Kusaidiana na mwenza wako ni muhimu!!!!!

Hapa ndipo pale ninaposemaga hakuna mke/mume asiye mwema ila ni mwema kwa nani?? Kwani anaweza asiwe mwema kwako lakini kuna mtu mwingine angeishi naye angekuwa mwema sana na kila siku angekuwa anamshukuru Mungu.


Kama hicho tu cha kupika, kumbeba mtoto mtu anaweza kuona ni kitu kibaya tena kibaya sana, huyu sio mume kwangu.

Hicho cha kuwaonea washikaji zako aibu wakati unanisaidia shughuli za nyumbani, wala hutaki wajue inamaana hawana hata cha kujifunza ktk hilo, huyo sio mume mwema kwangu.

Kama hayo mambo utafanya tu kwa sababu naumwa, yani ugonjwa tu, wala huna mapenzi ya kunisaidia hivo vishughuli tayari we sio mume kwangu. Basi nikitaka kusaidiwa siku hiyo najifanya kichwa kinauma nameza panado nalala.

Sikulazimishi wala sikuambii nisaidie. Lakini ndo ntakuwa naumia tu ndani kwa ndani.
 
Bado hubebi mtoto mgongoni unamwachia tu yeye mwenyewe.

Asante LD!!Uporoto swali la kuchagua kazi ndo tatizo!Kama unampenda kweli mwenzako sidhani kama vitu vidogo hivi vinaweza kua ishu!
 
Asante LD!!Uporoto swali la kuchagua kazi ndo tatizo!Kama unampenda kweli mwenzako sidhani kama vitu vidogo hivi vinaweza kua ishu!

Umeona ee!! Wala hatuitaji kufikiria na kuvijadili kama vile ni ishu kuubwaaa!!
 
Acheni ubrazameni wa kingemse kumsaidia wife kwa lolote lile hata kumfulia teitei kama amechoka au hajisikii vyema mi nafanya na kama mtaniita Bushoke kimpango wenu maana mi mwenyewe na yeye mbele ya madhabahu ndo tulitamkiana kwenye shida na raha.Sasa hapo mtoto kashakuja ajabu nini ukimpa tafu?Au ubaba ni suruali tu basi?Wahenga husema ukistaajabu ya Musa utaona ya Firauni basi kwa taarifa yenu mi hakuna kazi yeyote ya nyumbani anzia kupika,kumwogesha mwanangu,kufua za familia yangu nzima,kudeki,kuosha vyombo n.k ambayo siifanyi.Tunaamka saa kumi usiku na wife tunachapa mzigo mpaka saa moja Tunaishia kazini dogo tunamdrop school then jioni tunapitiana back to home na tena ye ndo ananidrive.Ndo malezi ya familia bora yenye upendo sio kuleta mfumo dume wa kiduwanzi hapa.Watoto watajifunza nini kutoka kwa libaba vivu au linalomsumbuasumbua mama yao kila kazi?Hayo mambo yalishapitwaga na wakati wakuu.
 
KIMICHIO ningekugongea Thanks sema niko Via M!Asante kwakutokua na akili mgando!
 
kimichio ningekugongea thanks sema niko via m!asante kwakutokua na akili mgando!
Ila ujue lizzy hii ndo sababu kubwa ya ndoa nyingi za siku hizi kutodumu.Wanaume tumekuwa na akili sijui za namna gani?Yaani eti ili uonekane dume la maana ukishaoa ukitoka tu kazini unatakiwa upitie nyumbani halafu ukishasalimia uhamie baa na marafiki mpate moja mbili mpaka chakula kiive home ndo urudishe tumbo zako ule wakati huohuo mkeo kashajichokea ka punda kalala zake na bado unamsumbua ukishashiba unataka mzigo.Hiyo ni roho ya ubinafsi na ni ukandamizaji wa kijinsia.Wanawake mko wapi kwa hili?
 
hapa ndipo pale ninaposemaga hakuna mke/mume asiye mwema ila ni mwema kwa nani?? Kwani anaweza asiwe mwema kwako lakini kuna mtu mwingine angeishi naye angekuwa mwema sana na kila siku angekuwa anamshukuru mungu.


Kama hicho tu cha kupika, kumbeba mtoto mtu anaweza kuona ni kitu kibaya tena kibaya sana, huyu sio mume kwangu.

Hicho cha kuwaonea washikaji zako aibu wakati unanisaidia shughuli za nyumbani, wala hutaki wajue inamaana hawana hata cha kujifunza ktk hilo, huyo sio mume mwema kwangu.

Kama hayo mambo utafanya tu kwa sababu naumwa, yani ugonjwa tu, wala huna mapenzi ya kunisaidia hivo vishughuli tayari we sio mume kwangu. Basi nikitaka kusaidiwa siku hiyo najifanya kichwa kinauma nameza panado nalala.

Sikulazimishi wala sikuambii nisaidie. Lakini ndo ntakuwa naumia tu ndani kwa ndani.
LD kwa maelezo yako nimekuelewa ila kazi bado tunayo mimi na wewe maana vijana wa kileo hii dhana imewakaa sana ila tukaze buti.
 
swala la kusaidiana na mwz wako ni zuri na linaongeza furaha na amani ktk nyumba yenu lakini mazingira ya kusaidiana yawe yale ambayo yanaendani na desturi zetu,sio mpaka unaosha vyombo huku mtoto mgongoni kulikoni??? mm kama mm huko si kusaidiana bali kubebeshwa mizigo na ni aibu kwa mwanaume ukifikia hapo hata kama umeoa mzungu

Tusaidiane lakini nafasi ya mwanaume ibakie palepale mfano mama anaosha vyombo ww unaweka mkaa store au unatoa viti kwa maandalizi ya kupika au kufuata dukani
 
Bado hubebi mtoto mgongoni unamwachia tu yeye mwenyewe.

Asante LD!!Uporoto swali la kuchagua kazi ndo tatizo!Kama unampenda kweli mwenzako sidhani kama vitu vidogo hivi vinaweza kua ishu!

Kubeba`mtoto mgongoni au kuosha vyombo/nguo mtanisamehe kinadada,naweza cheza na mtoto kumuogesha/kumlaza lakini mgongoni HAPANA!
 
Tusisahau wengine hufanya shughuli fulani ziziotarajiwa na jamii kwa sababu ya limbwata.
 
Kubeba`mtoto mgongoni au kuosha vyombo/nguo mtanisamehe kinadada,naweza cheza na mtoto kumuogesha/kumlaza lakini mgongoni HAPANA!

Hahahahahahahahaha kama nakuona umebeba mtoto mgongoni
 
LD kwa maelezo yako nimekuelewa ila kazi bado tunayo mimi na wewe maana vijana wa kileo hii dhana imewakaa sana ila tukaze buti.

Kimichio umeshaoa, maana naona machemistry yanaendana hapa!!
 
Tusisahau wengine hufanya shughuli fulani ziziotarajiwa na jamii kwa sababu ya limbwata.

Penye limbwata, hakuna mapenzi ya kweli, ni mapenzi ya nguvu za giza ambayo huwa hayadumu hata kidogo.

Usisubiri uwekewe limbwata, do it from your heart!!

Sasa ukiwa mbishi ndo hapooooooo.
 
Ila ujue lizzy hii ndo sababu kubwa ya ndoa nyingi za siku hizi kutodumu.Wanaume tumekuwa na akili sijui za namna gani?Yaani eti ili uonekane dume la maana ukishaoa ukitoka tu kazini unatakiwa upitie nyumbani halafu ukishasalimia uhamie baa na marafiki mpate moja mbili mpaka chakula kiive home ndo urudishe tumbo zako ule wakati huohuo mkeo kashajichokea ka punda kalala zake na bado unamsumbua ukishashiba unataka mzigo.Hiyo ni roho ya ubinafsi na ni ukandamizaji wa kijinsia.Wanawake mko wapi kwa hili?

https://www.jamiiforums.com/post_thanks.php?do=post_thanks_remove_user&p=1531688
The Following User Says Thank You to KIMICHIO For This Useful Post:

Lizzy (Today)​
 
Atiiii kama unaweza mtu mwenye 50kg washindwa nn katoto kako kenye 10kg tu. Acha bana!!
Kila mtu ana sehemu kachora mstari kwamba hapa mi hapana sasa mimi mstari wangu huo sivuki hapo najuwa nikikubali hilo linafata 'leo natoka na rafiki zangu usiku kaa na mtoto'.
 
Back
Top Bottom