Kutoka Bungeni Dodoma: Julai 18, 2011

Kutoka Bungeni Dodoma: Julai 18, 2011

Wakuu hivi kuna online radio yoyote au tv inayorusha bunge? kwa watu tulio nje ya bongo tupate kuona au kusikia! msaada plse


mimi nimefanikiwa kuangalia via online na ni rahis sana wacha nikupe procedure mkuu...kama link yako iko poa utaona ...ukimaliza kila kitu copy link hii na paste kwenye browser yako:
rtsp://196.28.65.226/diactus/movie.3gp?weUE9Qdy3GHWo2-5Tpic3b47H(i8afKugOTAdmjZcV1ljArP1641PQ7ee3h-yN20


NB kopy kama ilivyo hiyo link..


  • 1 Download VLC Media Player (see Resources).




  • 2 Install and open VLC Media Player.
  • 3 Click "Media," then click "Open Network Stream."
  • 4 Type or copy and paste the address of the RTSP stream you want to view and click "Play."
    .................................................. .................................................. .................................................. .................................................. .........

kwa kwa mnaotaka kuangalia hii link hapo juu, fanyeni hivi,

Lazima uwe na VLC au window media player,Winamp, n'k. Mimi natumia VLC na nitawaonyesha namna ya kutumia VLC,


Kama hauna VLC download hapa
VideoLAN - VLC: Official site - Free multimedia solutions for all OS! baada ya ku-istall ifungue VLC
 
Japokuwa spika aliwanyima ruhusa wabunge wa CDM kutochangia mjadala huu, lkn leo ameona kwamba kumbe la kuvunda halina ubani wabunge wote waliochangia wamemsulubu Geresha, mimi nina wasiwasi na hicho kikao cha wabunge wa CCM saa saba mchana wanaenda kujadili nini?
 
Japokuwa spika aliwanyima ruhusa wabunge wa CDM kutochangia mjadala huu, lkn leo ameona kwamba kumbe la kuvunda halina ubani wabunge wote waliochangia wamemsulubu Geresha, mimi nina wasiwasi na hicho kikao cha wabunge wa CCM saa saba mchana wanaenda kujadili nini?


kuna post yangu moja nimesema kuna njama ccm watafanya ili waipitishe hii bajeti......wacha nisubiri
 
Jeykey, Si kweli, fuatilia hii thread utakuta kuna wabunge wa CDM wamechangia!
 
Hawana kitu hawa, wakishawekwa sawa utafikiri sio hao waliukuwa wanakataa. Hivi washaitana, tutaona session ya jioni...Mark my words!
 
  • Thanks
Reactions: FJM
Rafu na faul nyingi zimeanza kuchezwa / kufanywa na CCM siyo KAWE tu ni sehemu mbalimbali za nchi -mfano mzuri ni kama Mwanza, Mbeya ma nk. lakini wananchi hawadanganyiki hadi kieleweke. Kuhusu Bunge leo Kwigangala ameongea tangu aingie Bungeni, ngoja tuone wamekwenda kupewa Lunch na Ngeleja- CCM watakaporudi watakuwa wamelainika. Yetu macho. Chadema simameni imara hadi kieleweke.
 
CCM yamwaga pikipiki Kawe Monday, 18 July 2011 08:11 newsroom NA KHADIJA MUSSA CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimetoa pikipiki 15 kwa vijana wa jimbo la Kawe, Dar es Salaam, ambapo pia kimezoa wanachama wapya 200, baadhi wakiwa kutoka vyama vya upinzani. Pikipiki hizo ni sehemu ya 26 zilizotolewa na Chama kwa ajili yavijana, ambapo 11 zimepelekwa mkoani Singida. Jumla ya gharama ya pikipiki hizo ni sh. milioni 46.8. Wanachama hao walijiunga na CCM jana, kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Tegeta, ambao uliohutubiwa na Katibu wa NEC yaCCM, Uchumi na Fedha, Mwigulu Nchemba. Kwa mujibu wa wanachama wapya, wamevutiwa na sera za CCM, hivyo kuamua kujiunga na Chama. Nchemba katika mkutano huo uliohudhuriwa na umati wa wananchi, wanachama na wapenzi wa CCM, alikabidhi pikipiki 15 kwa vijana wa jimbo hilo. Alisema pikipiki hizo zimetolewa kwa mkopo, ambapo vijana watatakiwa kuunda vikundi na kukabidhi sh. 30,000 kila wiki kwa kiongozi wa kikundi, yakiwa ni marejesho ili kuwezesha kununuliwa nyingine. Katibu huyo wa NEC alisema fedhahizo zitatumika kununua pikipiki nyingine zitakazogawiwa kwa vijana wengine, ambapo kila mwezi mmoja atapatiwa. Aliwataka vijana hao kuwa waaminifu, kwani wakirejesha fedha hizo kwa wakati zitawezesha vijana 360 kupata pikipiki katika kipindi cha miaka mitano. Nchemba alisema pikipikihizo zitawasaidia vijana kujipatia ajira, ikiwa ni utekelezaji wa Ilaniya uchaguzi ya CCM kwa vitendo. Aliwataka viongozi wa vyama vya upinzani kutumia nguvu na akili katika kubuni vitu ambavyo vitawakwamua wananchi kimaendeleo, na si kuchochea vurugu na maandamano, kwani hayana tija kwa taifa. Nchemba aliingia kwenye mkutano huo akiwa amepanda pikipiki, akiwa amefuatana na Katibu wa UVCCM Taifa, Martine Shigela.

pikipiki 360 kwa miaka 5 si maendeleo ya kuleta mabadiliko kwa maelfu ya vijana dar hilo ni changa la macho tu na mbinu za kuwadaka watu. Najus kwamba waliojiunga na ccm hapo ni geresha tu ya kupata mikopo, kwani walikuwa chama gani kabla ya hapo?
 
hakuna mbunge hata mmoja wa chasdema aliyechangia
Si kweli mkuu,wamechangia wabunge wawili wa Chadema viti maalum ambao ni Rebeka Mngodo na yule mama mtu mzima jina la kwanza anaitwa Naomi.......
 
hii link ina mushkeli kidogo...chek upya ulivyoupload hilo file mkuu

bonyeza hiyo link, itafungua browser ambao ni wetransfer, then itakuambia download then ukidownload utakutana na hilo faili, limekuwa recorded.
 
Yupo mbunge mwingine sijui mhindi yule, nadhani anatoka Magu au maeneo kama hayo. Yeye aliunga hoja kwa asilimia mia.
Huyo ni Mansoor mbunge wa Kwimba na Mweka hazina wa CCM mkoa. Ana kampuni ya kuuza mafuta MOIL na vituo vyake ni bingwa wa kuchakachua mafuta jijini Mwanza. Anaunga mkono kwa maslahi yake binafsi.
 
Za mwizi arobaini. Pamoja na mikakati mingi ya 'ndani' ili kuzima wasemaji hodari wa CHADEMA wasichangie, wabunge wengi wa ccm walioongea wamekataa kuunga mkono hoja huku wakitoa orodha ya vitu wanavyotaka virekebishwe i.e Kingwangala anasema atuanga mkono hoja mikataba itapobadilishwa.

Kwa upande mwingine ccm wanaweza kufikiri kuwa mpako hapo wamewapiku CHADEMA na kung'ara kwenye hii hoja ya Ngeleja, lakini hatari inakuja. Kama jioni hii wataunga mkono hoja bila ya majibu (ya kuridhidha) juu ya yale waliyoorodhesha basi neno UNAFIKI litakuwa lao rasmi, na watapata shida sana 2015. Nina wasiwasi haya majigambo ya ccm ni usanii lakini usanii wenyewe haujawa well-thought. In less than 6 hours tutajuwa kama kweli wana ujasiri wa kusimamia yale yote wanayosema au wakipewa 'chai' wanalainika.

Tusubiri.
 
kigwangwala wakamate hivyo hivyo.. Na leo mkiibitisha hii bajeti mchango wako hautakuwa na maana yoyote.
 
Back
Top Bottom