Huu sio udhaifu wa ccm wala viongozi wetu ila NI UDHAIFU WA SISI WANANCHI wenyewe, haiwezekani tufanywe wajinga kiasi hiki. Wakati wa ulimboka, Kova alijinadi mbele ya vyombo vya habari kuwa wamemkamata mtuhumiwa mkenya ilhali wakijua ni uongo.
Akafa Mwangosi, tume ya nchimbi wakaja na majibu ya hovyo hovyo tupo kimya tu. Ujinga huo hauwezi kufanywa na nchi nyingine. Tumewapa sisi nafasi ya kufanya yoote na kutudharau kiasi hiki.
umesahau viongozi wenu walivyo shabikia tukio la Dr. Uli?Unajua mtu unapokuwa lishabiki la maCCM directly unakuwa huna utu ndani yako, kitendo tu cha kuwa na kadi ya maCCM ni hatari hata zaidi ya magaidi na watuhimiwa wa ICC, Ukweli ni kuwa Ridhiwani na Nape ni vijana wasaliti na wamwaga damu kwani haiwezekani ushabikie kipropaganda mambo serious tena ya uhai wa mtu kama haya.
Wito: 2015 iwe kufa kipona makamanda yani mpaka kieleweke kwan hata hv sasa tumeshawadekeza vya kutosha.
Mara nyingi uwa nashindwa kufahamu kwanini huyu Ridhiwani na familia ya mkuu wa kaya wamekuwa wakijushughulisha na siasa kwa kiwango kikubwa kuliko familia zote za wakuu wa kaya waliowaishika Ikulu ya DSM. Nashindwa kuelewa kuwa kuna nini nyuma ya pazia. Hivi Mama Maria na akina Madaraka nk walifanya kama haya tunayoyaona kwa akina Ridhiwani? Hivi watoto wa Mwinyi na wake zake walifanya haya anayoyafanya huyu Ridhiwani sijui? Hivi watoto wa Ben ambao hata mimi siwajui na Mama Ben walifanya haya wanayoyafanya hawa wa familia ya sasa ya mkuu wa kaya? Ukweli ni kuwa hii familia ya sasa ya mkuu wa kaya imefanya ikulu kama sehemu ya kupata umaarufu na kuvuna mambo yao kiurahisi. Naomba JK awashughulikie hawa wanafamilia wake, wanatuumiza sana watanzania kwa kauli kama hizi? Hivi kweli mtoto wa raisi unayeweza ukakaa kuanza kuwadharau watu waliomuweka baba yako madarakani? Nani ajuaye kuwa Kibanda nae alikuwa mpiga kura wa JK? Nani ajuaye? Nadhani muda umefika sasa, familia ya Ikulu itambue kuwa kuna siku watatoka pale Ikulu, na wakitoka watarudi kuwa raia wa kawaida.
Mkuu nashukuru kwa kunipa 'like', lakini ukweli ni kwamba tunafahamu au nayafahamu mengi zaidi ya ninayoandika hapa, lakini mara nyingi nahofia 'BAN' na usalama wangu. JamiiForums si mahali ambapo waweza andika kila kitu unachokijua, nashukuru Mungu nimeligundua mapema hilo. Baada ya 'mzee' wangu kufariki nilipata makaratasi na barua za rafiki yake ambaye alikuwa balozi wa TZ katika nchi fulani zilizoelezea vitisho vya kifo kwa huyo balozi, na kwamba anawarudisha nyumbani watoto wake ili wasije wakapatwa na maswahiba huko ughaibuni na nzee ajitahidi kuangalia usalama wao. Mzee wangu na huyo balozi wote walifariki mwaka huo huo, yale makaratasi ulitokea wizi na kuibiwa. Mkuu, mambo ni mazito kuliko wengi tunavyofikiria.
hii yote ni kupoteza ukweli tu, CDM ndio wahusika wa hii kitu mbaya na wanataka kupoteza watu na hii gia ya riz1.
Mkwara wa JF huo, utabaki kuwa chini ya ungozi wa CCM maisha yako yote sio 2015 tu.Nyie endeleeni tu kuimba hizo tenzi zenu za Shaban Robert lakin mkae mkijua 2015 patachimbika hata nuie mawalakala wa lumumba humu JF hatutawaona tena maana mtakuwa mmekimbilia sudan na msumbiji kwenda kuomba hifadhi ya muda, hamtaamin kumuona Riz1 na Nape wanashare kikombe cha uji kwenye makambi ya hifadhi za wakimbizi.
"Hayo ni maoni yake binafsi na wala sio ya chama" unakumbuka haya maneno wakati ule Mtei alivyo ropoka?
Mkwara wa JF huo, utabaki kuwa chini ya ungozi wa CCM maisha yako yote sio 2015 tu.
Sawa mkuu, kumbuka hicho kihama na dhoruba inayokuja itawakuta wote sisi na wewe na familia zetu lakini hao wanao watumia kisiasa watakuwepo Dubai kwenye nyumbe walizo nunua.Piga 2 porojo zako ila subirieni kihama na dhoruba inayokuja 2015, kwani haya maCCM tunaoyaona leo hatutayaona tena. Period.
"Hayo ni maoni yake binafsi na wala sio ya chama" unakumbuka haya maneno wakati ule Mtei alivyo ropoka?
sihitaji udc wala rc kuona ukweli, fata upepo ni nyie washabiki wa CDM.Majebere, hivi na wewe umepewa U-DC au RC au ni bendera fuata . . . .