Ulongupanjala
JF-Expert Member
- Apr 9, 2013
- 8,508
- 13,974
Heshima kwenu wakuu?
Imekuwa ni tabia ya walio wengi kuanza kutamani wake/waume za watu,mara tu msiba unapotokea,wengine huanza kusema vibaya watu kuwa je ataweza kuvumilia bila ya kuwa na mwenza?
Kwa mfano hivi sasa waheshimiwa wabunge wamefariki,ila nimeona kwenye mitandao ya kijamii wakiposti picha za wenzi wao na kuanza kuwasifia kwa matamanio,nimeshindwa kuelewa hivi huu utamaduni wa kuwataka wajane kabla ya msiba kuisha umeanza lini? Mtu amefiwa na mwenza wake,wengine wanafika msibani ili kuona neema za Allah jinsi mjane alivyoumbika badala ya kumuombea kheri marehemu huko aliko,binafsi nimekerwa sana na wenye tabia hizo.
Tuelewe kwenye msiba ni sehemu ya maombolezo na sio sehemu ya kutamaniana hasa kwa wafiwa,pia kila nafsi itaonja mauti,ingekuwa wewe ungejisikiaje mkeo/mumeo atamaniwe/atongozwe wakati wewe bado hata kuzikwa/kuoza?
Tubadilike!!!
Imekuwa ni tabia ya walio wengi kuanza kutamani wake/waume za watu,mara tu msiba unapotokea,wengine huanza kusema vibaya watu kuwa je ataweza kuvumilia bila ya kuwa na mwenza?
Kwa mfano hivi sasa waheshimiwa wabunge wamefariki,ila nimeona kwenye mitandao ya kijamii wakiposti picha za wenzi wao na kuanza kuwasifia kwa matamanio,nimeshindwa kuelewa hivi huu utamaduni wa kuwataka wajane kabla ya msiba kuisha umeanza lini? Mtu amefiwa na mwenza wake,wengine wanafika msibani ili kuona neema za Allah jinsi mjane alivyoumbika badala ya kumuombea kheri marehemu huko aliko,binafsi nimekerwa sana na wenye tabia hizo.
Tuelewe kwenye msiba ni sehemu ya maombolezo na sio sehemu ya kutamaniana hasa kwa wafiwa,pia kila nafsi itaonja mauti,ingekuwa wewe ungejisikiaje mkeo/mumeo atamaniwe/atongozwe wakati wewe bado hata kuzikwa/kuoza?
Tubadilike!!!