akiomwa
Member
- Feb 4, 2015
- 34
- 19
Hello ndugu zangu wana JamiiForums,
Natumaini wote ni wazima. Mimi pia ni mzima. Binafsi si mkongwe sana JamiiForums lakini lazima nikiri kuwa JamiiForums imenifungua mengi sana na kunisaidia katika mengi kwa namna moja au nyingine. Kama ilivyo kwa wengi na mimi pia nilikuwa katika mahangaiko ya kusaka ajira hasa serikalini kwa muda mrefu; nilikuwa nikikatishwa sana tamaa baada ya kuona linatolewa tangazo na sekretariati ya ajira huku nafasi ni 1 lakini wanaoigombania ni zaidi ya watu 300.
Nilikuwa siamini kuwa bahati kama hii inaweza ikaangukia upande wangu lakini kupitia ushuhuda ambao wadau walikuwa wakiutoa humu JamiiForums kuwa walifanikiwa kupata kazi serikalini katika competition/ushindani kama huo tena kwa njia halali kabisa na mimi nilikata shauri kupambana nikiamini siku moja mambo yatakaa poa.
Namshukuru sana Mungu na pia nawashukuru sana wanaJamiiForums kwa moyo wenu wa kufunguka na kushare ideas kwani hatimaye jana nilipigiwa simu kuwa nimefaulu kupata kazi katika mamlaka moja ya serikali (TMA/mamlaka ya hali ya hewa) na ndio nipo katika michakato ya kukamilisha taratibu zao ili nianze.
My dear brothers and sisters, never give up!, ukimshirikisha Mungu na kuamini na kuweka juhudi pasipo kukata tamaa kila kitu kinawezekana duniani hapa nothing is impossible (Neno lenye impossible ukilitenganisha linasema I'M POSSIBLE). Msikate tamaa wanaharakati wenzangu, when your time comes no one will be able to stop anything.
Thanks and be blessed much
Nawasilisha
Natumaini wote ni wazima. Mimi pia ni mzima. Binafsi si mkongwe sana JamiiForums lakini lazima nikiri kuwa JamiiForums imenifungua mengi sana na kunisaidia katika mengi kwa namna moja au nyingine. Kama ilivyo kwa wengi na mimi pia nilikuwa katika mahangaiko ya kusaka ajira hasa serikalini kwa muda mrefu; nilikuwa nikikatishwa sana tamaa baada ya kuona linatolewa tangazo na sekretariati ya ajira huku nafasi ni 1 lakini wanaoigombania ni zaidi ya watu 300.
Nilikuwa siamini kuwa bahati kama hii inaweza ikaangukia upande wangu lakini kupitia ushuhuda ambao wadau walikuwa wakiutoa humu JamiiForums kuwa walifanikiwa kupata kazi serikalini katika competition/ushindani kama huo tena kwa njia halali kabisa na mimi nilikata shauri kupambana nikiamini siku moja mambo yatakaa poa.
Namshukuru sana Mungu na pia nawashukuru sana wanaJamiiForums kwa moyo wenu wa kufunguka na kushare ideas kwani hatimaye jana nilipigiwa simu kuwa nimefaulu kupata kazi katika mamlaka moja ya serikali (TMA/mamlaka ya hali ya hewa) na ndio nipo katika michakato ya kukamilisha taratibu zao ili nianze.
My dear brothers and sisters, never give up!, ukimshirikisha Mungu na kuamini na kuweka juhudi pasipo kukata tamaa kila kitu kinawezekana duniani hapa nothing is impossible (Neno lenye impossible ukilitenganisha linasema I'M POSSIBLE). Msikate tamaa wanaharakati wenzangu, when your time comes no one will be able to stop anything.
Thanks and be blessed much
Nawasilisha