Kura ya Meghji yazua utata mpya

Kura ya Meghji yazua utata mpya

Mkuu huyu mama ni mjumbe toka Wabunge wa Muungano kama sikosei na si kundi la 201

BACK TANGANYIKA

Hapana kiongozi, Mh. Meghji ni miongoni wa Wabunge wateule wa Rais kundi la Mh. Mbatia. Hili linaongeza utata na ndio Katibu wa Bunge anapaparika kutetea yasiyofaa badala ya kumwachia Sitta, Sululu na Werema.

Ukichunguza kwa undani utaona utata na mkanganyiko mkubwa sana, na ambao kila upande ukitoa utetezi unaweza kukubalika. Ndiposa tunona Tume ya Warioba ilikuwa sahihi kuja na wazo la Serikali tatu, lkn CCM kwa kufaidika na mikanganyiko hii inafaidika saba.

Hata hivyo, ukweli ulio wazi ni kuwa Meghji hakutakiwa kupiga kura upande wa Zanzibar maana hajawahi hata siku moja kuwakilisha Zanzibar na hata uteuzi wake haujuzingatia asili yake bali ni coincidence ambayo BMK wameitumia wakidhani Watanzania bado tunaweza kumezeshwa chochote na tukakubali.

Vv
 
hii tu inadhihirisha umuhimu wa serilali3, ijulikane yupi anasimamia wapi na sio kuwa popo...
 
Huyu mama alishazoe kujilipua, kumbukeni wakati wa EPA yeye ndiyo alikubali kujifunga mabomu hadi pesa zikakwapuliwa pale BOT, leo teeeeeena uchakachuaji wa Katiba.Ukisikia kina mama wa bongo basi ni huyu mama
 
Huyo katibu wa Bunge ana hoja dhaifu sana na anaonekana mzito kujieleza.

Hivi Hamad Rashid si Mbunge wa Wawi iliyopo Zanzibar? Sasa si lazima angepiga kura kwa Upande wa Zanzibar maana sheria inataka pande mbili za muungano na yeye amekua mjumbe kwa tiketi ya Kuwa Mbunge wa Wawi ya Kule Zanzibar


Huu ni Upuuzi

Hawezi kuwa na hoja
 
Licha ya kuangalia alizaliwa wapi, jambo muhimu la kuzingatiwa hapa ni kwamba alikuwa kwenye bubge la taifa kwa kigezo kipi. Je alikuwa kwenye bunge la katiba kama mwakilishi wa Tanganyika, Zanzibar, au kundi ka waganga wa kienyeji?
 
Kakke huyo mama ni mzanzibar wa kuzaliwa kama ilivyo kwa wazanzibar wote kuwa wana haki zote za utanzania hivyo anaweza kushika cheo chochote tanzania maana ni mtanzania.

ila kwa mtu wa bara kuwa mznz lazima awe kaishi muda usiozidi 10yrs zanzibar .hapo hakuna utata. sasa huyo mama unasemaje sio mzanzibar kwa vile ameamua kuhamia dar ndio asiwe mznz,wewe uliyehamia huko UK tukuite sio mznz?
au kuna mahali popote kaelezwa kuwa yeye anawakilisha jimbo fulani bara?
hizi hoja za kitoto ndio ccm huwapiga nazo mnabaki mmeduwaa.


AWOTTA: Member: Zakia Hamdani Meghji

Sasa uteuzi wake umezingatia kigezo kipi kati ya Utanzania au Uzanzibari? Maana kuna asili mbili za kiraia katika JMT; je, Meghji amejiandika kupiga kura upande gani wa Muungano?

Kwa hiyo ili angalau tupate kuridhika maswali haya matatu yajibiwe:
1.Uteuzi wake kama Mbunge, ni kutikea upande gani wa Muungano?
2. Je, anacho kitambulisho cha ukazi wa Zanzibar?
3. Je, wakati wa Uchaguzi Mkuu, alipiga kura upande gani wa Muungano?

Vv
 
Last edited by a moderator:
Kakke huyo mama ni mzanzibar wa kuzaliwa kama ilivyo kwa wazanzibar wote kuwa wana haki zote za utanzania hivyo anaweza kushika cheo chochote tanzania maana ni mtanzania.

ila kwa mtu wa bara kuwa mznz lazima awe kaishi muda usiozidi 10yrs zanzibar .hapo hakuna utata. sasa huyo mama unasemaje sio mzanzibar kwa vile ameamua kuhamia dar ndio asiwe mznz,wewe uliyehamia huko UK tukuite sio mznz?
au kuna mahali popote kaelezwa kuwa yeye anawakilisha jimbo fulani bara?
hizi hoja za kitoto ndio ccm huwapiga nazo mnabaki mmeduwaa.


AWOTTA: Member: Zakia Hamdani Meghji
ingawa mm si shabiki wa ccm lakini ukilifuatilia kiundani ccm wameshinda ni wap anatakiwa apigie kura huyu mama huwezi kumbagua sijui mzanzibar au kakaa sana bara hapo tumepigwa bao yaelekea walimuweka wa akiba alikuwa anapasha misuli nje panapopwaya wanamuongezea.
 
yule kateuliwa na rais kupewa ubunge sio yeye wako pia akina sada mkuya, Nahodha na wengine sasa wote hao utasema sio waznz ,au kuishi bara ndio kupoteza uznz? sasa nyie mliokimbilia england nanyi mtakuwa sio waznz?

Unatudanganya, Hamadi Rashidi ni Mbunge wa Jimbo la Wawi, Pemba.

Vv
 
Huyu Zakia ni mzanzibar kwasababu nakumbuka mimi kuna kipindi huyu bibi alikuwa waziri alikuwa anapenda kuja pale kwa kakake anaitwa Hamdani alikuwa anaishi pale msikiti mabati mtaa wa Kisiwandui znz.
 
Hapana kiongozi, Mh. Meghji ni miongoni wa Wabunge wateule wa Rais kundi la Mh. Mbatia. Hili linaongeza utata na ndio Katibu wa Bunge anapaparika kutetea yasiyofaa badala ya kumwachia Sitta, Sululu na Werema.

Ukichunguza kwa undani utaona utata na mkanganyiko mkubwa sana, na ambao kila upande ukitoa utetezi unaweza kukubalika. Ndiposa tunona Tume ya Warioba ilikuwa sahihi kuja na wazo la Serikali tatu, lkn CCM kwa kufaidika na mikanganyiko hii inafaidika saba.

Hata hivyo, ukweli ulio wazi ni kuwa Meghji hakutakiwa kupiga kura upande wa Zanzibar maana hajawahi hata siku moja kuwakilisha Zanzibar na hata uteuzi wake haujuzingatia asili yake bali ni coincidence ambayo BMK wameitumia wakidhani Watanzania bado tunaweza kumezeshwa chochote na tukakubali.

Vv

Mkuu Vyamavingi, Mimi na wewe tunahoja moja sema tu ktk kuzibainisha ndipo penye tofauti...

Huyu mama pamoja na kwamba ni mteule wa Rais toka kundi la Mbatia kama unavyodai, Aliteuliwa na Rais kuwa Mbunge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwamba aliteuliwa kuwa Mbunge toka jimbo au Upande gani wa Muungano hili ndilo hatujui kwani Rais hakubainisha haya wakati wa uteuzi wake/Wao

Na kuteuliwa kwake na Rais hakumuondolei haki ya kuwa Mbunge. Hivyo kusema kwamba huyu ni Mbunge wa Muungano ni sahihi kabisa

BACK TANGANYIKA
 
Huyo katibu wa Bunge ana hoja dhaifu sana na anaonekana mzito kujieleza.

Hivi Hamad Rashid si Mbunge wa Wawi iliyopo Zanzibar? Sasa si lazima angepiga kura kwa Upande wa Zanzibar maana sheria inataka pande mbili za muungano na yeye amekua mjumbe kwa tiketi ya Kuwa Mbunge wa Wawi ya Kule Zanzibar


Huu ni Upuuzi

Mbatia Naye wa CCM au UKAWA
 
ulaghai ni kitu kibaya sana... huyu mama for so many times amekua kwenye wrong side of history

Hajui haya madhuluma huwa yanabaki kwenye vizazi vyake

apunguze tu adhabu kwa wanaye na wajukuu kwa kuacha ulaghai
 
Huyu Zakia ni mzanzibar kwasababu nakumbuka mimi kuna kipindi huyu bibi alikuwa waziri alikuwa anapenda kuja pale kwa kakake anaitwa Hamdani alikuwa anaishi pale msikiti mabati mtaa wa Kisiwandui znz.

Ndiyo kuzaliwa ZnZ haina ubishi. Wana-jf wanauliza, je anacho kitambulisho cha Mzanzibari? Je, uchaguzi mkuu uliopita alijiandikisha kupiga kura kama Mzanzibari au Mtanganyika. Pia ni lini Mzanzibari akawa mkuu wa wilaya au mkoa wa Tanganyika?
Akina mzee Warioba walipokuja na formula ya S3 maghambas yakapinga - ili yaendelee kuwa yanatuzuga. Huu si ndio uraia-pacha wanaoukataa?
 
yaani ndugu unaongea kama vile umepagawa au hujitambui. huyu ni mbunge wa kuteuliwa na rais kama alivyo sada mkuya.

Kama ambavyo ni Bahati mbaya kwa taifa hili kuwa na Kiongozi tuliyenaye mpaka sasa Madarakani......

Vilevile ni bahati mbaya kwa Mtandao kama wa Jamiiforums kuwa na mwanachama kama wewe, Ni aibu iliyoje!!!!

Hebu soma tena post uliyoni-quote then oanisha na hiki ulichomiandika,Je ni nani kati yangu mimi na wewe abaye hajitambui!!!!?

Rudia tena kusoma

BACK TANGANYIKA
 
....hapa shida ni nini?,meghji anotoka 201,je jina lake linatoka upande gani wa Tanganyika au Zanzabar,angalieni aliomba kupitia taasisi gani?.Atakamatika tu.....ikija kungundulika kama kamafanya hivyo..duh huyu mkwe atadharaulika na pengine akajipatia maadui wabaya sana.

Meghj aliingia kwenye bunge la katiba kama mjumbe wa bunge la jamuhuri ya muungano wala sio kundi la 201.
 
ccm mm sina hamu nao kabisa kama waliweza kumwasha marehemu akapiga kura ya NDIYO basi hakuna wanachoshindwa kufanya huyu mama hana kosa anafuata maelekezo aliyemteua ukomo wa ccm umeshakaribia kila siku wanazidi kuumbuka na bado
 
Ndiyo kuzaliwa ZnZ haina ubishi. Wana-jf wanauliza, je anacho kitambulisho cha Mzanzibari? Je, uchaguzi mkuu uliopita alijiandikisha kupiga kura kama Mzanzibari au Mtanganyika. Pia ni lini Mzanzibari akawa mkuu wa wilaya au mkoa wa Tanganyika?
Akina mzee Warioba walipokuja na formula ya S3 maghambas yakapinga - ili yaendelee kuwa yanatuzuga. Huu si ndio uraia-pacha wanaoukataa?
umenena mkuu hapo sina majibu ya kina kuhusu hoja hizo.
 
Back
Top Bottom