mwandiga
JF-Expert Member
- Dec 5, 2011
- 1,506
- 661
Hii tabia ya kukubali hoja bungeni kwa kusema ndio kwa wanaokubali na hapana kwa wanaokataa na kisha spika kufanya maamuzi kwa kile alichosikia ni ujinga na kuwadanganya watanzania. Hivi kwa nini wasitumie mfumo wa kompyuta ambapo kila mbunge atabonyeza kitufe mezani kwake cha ndio au hapana kisha kwenye screen itakayokuwa hapo pembeni ya spika inaonesha ndio ni ngapi na hapana ni ngapi in figures. Mimi naona hilo halitushindi ila ni kwa ajili ya maslahi ndio maana halikufanywa. Muda umefika sasa wa kuanza kutumia hivi vitu