Kurugenzi ya Mawasiliano CHADEMA iamke

TinyMonster

JF-Expert Member
Jun 15, 2009
248
154
Nimeona nilisemelee hili mapema kabla kampeni hazijaanza, kiukweli kurugenzi ya mawasiliano CHADEMA imepwaya sana suala la organization ya huu mkutano mkuu. Mtu anaweza kuwaza kuwa uhaba wa vyombo vya habari kwenye Mkutano ni kwa sababu vyombo vya habari vina uoga lakini ukweli ni kwamba newsroom nyingi hazikuwa na taarifa za uhakika kuhusu kama kitakuwa kikao cha ndani au wataruhusiwa kurusha live matokeo yake wengi wakaishia kutuma mwandishi na cameraman mmoja badala ya crew ya live.

Kitu kingine katika zama hizi ambazo vitu vingi vinaenda kupitia YouTube ilitakiwa CHADEMA Digital wawe na live link moja ambayo wangesambaza kwa waandishi wote ili ambaye anataka kupeleka hewani anafanya kuichukua, kwa hili ACT Wazalendo walilifanya siku wanamtambulisha Membe na matokeo yake walipata visibility kubwa mno na ninaamini hata Jumatano kwenye Mkutano Mkuu wao watafanya hivi hivi, Tumaini Makene na wenzako mnaweza kujifunza hiki kitu.

Ushauri wangu ni kwamba idara iamke iwe aggressive kwenye kusukuma brand ya CHADEMA na kutoa ushirikiano kwa waandishi wa habari, tuache kufanya vitu kwa mazoea kwa sababu wakati sisi tunatembea wenzetu wanakimbia. Na muhimu zaidi tafuteni vijana ambao ni tech savy wanaojua kufanya graphic designing na video editing wakae ofisini kipindi chote kizima cha uchaguzi wasaidie kwenye social media.
 
Uwaambie pia sio kila asiyeiunga mkono CDM anabanwa na dola au anajikomba.

Waelewe itikadi zinazofautiana. Wengine wanajiuliza hivi hawa CDM ndiyo chama gani.

Kama wao wajiulizavyo kwa CCM. Demokrasia ni kukubali pia kuna mwenzako yupo tofauti na wewe. Na kutofautiana ndiyo demokrasia yenyewe.
 
Hawana hela wasisingizie vyombo vya habari eti.vinaogopa ,viogope nini wakati ni tukio halali?,ni wapi sheria ilikuwa inavunjwa?,hawana hela wawe wawazi tu
 
Hawana hela wasisingizie vyombo vya habari eti.vinaogopa ,viogope nini wakati ni tukio halali?,ni wapi sheria ilikuwa inavunjwa?,hawana hela wawe wawazi tu

Kwani shilingi ngapi hata useme hawana pesa? Naona kama vile hujui ulijualo...

Tatizo lako ni kuwa unazikia masikioni serikali zinazoongozwa na madikteta. Hujui jinsi zinavyo operate. Ungeuliza, ungeambiwa...

Hatuhitaji kuponza vyombo vya habari vya watu kufungiwa na kisha ndugu zetu wakapoteza ajira zao bure....

Tunaposema, nchi inahitaji ukombozi wa pili toka kwa mkoloni mweusi, muwe mnaelewa....
 
Hawana hela wasisingizie vyombo vya habari eti.vinaogopa ,viogope nini wakati ni tukio halali?,ni wapi sheria ilikuwa inavunjwa?,hawana hela wawe wawazi tu

Jiwe ana wivu wa kisiasa, yeye ndio anatumia madaraka yake kutisha vyombo vya habari visiwatangaze cdm.
 
Nimeona nilisemelee hili mapema kabla kampeni hazijaanza, kiukweli kurugenzi ya mawasiliano CHADEMA imepwaya sana suala la organization ya huu mkutano mkuu. Mtu anaweza kuwaza kuwa uhaba wa vyombo vya habari kwenye Mkutano ni kwa sababu vyombo vya habari vina uoga lakini ukweli ni kwamba newsroom nyingi hazikuwa na taarifa za uhakika kuhusu kama kitakuwa kikao cha ndani au wataruhusiwa kurusha live matokeo yake wengi wakaishia kutuma mwandishi na cameraman mmoja badala ya crew ya live.

Kitu kingine katika zama hizi ambazo vitu vingi vinaenda kupitia YouTube ilitakiwa CHADEMA Digital wawe na live link moja ambayo wangesambaza kwa waandishi wote ili ambaye anataka kupeleka hewani anafanya kuichukua, kwa hili ACT Wazalendo walilifanya siku wanamtambulisha Membe na matokeo yake walipata visibility kubwa mno na ninaamini hata Jumatano kwenye Mkutano Mkuu wao watafanya hivi hivi, Tumaini Makene na wenzako mnaweza kujifunza hiki kitu.

Ushauri wangu ni kwamba idara iamke iwe aggressive kwenye kusukuma brand ya CHADEMA na kutoa ushirikiano kwa waandishi wa habari, tuache kufanya vitu kwa mazoea kwa sababu wakati sisi tunatembea wenzetu wanakimbia. Na muhimu zaidi tafuteni vijana ambao ni tech savy wanaojua kufanya graphic designing na video editing wakae ofisini kipindi chote kizima cha uchaguzi wasaidie kwenye social media.
Wamechukua tahadhari ya kuumizwa wameumizwa vyakutosha
 
Bora umelisema hilo, kitengo cha habari kimechoka hilo halina mjadala.
Hata Ile siku Tundu Lissu anakuja coverage ilikuwa poor Sana, wananchi wengi walitaka kuona Ila hawakupata online

Wasiwategemee akina Millard Ayo na Global Tv

Hawa jamaa Wana resources nyingi kuliko ACT Ila wamepigwa bao na ACT hapa,
 
UKWELI NI KWAMBA BAADA YA RAISI KUANZA KUWATEUA WAANDISHI WA HABARI, SASA HIVI KILA MWANDISHI ANATAKA KUTEULIWA. HIVYO USITEGEMEE HABARI ZA UPINZANI KUPEWA KIPAUMBELE HASWA ZAIDI CHADEMA NDIO SABABU WALIFUNGIA MPAKA GAZETI LA TANZANIA DAIMA WAKATI MAGAZETI YA TANZANITE NA UHURU YANAYOSIFIA UTAWALA BADO YAPO SOKONI MIAKA YOTE
 
Hawana hela wasisingizie vyombo vya habari eti.vinaogopa ,viogope nini wakati ni tukio halali?,ni wapi sheria ilikuwa inavunjwa?,hawana hela wawe wawazi tu
Issue sio hela. Issue ni maagizo kutoka juu..
Hivi ni mara ngapi mabalozi huenda Ikulu kujitambulisha kimya kimya?
Jiulize what was so special juzi balozi wa Marekani awe live kwenye vyombo vya habari? Kisa Chadema wasiwe covered?? Ati na jukwaa sujui la kina nani nalo live na Baba la Baba apige simu iwe live. Kuzuia Chadema na ACT wasionekane. Siasa za kizamani kabisa..
 
Issue sio hela. Issue ni maagizo kutoka juu..
Hivi ni mara ngapi mabalozi huenda Ikulu kujitambulisha kimya kimya?
Jiulize what was so special juzi balozi wa Marekani awe live kwenye vyombo vya habari? Kisa Chadema wasiwe covered?? Ati na jukwaa sujui la kina nani nalo live na Baba la Baba apige simu iwe live. Kuzuia Chadema na ACT wasionekane. Siasa za kizamani kabisa..
Hii ya wanawake nilikua siijui ila nilishangaa kuikuta live badala ya issue ya chadema ilinishangaza mno na baada ya hapo vyombo vya habari vikaanza kuikuza zaid rais alipopiga simu ila yote kwa yote habari ya chadema ikabaki juu kileleni
 
Hii ya wanawake nilikua siijui ila nilishangaa kuikuta live badala ya issue ya chadema ilinishangaza mno na baada ya hapo vyombo vya habari vikaanza kuikuza zaid rais alipopiga simu ila yote kwa yote habari ya chadema ikabaki juu kileleni
Wana mkakati wa Ccm ni low minded. Hawakujua kwamba Chadema wata rusha matangazo yao kupitia BBC na DW ambao wako mitndaoni.. Tbc mpaka utafute ilipoTv kama ilivyo kwa Channel 10
 
Back
Top Bottom