Kususia michezo ya Olimpiki ya Beijing ni kukiuka haki za binadamu

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,034
Na Caroline Nassoro



Maandalizi ya Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi itakayofanyika Beijing yamekamilika, na wanariadha wanaofanya majaribio katika viwanja vitakavyotumika kwa mashindano hayo, wametoa maoni chanya kuhusu maeneo yote yatakayotumika katika mashindano hayo.

Si hivyo tu, bali hata Kamati ya Olimpiki ya Kimataifa (IOC) imeridhishwa na maandalizi hayo, na haina kipingamizi chochote cha kufanyika kwa mashindano hayo mwezi Februari mwaka ujao.

Lakini pamoja na hayo, baadhi ya watu wanaojiita ‘wanaharakati wa haki za binadamu’ wanachochea michezo hiyo kususiwa, wakiitaka IOC kuahirisha ama kuhamishia mashindano hayo sehemu nyingine. Watu hao wanaoipinga China, wanatumia kila fursa wanayopata kuichafua China, na safari hii, wamegeukia mashindano ya Olimpiki, kwa kupitia siasa za magharibi dhidi ya nchi hii ya Kikomunisti na kueleza wasiwasi wao kuhusu haki za binadamu. Wanaharakati hawa wanatumia kila mbinu wanayoweza kuibadili Michezo hii kuwa suala la kisiasa, na hivyo, wao wenyewe kuwa wakiukaji wa haki za binadamu.

Wanaharakati hao wanajaribu kutumia Mashindano hayo ya Olimpiki kuichafua China, lakini wameshindwa kuishawishi IOC, kwani kanuni ya Kamati hiyo inaweka wazi kuwa, mashindano ya Olimpiki ni mali pekee ya IOC, ambayo ina haki zote kuhusiana na masuala yote ya Michezo hiyo.

Kitu ambacho wanaharakati hao wanashindwa kuelewa ni kwamba, ni kweli Beijing ni mwenyeji wa mashindano hayo, lakini, mashindano ya Olimpiki ni jukwaa kwa wanamichezo kuwasiliana na kushindana, na China ina haki ya kuandaa tu, na wala sio kumiliki Mashindano ya Olimpiki ya Majira ya Baridi ya mwaka 2022, hivyo, kususia michezo hiyo ni kukiuka wazi kazi za IOC na moyo wa Olimpiki, na wanaoathirika zaidi ni wanariadha!

Wanarahakati hawa wanadai kuwa, vitendo ambavyo China inawafanyia watu wa Tibet, Xinjiang, na Hong Kong, vinahalalisha kususiwa kwa mashindano. Kwa mara nyingine tena, wanarudia uongo ule ule! Nchi za Magharibi, zikiongozwa na Marekani, mara nyingi zimekuwa zikieleza wasiwasi wao kuhusu ‘vitendo vibaya’ ambavyo serikali kuu ya China inawafanyia watu wa makabila madogo wa mikoa hiyo. Cha kushangaza zaidi, hakuna hata mara moja ambapo nchi hizo zimetoa ushahidi thabiti wa madai hayo, na kwa wale wanaoitwa mashuhuda wa vitendo hivyo, wanashindwa kuthibitisha taarifa zao!

Ukweli ni kwamba, licha ya tuhuma hizo za nchi za Magharibi, Tibet, Xinjiang, na Hong Kong zimeshuhudia ukuaji wa kasi chini ya serikali kuu ya China, na ustawi wa pamoja ndio njia ambayo China inatumia katika kulinda haki za binadamu.

Kwa wanaharakati hao, haki za binadamu ni chombo cha kutumia ili kutimiza matakwa yao, lakini sio kwamba wanajali na ni watetezi wa kweli wa haki hizo.

Michezo ni kitu kinachotumika kuunganisha watu wa jamii mbalimbali pamoja, kufurahi, kushindana, na kuleta watu wa tamaduni tofauti pamoja kwa lengo moja.

Badala ya kuchochea kuahirishwa ama kuhamishwa kwa kituo cha Mashindano ya Olimpiki ya Majira ya Baridi yatakayofanyika Beijing, jamii ya kimataifa inapaswa kuungana pamoja na kuhakikisha mashindano hayo yanafana na kuwa mlinzi halali wa haki za binadamu.

VCG111357598236.jpg
 
Bora wachochee hivyo hivyo nikikumbuka blacks walivyoteswa kipindi cha korona
 
Back
Top Bottom