Kutapeliwa

Polee we,na karibu ndani ya club ya wahanga wa MITANDAONI. Juzi nilileta uzi wa kujinjwa pesa kupitia tigo pesa wachangiaji wakaninanga saana. Jàmani haya mambo yanaweza kukutokea ukabaki unashangaa hasa baada ya kuibiwa. Pole tena Jamaa yangu.
Mkuu matapeli wamezidi kua wajanja mimi nilipigwa laki 3 tu,nikaona ni kama milioni 3 hiv,kumbe watu wanapigwa vibunda virefu hivi.yaani tapeli wakikamatwa saiv nao sio wakuwaonea huruma.wanaliza watu na kuvuruga mipango kabisa na kama ni biashara wanakuingizia loss kubwa sana.
 
Huyo wala sio ndugu ni matapeli itakua walijipanga kumuibia mdau
 
Kila kukicha wajinga wanazaliwa.

............pesa ndefu kama hiyo kwanini hukumpa akaunti namba akadeposit huko?
Sio ujinga hizo mambo zinatokea sana watu wanatapeliwa nyumba na mashamba sembuse milioni 1.
 
hao mbona wepesi tu,nenda polisi kitengo cha cyber.
 
Mkuu hapo walijua kufwatilia kwa mtu mwingine itakuwa kazi maana hatakuwa makini kama wewe, na walijua wataituma muda ambao benki zimefungwa na wewe utakapopata taarifa tuu kuwa imefika utaachia mzigo.
 
huyo kumdaka rahisi sana andaa za kubrashia viatu then nenda kitendo cha vyber crimes polisi Kwakifupi mchezo wanaocheza au mchezo matapeli wenzao wanaocheza ni kwamba wananunua zile bulk sms service ambayo unasajili kwa jina la kampuni kama sender hii wanatumia wafanyabiashara wakubwa wakubwa
ukienda polisi na message wanaweza trace mtumaji wakafatilia kabisa mpaka wakajua iyo package ni nani alinununua inaonekana wanawatapeli wengi
 

Mkuu hapa tunahitaji samalaizi kidogo tupate la kujifunza
 
Hiyo ishawahi nitokea Maeneo ya Kimara(Dar) .
Mchezo ulikuwa kama ifuatavyo.

Nimepewa mzigo toka zenji niufikishe kwa muhusika alouagiza. Mzigo ulikuwa unadhamani ya laki 7 na nikifika anipatie hiyo hela.

Muhusika alilalamika yuko bize muda wa mchana hivyo anaomba tukutane mida ya sa moja na nusu (Hiyo sa moja na nusu nilikuja elewa maana yake badae).
Muda ulipofika bado akachelewa akafika sa 2 . Alikuja na boda boda sehemu aliposema anikute na makubaliano ni kwamba anataka anitumie hiyo hela kupitia NMB maana nikatoe mimi kwani ataweka hadi ya kutolea.
Wasiwasi ukanijaa pia body language yake nilimuona sio mzuri(Kwenye kumsoma mtu nashukuru Mungu ninakipawa cha juu sana) . Nikaitikizia, akatuma hiyo hela tena sio yeye alidai mke wake ndo ataituma ,akampigia kweli mwanamke pale pale nikimskia baada ya dakika 2 nikaona msg imekuja kwangu kutoka NMB kwani alimpa namba zangu . Kilichonihakikishia kuwa sio hela ni hiyo NUKTA ambayo hata wadau wameisema ,Pia msg hiyo ilikuwa inakubali sehem pa ku reply(Navyofaham msg za huduma kubwa nyingi haziruhusu hilo)

Baada ya kuona haufu ya utapeli nilimwambia twende Kimara stendi pale hatuwezi kosa mawakala wakubwa wa ki benk tutoe hiyo hela.
Akadai. Akadai ana haraka ndo maana amekuja na bodaboda wa kukodisha.
Niligoma kataka kata . Na kuna muda nilipanick nika mwambia sababu ya mimi kukataa ni kwamba hii sio hela ila ni msg ili kuondoa huu utata twende tukaitoe wote nikupe mzigo wako.
Akasema kwa vile mimi simuamini basi ngoja anamwambia mkewe aombe wairudishe alafu kesho ataniletea cash. Niliitikia maana niliona nikupotezana Muda . Na baada ya hapo K namba yake haikupatikana ten ndo ikawa pona ya huo mzigo.

HAPO MTOA MADA NI USHATAPELIWA MAANA NILISHAKUMBANA NAYO HII
 
Pale mlinzi hawezi kukusaidia lolote zaidi inabidi upige simu benki husika ambapo watakupa maelezo utembelee branch yao na risiti then hela itarudi kwenye account baada ya masaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole ndugu. Naomba niongeze uelewa kwa ambao hawajui vizuri. Mfano mdogo, Kuna app mfano ambayo nimeambatanisha hapa chini, ukishajisajili na ukilipia, ukimtumia mtu msg haiandiki namba, bali Jina..Mfano BULKSMS, Au Jina analochagua mtumaji, na haioneshi namba. Wana free sms 5, u can try.
 
Kama nihivyo mifumo bank zetu haipo stable inawapa loophole wanaoweza kucheza nayo sasa
 
Ame edit meseji ya benki akaongeza tarakimu!!huu mchezo tumechezeana sana kwenye upatu na washkaji zangu !!!
sasa mbona message imeingia kwa jina la NMB wakati hizo number mbili za airtel hazijawahi kuwasiliana
 
Anatuma kwanza pesa unahakikisha imeingia ndio unakabidhi mzigo Bro.

Watu mpo Darisalama bado mnapigwa kizembe hivyo.
Na si imeingia tu. Na wewe unaihamisha kwenda benki kwa simu na kuhakikisha zimeenda.
 
mzee wewe ni introvert?imekuaje message yake ije kwa jina la NMB? wamefanya mchezo gani hapo.maana I guess wewe na hiyo number ya mke wake hamjawahi kuwasiliana
 
Kama nihivyo mifumo bank zetu haipo stable inawapa loophole wanaoweza kucheza nayo sasa
Kwa uzoefu wangu bwana Bongo kila kitu kindaendeshwa kwa uzembe. Nchi yetu ina watu wavivu na wazembe mno. Umeshakuwa ni utamaduni wetu.
 
hao mbona wepesi tu,nenda polisi kitengo cha cyber.
Shida unakuta kadi iliyotumika kusajilia siyo yake. Hawa wasajili laini ukienda kusajili wanafanya janjajanja wantumia kitambulisho chako kusajili laini 3 baadae wanaziuza
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…