Kupanda gari za magazeti,nimekoma

Kupanda gari za magazeti,nimekoma

Unataka kuhadithiwa mtu alivyokufa?Ajabu
No, sio hivyo. Umeeleza lakini sio kiundani.


Alikuwa dereva au abiria?
Au aligongwa na hizo gari.?!


Hicho ndio nilicho maanisha.
 
Mkuu huo ni unafiki we mwenyewe hukupanda bus ukaona upande gari la magazeti ili uwahi ishu yako umesolve basi ushaanza kuomba wakamatwe. Dah kweli wema mtendee MBUZI utakunywa hata Mchuzi

Au mbwa atakulinda
 
Dereva aliona akikwambia sipakii abiria basi ungelalama wee mpaka kumsababishia mkosi, hivyo akatumia mbinu ya 'action speak louder than words' ili next time ukiona gari la magazeti unageuka upande wa pili lisije likasimama kukwambia 'twende'

Ata akisoma hili andiko lako sasa atasema 'meseji sent' huku anacheeeka.
 
Kaka hiyo Gari nilipanda aisee toka Makambako kuja Dar..nakumbuka Dereva alikuwa anazungumza na wenzake kwamba anataka kuwahi kuchek gem ya UEFA Dar..makambako tulitoka saa 7..ila tuliwa mech mapema sana...

Kikubwa sio kulaumu kwanza hao jamaa ni special case hawasimamishwi na Traffic..

Nimeskia hutafutwa madereva maalum kwa kazi hizo na sio madereva waoga waoga
KUNA RAFIKI YANGU ALISHAWAHI KUWA TRANSPORT MANAGER KWENYE KAMPUNI MOJA YA MAGAZETI ALINIAMBIA KUWA GARI ZA MAGAZETI HUWA HAZISIMAMISHWI NA MATRAFKI HIYO NI SHERIA HATA MATRAFKI WANAJUA, PILI DEREVA ANAEWAHI KUFIKISHA MAGAZETI MAPEMA ZAIDI YA MUDA ALIOPANGIWA HUWA ANAONGEZEWA MUDA, MFANO KAMA AMETOKA DAR SAA SABA USIKU ANAENDA ARUSHA AKIFIKA SAA KUMI NA MBILI MUDA ALIOPANGIWA ATAPEWA ELFU 50 HIYO NI NJE YA MSHAHARA NA IKITOKEA AMEFIKISHA MAGEZTI MAPEMA ZAIDI MFANO SAA KUMI NA MOJA ASUBUHI BADALA YA KUPEWA ELFU 50 ATAPEWA LAKI MOJA NA IKITOKEA AMECHELEWA KUFIKA KABISA HAYO MAGAZETI YANAKUWA HASARA KWAKE ANAYANUNUA NA KUKATWA MSHAHARA KWAKUWA MAKAMPUNI YA MAGAZETI WANA MICHEZO YA KUHUJUMIANA,MFANO IKITOKEA GAZETI LAMWANANCHI LIMEWAHI KUFIKA ARUSHA KABLA YA NIPASHE INA MAANA WATU WATAANZA KUNUNUA GAZETI LA MWANANCHI KWAHIVYO WA NIPASHE AKICHELEWA LINAKOSA SOKO HALAFU HAYA MAKAPUNI MFANO LINAWEZA KUMFUATA DEREVA WA MWANANCHI LIKAMWAMBIA DEREVA TUNAKUPA LAKI 2 TUNATAKA UCHELEWE KUFIKA ILI SISI WA NIPASHE TUWAHI KUFIKA TUUZE NA DEREVA AKIAANGALIA HATA AKIWAHI SANA ANAPEWA LAKI KWAHIVYO ANAONA ACHUKUE LAKI 2 ILI ACHELEWE NDO HUJUMA ZENYEWE HIZO NA LA MWISHO MAGARI MENGI YA MAGAZETI HUWA YANAPIGWA BOMBA KWAHIVYO INAPOTOKEA AJALI YA TAIRI KUPASUKA NA GARI KUPINDUKA HUWA WANATOKA NDANI YA GARI HAWANA HATA JERAHA ZAIDI YA KUJIKUNG'UTA VUMBI TU ILA ZILE AJALI ZA KUOVERTAKE NA KUKUTANA USO KWA USO NA GARI NYINGINE HUO MZINGA NDIO HUWA HAWATOKI SALAMA.
 
Wabongo hawana shukrani nimeamini, sasa wewe umewahishwa safari zako alafu unasema wadhibitiwe tena mkuu?! Wangedhibitiwa ungewahi?
Ni moja ya nne huyo Mkuu umesahau ule utafiti!!?
 
Mbona 160 ni speed ya kawaida, mim mwenyewe siyo driver by professional lakini natembea mpaka 180 km per hour kama naenda Arusha sasa hao kila siku wako barabarani unashangaa 160!!!
Kachukue kazi kaka kwenye Magazeti
 
Salam sana ndugu zangu.Ni matumaini yangu kwamba week-end inakwenda vizuri sana!

Juzi siku ya Alhamisi January 19, 2017 niliingia "mkenge" kwa kupanda gari ya magazeti ya MWANANCHI kutoka Dsm to Arusha. Nilipanda hilo gari kwa sababu nilipata wito muhimu sana wa kuonana na mtu muhimu sana kesho yake Ijmaa saa 3 kamili asuubuhi.

Na nilifanikiwa kukaa seat ya mbele,hivyo nikawa naona namna dereva anavyocheza na usukani wake barabarani.

Speed 100 km /hr n ya kawaida sana kwa gari ya magazeti. Kuna muda anatembea speed mpk 160 km/hr.Dereva alikuwa amevaa shuka la kimasai na simu yake ya touch kwenye dushboard!

Ku-overtake malori hata kwenye kona, n kitu cha kawaida sana. Dereva anateendesha gari kuna wakati ananing'iniza mkono wake mmoja dirishani kwenye mlango wake, huku mkono mmoja ukiwa ndiyo unapapasa usikani!Balaaa.

Mbaya zaidi akawa anaongea na madereva wenzie ambao nao wameondoka Dsm na kuelekea mikoani.

Kuna vitu visivyoisha,dereva alianza kuvitafuna Dsm mpk tumeingia Arusha.

Tochi za kuwathibiti hawa madereva haziwanasi jamani?

Kwann trafic wasiwakamate hao madereva pindi wanapoona muda ambao wametumia n mfupi?Na kwann wasitumie usafiri wa ndege kutawanya hayo magazeti Au kwa nn wasiongeze vituo vya uchapishaji huko mikoani?
ww unastahili kupewa tuzo ya mnafiki bora wa mwaka.
 
Salam sana ndugu zangu.Ni matumaini yangu kwamba week-end inakwenda vizuri sana!

Juzi siku ya Alhamisi January 19, 2017 niliingia "mkenge" kwa kupanda gari ya magazeti ya MWANANCHI kutoka Dsm to Arusha. Nilipanda hilo gari kwa sababu nilipata wito muhimu sana wa kuonana na mtu muhimu sana kesho yake Ijmaa saa 3 kamili asuubuhi.

Na nilifanikiwa kukaa seat ya mbele,hivyo nikawa naona namna dereva anavyocheza na usukani wake barabarani.

Speed 100 km /hr n ya kawaida sana kwa gari ya magazeti. Kuna muda anatembea speed mpk 160 km/hr.Dereva alikuwa amevaa shuka la kimasai na simu yake ya touch kwenye dushboard!

Ku-overtake malori hata kwenye kona, n kitu cha kawaida sana. Dereva anateendesha gari kuna wakati ananing'iniza mkono wake mmoja dirishani kwenye mlango wake, huku mkono mmoja ukiwa ndiyo unapapasa usikani!Balaaa.

Mbaya zaidi akawa anaongea na madereva wenzie ambao nao wameondoka Dsm na kuelekea mikoani.

Kuna vitu visivyoisha,dereva alianza kuvitafuna Dsm mpk tumeingia Arusha.

Tochi za kuwathibiti hawa madereva haziwanasi jamani?

Kwann trafic wasiwakamate hao madereva pindi wanapoona muda ambao wametumia n mfupi?Na kwann wasitumie usafiri wa ndege kutawanya hayo magazeti Au kwa nn wasiongeze vituo vya uchapishaji huko mikoani?
Hiyo siyo gari ya abiria saasa wewe hizo ni shida zako tuu. Huo ni mwendo wa kawaida sana hususan usiku.
 
Mbona wewe usipande hiyo ndege? Halafu hivyo vitu anavyotafuna usiku kucha ndo vinampa stamina na ujasiri vinginevyo ni RISK, RISK.
 
Salam sana ndugu zangu.Ni matumaini yangu kwamba week-end inakwenda vizuri sana!

Juzi siku ya Alhamisi January 19, 2017 niliingia "mkenge" kwa kupanda gari ya magazeti ya MWANANCHI kutoka Dsm to Arusha. Nilipanda hilo gari kwa sababu nilipata wito muhimu sana wa kuonana na mtu muhimu sana kesho yake Ijmaa saa 3 kamili asuubuhi.

Na nilifanikiwa kukaa seat ya mbele,hivyo nikawa naona namna dereva anavyocheza na usukani wake barabarani.

Speed 100 km /hr n ya kawaida sana kwa gari ya magazeti. Kuna muda anatembea speed mpk 160 km/hr.Dereva alikuwa amevaa shuka la kimasai na simu yake ya touch kwenye dushboard!

Ku-overtake malori hata kwenye kona, n kitu cha kawaida sana. Dereva anateendesha gari kuna wakati ananing'iniza mkono wake mmoja dirishani kwenye mlango wake, huku mkono mmoja ukiwa ndiyo unapapasa usikani!Balaaa.

Mbaya zaidi akawa anaongea na madereva wenzie ambao nao wameondoka Dsm na kuelekea mikoani.

Kuna vitu visivyoisha,dereva alianza kuvitafuna Dsm mpk tumeingia Arusha.

Tochi za kuwathibiti hawa madereva haziwanasi jamani?

Kwann trafic wasiwakamate hao madereva pindi wanapoona muda ambao wametumia n mfupi?Na kwann wasitumie usafiri wa ndege kutawanya hayo magazeti Au kwa nn wasiongeze vituo vya uchapishaji huko mikoani?
Bila hilo gari ungewahi hiyo ahadi yako?
 
Salam sana ndugu zangu.Ni matumaini yangu kwamba week-end inakwenda vizuri sana!

Juzi siku ya Alhamisi January 19, 2017 niliingia "mkenge" kwa kupanda gari ya magazeti ya MWANANCHI kutoka Dsm to Arusha. Nilipanda hilo gari kwa sababu nilipata wito muhimu sana wa kuonana na mtu muhimu sana kesho yake Ijmaa saa 3 kamili asuubuhi.

Na nilifanikiwa kukaa seat ya mbele,hivyo nikawa naona namna dereva anavyocheza na usukani wake barabarani.

Speed 100 km /hr n ya kawaida sana kwa gari ya magazeti. Kuna muda anatembea speed mpk 160 km/hr.Dereva alikuwa amevaa shuka la kimasai na simu yake ya touch kwenye dushboard!

Ku-overtake malori hata kwenye kona, n kitu cha kawaida sana. Dereva anateendesha gari kuna wakati ananing'iniza mkono wake mmoja dirishani kwenye mlango wake, huku mkono mmoja ukiwa ndiyo unapapasa usikani!Balaaa.

Mbaya zaidi akawa anaongea na madereva wenzie ambao nao wameondoka Dsm na kuelekea mikoani.

Kuna vitu visivyoisha,dereva alianza kuvitafuna Dsm mpk tumeingia Arusha.

Tochi za kuwathibiti hawa madereva haziwanasi jamani?

Kwann trafic wasiwakamate hao madereva pindi wanapoona muda ambao wametumia n mfupi?Na kwann wasitumie usafiri wa ndege kutawanya hayo magazeti Au kwa nn wasiongeze vituo vya uchapishaji huko mikoani?
Hii habari imerudiwa naona imebadilishwa tarehe tu sawa pole
 
Umesaidiwa kuwahi

Halafu unawaponda unataka wadhibitiwe

Bila hao wa magazeti unafikiri safari yako ungeiwahi

Kama ulivyokuwa na shida nao siku ya alhamisi fahamu kuna watu kila siku wanashida nao wanataka kuwahi na emergency kibao hupata

Mwisho ushawahi kusikia ajali za hizi magari za magazeti? Nadra sana

Waache wapige gia bwana..hawa madereva huwa ni tatizo usipokuwa mvumilivu utaomba ushushwe porini

Hawa ni special case kwahiyo unataka watembee na 60 wafikishe magazeti saa ngapi huko?

[/QUOTE swali zuri
 
Back
Top Bottom