Ila mahusiano na ndoa nyingi zinahusika sana na hayo hapo juu. . . .
Kama ni mke mume anamtambua kama mke jina tu ila matendo mazuri na haki za mke zinaelekezwa kwa mtu mwingine. Mume nae hamna analopata kwa mke zaidi ya kulala nae kitanda kimoja. Kazi zote dada w
a kazi, unyumba hamna na hata anapoongeleshwa anafokewa tu.
Mpenzi/mchumba nae anatreatiwa kama choo cha barabarani akiwa ndani ila nje kila mtu anamkubali na kumsifia kwa kuwa na fulani.
Kweli kabisa
Yaani kuna mazingira unatambulika kama mke na mengine uko kama kioo tuu waka uwepo wako hautambuliki
Yaani mbele za watu wewe ni nobody na wala hatakutambulisha kama mkewe wala mpenzi wake
Ila ukirudi nyumbani mbele ya wale wanafamilia ndo anakutambulisha
na mazingira mengine unatambulishwa nje kama mpenzi au mke ila ndani ya familia yake wewe si lolote wala huna thamani
Haya mambo yapo sana na kwa kweli sometime mioyo ya watu na nyumba zinaficha mengi sana
Unaweza shangaa couple wako sehem wanacheka na kugongesheana glass wakiwa mbele ya watu ila wakiwa pamoja ni fulkl kunua na hakuna maongezi yoyote
Au wanaenda pamoja sehem wakishafika kwenye eneo la tukio kila mmoja na hamsini zake na kila mmioja na rafiki zake na mambo yake