Kutoka kwa Abdul Nondo

Kutoka kwa Abdul Nondo

Unanijua mimi ni nani wewe? Kwani ni yeye pekee kapitia madhila na wakati mgumu?

Tii mamlaka iliyopo madarakani hata tumeamriwa hivyo kwenye maandiko matakatifu.

Amri!
Maandiko yale pia ni tungo za kiutawala
 
Utatii dictator? Utatii ukatili? Utatii mauaji? By the way, maandiko unayajua wewe, kuna wapagani wasio na dini wala Mungu, andiko hilo haliwahusu!
Maandiko yapi??? Tungo za wanyonyaji tuu hizo
 
Pole sana
Najua umechagua fungu jema na sio la na crazy psychopath walahi
Good luck on your endeavors walahi
 
Yule jamaa ana vibweka sana.Eti anajipigapiga kifuani kama anaumwa kifaduro na kujiita yeye ni kichaa.Zamani zile tungesema yeye ni "mental"!
Halafu ukitaka kujua kuwa yule jiwe ni kichaa kweli muite "Kichaa Jiwe" hadharani uone timbwiri lake. Anakuwa kishasahau kuwa alijipa hayo majina yeye mwenyewe mbele ya kamera hahaha.
Frustrations ÷ madness = predicaments to the ruled class
 
Habari watanzania.

Kwanza napenda kumshukuru Mwenyezimungu,kwa kunisimamia na kunilinda mara zote,natoa shukrani zangu za dhati kwa Mtandao wa watetezi wa haki za binadamu (THRDC) chini ya mkurugenzi wake Onesmo Olengurumwa Kwa kusimamia uendeshaji wa kesi yangu kuanzia mwanzo hadi mwisho, bila kusahau kituo cha haki za binadamu Tanzani (LHRC),pia shukrani zangu za dhati kwa Mawakili wangu Jebra Kambole(based in Dar) na Chance luogo(based in Iringa).kwa uwezo wao wa utetezi imara katika kesi yangu,na kusimama kwangu pia kama washauri na wafariji kwangu Mungu awabariki sana.

Pia napenda kutoa Shukrani za dhati kwa viongozi na wanachama wenzangu wa TSNP ,pia ndugu zangu,jamaa , marafiki na watanzania wote kwa maombi yao,faraja na matumaini kwangu,Mungu awabariki sana.

Mwisho,napenda kupongeza Mahakama ya hakimu Mkazi Iringa kwa kutenda haki kwa kufuata sheria na taratibu zote katika utoaji haki,bila kusahau nawashukuru pia wanasheria wa Serikali (State attorneys) kwa kuleta mashahidi wao kwa wakati kufanya kesi yangu kuwahi kuisha ndani ya miezi 9.

Nilisimamishwa chuo kutokana na sheria iliyopo ,sasa kesi imeisha namshukuru Mungu,utaratibu rasmi utafanyika mimi kuendelea na masomo hilo ndio jambo kubwa lilopo mbele yangu,kuhakikisha namaliza masomo yangu salama kwa muda uliobaki (one semester)

Sina nia ya yeyote ya kufungua shauri ,au kuomba madai kwa mtu yeyote au taasisi yeyote hili kwangu sio jambo la msingi ,na sina chuki na Mtanzania yeyote, au taasisi yeyote yote yametokea yametokea(Forward Ever Backward Never).Namshukuru mwenyezimungu kwa yote.

Nawaomba watanzania wote ,au taasisi yeyote kwa kipindi nilichokuwa katika changamoto kama niliwahi udhi au kukosea yeyote naomba radhi naomba kusamehewa .mniruhusu kuanza maisha yangu yakawaida kwa upendo na amani.

Hakika nina upendo wa dhati kwa kila Mtanzania ,kwa Taasisi yeyote, kiongozi yeyote ,bila kujali rangi,dini,kabila au chama cha siasa.

Mungu atujalie Afya njema,upendo na amani kwa maslahi ya jamii yetu na Taifa letu kwa ujumla.

Wako.

Abdul Omar Nondo.
abdulnondo10@gmail.com

Mwenyekiti mstaafu wa TSNP.

The right meaning of a word gentleman...... Good
 
Mwisho wa ubaya ni aibu,mapambano yanaendelea,maliza Kwanza masomo yako.###abdul nondo.
 
Halafu ukitaka kujua kuwa yule jiwe ni kichaa kweli muite "Kichaa Jiwe" hadharani uone timbwiri lake. Anakuwa kishasahau kuwa alijipa hayo majina yeye mwenyewe mbele ya kamera hahaha.
Frustrations ÷ madness = predicaments to the ruled class
Nilisahau kama alisemaga ana "fulasitesheni"! Hahahahaaaa!Vibweka country!
 
Utatii dictator? Utatii ukatili? Utatii mauaji? By the way, maandiko unayajua wewe, kuna wapagani wasio na dini wala Mungu, andiko hilo haliwahusu!
Tii wewe!
Mbona kwenye chama chetu hata tukiletewa FISADI ligombee URAIS na mwenyekiti sote lazima tutii.
Hakuna kugombea nafasi ya uwenyekiti sote tunatii.
hata udikteta tii tu! Vinginevyo tutakuita MSALITI kama tulivyowaita akina Zitto walipokataa kutii amri ya kutogombea uwenyekiti na yule "MSALITI" Dr Slaa aliyegoma FISADI kugombea URAIS kupitia chama chetu.
Ukitaka uishi kwa amani we TII tu!
 
Pole sana jembe.
Nadhani wabaya wako wameumbuka.
Pia vipi kuhusu ishu ya uhamiaji mmeshamalizana au bado wanatafuta nchi ya kukupeleka wakufanyie kama Migunamiguna?
 
Tii mamlaka iliyopo madarakani hata tumeamriwa hivyo kwenye maandiko matakatifu.

Amri!
Mkuu kuna watanzania hawayajui hayo maandiko wala hawakijui hicho kitabu, nafikiri unajua kuwa Tanzania ina zaidi ya makabila 250,watanzania ni jamii ya watu mchanganyiko kama tunataka Amani itawale kwenye nchi yetu basi kila mtu apewe heshima yake, acha ubinafsi mjomba
 
Tii wewe!
Mbona kwenye chama chetu hata tukiletewa FISADI ligombee URAIS na mwenyekiti sote lazima tutii.
Hakuna kugombea nafasi ya uwenyekiti sote tunatii.
hata udikteta tii tu! Vinginevyo tutakuita MSALITI kama tulivyowaita akina Zitto walipokataa kutii amri ya kutogombea uwenyekiti na yule "MSALITI" Dr Slaa aliyegoma FISADI kugombea URAIS kupitia chama chetu.
Ukitaka uishi kwa amani we TII tu![/QUOTE
]
Hivi umerudia kusoma ulichoandika mkuu?Mbona kama unajing'ong'a?
 
Back
Top Bottom