Kachanchabuseta
JF-Expert Member
- Mar 8, 2010
- 7,263
- 684
hakuna mbunge hata mmoja wa chasdema aliyechangia
Wakuu hivi kuna online radio yoyote au tv inayorusha bunge? kwa watu tulio nje ya bongo tupate kuona au kusikia! msaada plse
Baadhi ya michango bungeni leo katika linki hapo chini (audio). Kwa wale ambao hawakubahatika kulisikia, kwa mliosikiliza mpotezee.
http://wtrns.fr/_dZ7KCoREbGAJM
Japokuwa spika aliwanyima ruhusa wabunge wa CDM kutochangia mjadala huu, lkn leo ameona kwamba kumbe la kuvunda halina ubani wabunge wote waliochangia wamemsulubu Geresha, mimi nina wasiwasi na hicho kikao cha wabunge wa CCM saa saba mchana wanaenda kujadili nini?
CCM yamwaga pikipiki Kawe Monday, 18 July 2011 08:11 newsroom NA KHADIJA MUSSA CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimetoa pikipiki 15 kwa vijana wa jimbo la Kawe, Dar es Salaam, ambapo pia kimezoa wanachama wapya 200, baadhi wakiwa kutoka vyama vya upinzani. Pikipiki hizo ni sehemu ya 26 zilizotolewa na Chama kwa ajili yavijana, ambapo 11 zimepelekwa mkoani Singida. Jumla ya gharama ya pikipiki hizo ni sh. milioni 46.8. Wanachama hao walijiunga na CCM jana, kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Tegeta, ambao uliohutubiwa na Katibu wa NEC yaCCM, Uchumi na Fedha, Mwigulu Nchemba. Kwa mujibu wa wanachama wapya, wamevutiwa na sera za CCM, hivyo kuamua kujiunga na Chama. Nchemba katika mkutano huo uliohudhuriwa na umati wa wananchi, wanachama na wapenzi wa CCM, alikabidhi pikipiki 15 kwa vijana wa jimbo hilo. Alisema pikipiki hizo zimetolewa kwa mkopo, ambapo vijana watatakiwa kuunda vikundi na kukabidhi sh. 30,000 kila wiki kwa kiongozi wa kikundi, yakiwa ni marejesho ili kuwezesha kununuliwa nyingine. Katibu huyo wa NEC alisema fedhahizo zitatumika kununua pikipiki nyingine zitakazogawiwa kwa vijana wengine, ambapo kila mwezi mmoja atapatiwa. Aliwataka vijana hao kuwa waaminifu, kwani wakirejesha fedha hizo kwa wakati zitawezesha vijana 360 kupata pikipiki katika kipindi cha miaka mitano. Nchemba alisema pikipikihizo zitawasaidia vijana kujipatia ajira, ikiwa ni utekelezaji wa Ilaniya uchaguzi ya CCM kwa vitendo. Aliwataka viongozi wa vyama vya upinzani kutumia nguvu na akili katika kubuni vitu ambavyo vitawakwamua wananchi kimaendeleo, na si kuchochea vurugu na maandamano, kwani hayana tija kwa taifa. Nchemba aliingia kwenye mkutano huo akiwa amepanda pikipiki, akiwa amefuatana na Katibu wa UVCCM Taifa, Martine Shigela.
Si kweli mkuu,wamechangia wabunge wawili wa Chadema viti maalum ambao ni Rebeka Mngodo na yule mama mtu mzima jina la kwanza anaitwa Naomi.......hakuna mbunge hata mmoja wa chasdema aliyechangia
muwe mnatembelea jukwaa la technolojia huko ndiko huwa tunapeana ma ujanja
procedure zote nilizotoa hapo juu waweza zipata kwa uzuri via link hii https://www.jamiiforums.com/tech-ga...-airtel-tigo-na-hata-zantel-na-voda-hapa.html
hii link ina mushkeli kidogo...chek upya ulivyoupload hilo file mkuu
Huyo ni Mansoor mbunge wa Kwimba na Mweka hazina wa CCM mkoa. Ana kampuni ya kuuza mafuta MOIL na vituo vyake ni bingwa wa kuchakachua mafuta jijini Mwanza. Anaunga mkono kwa maslahi yake binafsi.Yupo mbunge mwingine sijui mhindi yule, nadhani anatoka Magu au maeneo kama hayo. Yeye aliunga hoja kwa asilimia mia.