Kura ya maoni: Zitto vs Dr Slaa

Kura ya maoni: Zitto vs Dr Slaa

Ni nani ungependa agombee urais mwaka 2015 kwa tiketi ya CHADEMA?

  • Zitto Z. Kabwe

    Votes: 180 15.3%
  • Wilbrod P. Slaa

    Votes: 996 84.7%

  • Total voters
    1,176
  • Poll closed .
Status
Not open for further replies.
Dr. P.W. Slaa na Mr. Zito Z. Kabwe ni wanasiasa mashuhuri hapa nchini.

Pamoja na kuwa Zito ana kasoro zake nyingi tu, bado ni kijana anayeuzika sana kwenye siasa za Tanzania. Ameshajijenga vizuri sana. Kuna siku alimbeza mwenzake Tundu Lissu bungeni, nikaona kuwa huyu jamaa kumbe kweli anatakiwa aekue kidogo. Sometimes busara zinaongezeka kulingana na muda.

Kama Zito kabwe atampisha Dr. W.P. Slaa agombee uraisi uchaguzi wa mwaka 2015 na kumfanyia kampeni ya dhati, CHADEMA itafanya vizuri sana kwenye uchaguzi. Lakini kukiwa na kutofautiana kati ya Zito na Slaa, basi CHADEMA inaweza ikakosa mafanikio kwenye uchaguzi wa mwaka 2015. Matokeo ya mwaka 2015 yatachangia sana matokeo ya uchaguzi wa mwaka 2020.

Napendekeza, Dr. Slaa aachiwe agombee mwaka 2015 na baada ya hapo akiwa raisi aongoze kwa miaka mitano tu, amuachie Zito, akikosa astaafu siasa, ataheshimika sana kisiasa hapa Tanzania kuliko wale ambao wanasema wamestaafu alafu baada ya muda mfupi wanarudi. Zito pia anatakiwa amrudishe David Kafulila CHADEMA ili washirikiane kuhakikisha Kigoma inakuwa ngome muhimu ya CHADEMA.

Mkuu mwaka 2020 Dr Slaa atakuwa na miaka 95.
 
Mkuu, mawazo yako mazuri na umeona mbali ingawa katika CHADEMA muda wa kupendekeza wagombea bado.

Sasa hivi ni muda wa kujenga chama na si wa kujenga watu na makundi ya kuwania urais
 
Ebo.....
Kumbe kuna watanzania wawili tu wanaofaa kugombea!!!!????
 
Dr. P.W. Slaa na Mr. Zito Z. Kabwe ni wanasiasa mashuhuri hapa nchini.

Pamoja na kuwa Zito ana kasoro zake nyingi tu, bado ni kijana anayeuzika sana kwenye siasa za Tanzania. Ameshajijenga vizuri sana. Kuna siku alimbeza mwenzake Tundu Lissu bungeni, nikaona kuwa huyu jamaa kumbe kweli anatakiwa aekue kidogo. Sometimes busara zinaongezeka kulingana na muda.

Kama Zito kabwe atampisha Dr. W.P. Slaa agombee uraisi uchaguzi wa mwaka 2015 na kumfanyia kampeni ya dhati, CHADEMA itafanya vizuri sana kwenye uchaguzi. Lakini kukiwa na kutofautiana kati ya Zito na Slaa, basi CHADEMA inaweza ikakosa mafanikio kwenye uchaguzi wa mwaka 2015. Matokeo ya mwaka 2015 yatachangia sana matokeo ya uchaguzi wa mwaka 2020.

Napendekeza, Dr. Slaa aachiwe agombee mwaka 2015 na baada ya hapo akiwa raisi aongoze kwa miaka mitano tu, amuachie Zito, akikosa astaafu siasa, ataheshimika sana kisiasa hapa Tanzania kuliko wale ambao wanasema wamestaafu alafu baada ya muda mfupi wanarudi. Zito pia anatakiwa amrudishe David Kafulila CHADEMA ili washirikiane kuhakikisha Kigoma inakuwa ngome muhimu ya CHADEMA.

Slaa akiwa rais sidhani kama atakubali kuongoza miaka 5 tu! ninavyo mjua na anavyopenda Uongozi huenda akataka kubadili hata na katiba ili aendelee kukaa madarakani! haya tumeyaona huko Senegal pale Wade alipotaka kubadilisha katiba na hata Zambia mpinzani Chiluba alipoukwaa Urais nae alitaka kubadili katiba!
 
Mkuu kwa nini tusijikite kwenye kuwashauri viongozi jinsi ya kukijenga chama kuliko kufikiria nani agombee na nani anafaa?
 
Nilichojifunza ni kwamba dr.slaa anaogopeka sana kwa mafisadi.kila siku mara kibabu mara hana mke .lakini yote tisa sasa ameamua kujikita kutoa elimu ya uraia BUREEEEEEEEEEEEEEEEEE Kwa watanzania ili 2015 kila mtanzania awe na ufahamu wa kutosha kitakachobaki ni KUTIA KITU KATIKA SANDUKU LA KURA.Nina matumaini na dr.slaa atakuwa SATA wa tanzania
 
Slaa akiwa rais sidhani kama atakubali kuongoza miaka 5 tu! ninavyo mjua na anavyopenda Uongozi huenda akataka kubadili hata na katiba ili aendelee kukaa madarakani! haya tumeyaona huko Senegal pale Wade alipotaka kubadilisha katiba na hata Zambia mpinzani Chiluba alipoukwaa Urais nae alitaka kubadili katiba!

Mkuu haya ni mawazo yako tu, dr Slaa hajawahi kusaka uras. Ni wanachama wa Chadema wanaomtaka awe rais
 
zitto atapata kura nyingi akigombea urais kuliko slaa,Slaa ni mzee kwa sasa.

Mkuu, mzee kwenye siasa maana yake ni mini? hebu tuchambulie Na jaribu kulinganisha na watu kama kina Mandela waliotawala wakiwa na umri mkubwa pia na watu waliotawala na umri mdogo kama kina Kabila jnr
 
Muda huu ni wakujenga chama,angalia jimbo la KWIMBA lipo waazi kabisa mansoor alishaamia dar,kwanini isiende timu hata ya wabunge tu wakaamshe amshe hilo jimbo na kuweka uongozi wa kueleweka mapema kabla 2015,angalia hata jimbo la Magu.mi nashaa akina wenje kwanini wasifanye hiyo kazi ya kuzungukia majimbo ya jirani
 
Ujana wake nayo ni sifa? kwani ukiwa mzee huwezi kuwa rais?
sababu za kuto mchagua Zitto Kabwe
1. hana sifa ya kugombea urais coz hajatimiza umri unaotakiwa na sheria
2. hana sifa ya kugombea coz ana uchu wa madaraka
3. hana sifa ya kugombea urais coz hana Busara na hekima
4. hana sifa ya kugombea coz anatumiwa na ccm

Yaani majibu ya hapo juu ni KWELI TUPU NA NINASEMA MUNGU NDIYE AMJUAYE KIJANA HUYU JINSI ALIVYO NYOKA MKUBAWA KWENYE CHAMA CHA CHADEMA. NINAKUBALI DR. SLAA ANA MAPUNGUFU YAKE KWENYE NDOA LAKINI KIKAZI NI MZURI NA ANAFAA KULIKO ZITO KABWE. NINAUNGA MKONO HOJA NA SABABU ZOTE ZILIZOTOLEWA HAPO JUU KWA NINI ZITTO KABWE HAFAI.
ASANTE SANA MTOA SABABU
 
Mi nafikiri Zito ni bora na yeye apewe nafasi ili tumpe kura. Zito ni chaguo la watanzania.
 
On my side, w. slaa kwasababu (1)anakubalika (2)sera bora zenyemvuto wa kuleta mabadiliko (3)mtetezi wa haki za wanyonge wa wa2 wa kipato cha chini (4)mtetezi wa wala laslmali za taifa [mafisadi]
 
Hivi ile kura ya maoni kati ya Dr. Slaa na Lowasa ilikwenda wapi mbona ilifutwa mapema sana na hatujaona matokeo yake?
 
Tuache kelele nyingi, kama ungepewa mamlaka ya kumteua kati ya Zitto Zuberi Kabwe ama Wilbroad Peter Slaa kugombea nafasi ya urais mwaka 2015. Ni nani ungemteua? Na Kwa Nini? Toa sababu kuu nne TU.

Hizi taarifa za kura unazifanyia nini????
Tukishajua kuwa ni Zitto au ni Dr Slaa, ndio mtawaita muwaambie juu ya hizi kura zilizopigwa??
 
Yaani poll tu inasema 15% na Dr. 84% (whole figures) halafu linabwabwaja linataka urais. Kwisha na masalia wako. Hufiki kokote Zitto!! Unakiliwaza na kupoteza muda wako. Mwisho wako kisiasa ni 2015 na baada ya hapo rudi kwa wanaokutumia!! They will dump you maana wanaokutumia leo watakuwa hawapo tena. You are done!!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom