Kura moja ya Lindi ina uzito mara tano ya Dar. Nani ameamua?

Mwanamkiwi

JF-Expert Member
Mar 7, 2019
2,023
2,399
Kura moja ya raia wa Lindi inabeba uzito kisiasa mara tano kuliko raia wa Dar es Salaam. Kwa nini?
Angalia namba (nazitumia za 2016 na 2010, 2020 sijaona lakini kimsingi ni vile):
Dar es Salaam wakazi 5,465,420 (2016), majimbo ya bunge 10, maana raia 546,000 = mbunge 1
Lindi
wakazi 897,533 (2016), majimbo ya bunge 8, maana raia 112,000 = mbunge 1
Wastani
kitaifa:
Tanzania bara wakazi 48,676,698 (2016), majimbo ya bunge 214, maana raia 227,000 = mbunge 1

Katika takwimu ya 2016 mikoa iliyohitaji kura nyingi kumpata mbunge 1 ilikuwa: Dar es Salaam, Mwanza, Kagera na Kigoma. Ilikuwa na wakazi milioni 13.7, waliweza kuchagua wabunge 36. Kama wastani wa kitaifa ungefuatwa, wangepata wabunge 60.
Mikoa iliyohitaji kura chache kwa wabunge wao ilikuwa: Iringa, Mtwara, Pwani, Katavi, Njombe na Lindi.
Ilikuwa na wakazi milioni 5.78, waliweza kuchagua wabunge 45.
Kama wastani wa kitaifa ungefuatwa, wangepata wabunge 25.

Kwenye mikoa mingine tofauti kati ya wastani na idadi halisi ya wabunge ilikuwa 1-1 tu.
Ninaiona leo tu. Je imewahi kujadiliwa?

(Chanzo: https://www.nbs.go.tz/nbs/takwimu/majimbo/MAJIMBOApril_Kisw.pdf)
 
... ondoa viti maalumu; kila wilaya iwe pia jimbo la uchaguzi na iwakilishwe na wabunge wawili wa kuchaguliwa mwanaume na mwanamke. That's it!
 
Mkuu, naona unaliamusha dude ili kanda ya ziwa na magharibi wadai majimbo zaidi ya uchaguzi kulingana na population density yao!
 
... ondoa viti maalumu; kila wilaya iwe pia jimbo la uchaguzi na iwakilishwe na wabunge wawili wa kuchaguliwa mwanaume na mwanamke. That's it!
Lako ni pendekezo lingine; lakini vita maalum kwa sasa havibadilishi takwimu, maana vyama vinateua orodha ya viti maalum, haviamui kufuatana na jiografia.
 
Ndomaana kuna haja ya kua na two houses house of representative ambayo inaendana na idada ya watu na house of senate anae endana na geographical area.......kwa bunge moja sio fair katika democracy
Sisi tunataka tupunguze wapiga mboyoyo na makofi wewe unataka waongezeke ?

Wanamsaada gani kwa wananchi!! Kupitisha sheria mbovu?
 
... kupiga hatua kama taifa sio lelemama Mkuu. Lazima wengine waumie. Kwingine huko walimwaga damu sembuse kupoteza jimbo!
Ukitaka kukaribia usawa wa kura za wananchi, bila kufuta wabunge Lindi, basi ungeweza kutumia wastani wao wa wakazi 112,000 kila mbunge.
Ingeleta bunge la wabunge wa majimbo 430 hivi; Dar es Salaam ingepata wabunge 50 (badala ya 10), ili Lindi ibaki na hao 8.
(swali la viti maalumu halimo)
 
Mkuu, naona unaliamusha dude ili kanda ya ziwa na magharibi wadai majimbo zaidi ya uchaguzi kulingana na population density yao!
Kweli, lakini changamoto kubwa ni Dar es Salaam. Wanahitaji zaidi ya nusu milioni ili wampate mbunge. Linganisha ni mikoa isiyohitaji lakhi mbili.

Kuna nchi ambako mahakama ziliingia kati, maana mahali pengi "usawa mbele ya sheria" ni kanuni ya kimsingi.
 
... ondoa viti maalumu; kila wilaya iwe pia jimbo la uchaguzi na iwakilishwe na wabunge wawili wa kuchaguliwa mwanaume na mwanamke. That's it!
Um hii hapana matumizi mabaya ya Fedha. Fair competition tu inatosha..!
 
Back
Top Bottom