumbi mzima umelipuka kwakumzomea, alianza kuwambia watu pipoziii, hahaa watu wakamjibu kwa kumzomea sana,
naaam watu wametulia wakimsubili jaji Utamwa aje akate mzizi wa fitina
UPDATES,
Wakili wa Zitto Bwana Msando ameshawasili, hahaa kaja moja kwa moja kunishika mkono, sijasita, nimemsalimia tena kwakicheko huku nikimwambia leo mnapigwa chini rasmi,
Bado mawakili wa Chadema bado hawajafika, tunawasubiri
UPDATES,
Mwanasheria mashuhuri katika ardhi ya Tanzania ndugu Tundu Lissu ndio anawasili, wapi pipooooooz!!!!
Watu wanashangilia hamna mfanoooooooo!
Heheeee kweli nguvu ya umma ni balaaa
UPDATES,
Wakili Kibatala ameingia, watu wanaendelea kushangilia,
Saaa tunamsubiri jaji Utamwa tu