KUOA MWANAMKE MUUZA BAR/PUB

KUOA MWANAMKE MUUZA BAR/PUB

Mke amefungua pub bila kunishirikisha na anauza mwenyewe kama bar maid nyumba imewaka moto Sababu mke amekua jeuri na kiburi,so aggressive hakuna unachouliza ukajibiwa kistaarabu. Kila mteja anayeenda pale akiomba namba anapewa tu bila shida yupo bize muda wote ni pub pub na `wateja wake" kama anavyowaita hajali familia wala ndoa tena nyumba,chumba chakulala kimekua km stoo kitanda ndio usiseme hajali na imefikia hatua naambiwa nisifike hata kwenye biashara yake sababu namfukuzia wateja wake.
Tupo kwenye ndoa yakikatoliki mwaka wa 4 sasa na tuna watoto wawili wadogo 4yrs na 2yrs.

Ushauri, nifanye nini?
Muache haraka sana....
 
Nilipata kibarua mkoani kwenye kampuni moja ya ujenzi
Pole sana, lakini nikulize kitu mpaka mkeo anafungua pub wewe ulikuwa wapi? Au ndiyo yale haujulikani saangapi unakuwa mke au baba, maana kama ulikuwa upo naye kwakila kitu halafu yeye akafanya alioyafanya! Maana wanaume wengi mkioa wake zenu mnaona kama mfugo ndani mnawapuuza mtu mpaka afungue biashara upo tu
 
Aseee hapo itabidi Sasa umshirikishe MUNGU uone anasemaje
 
Unasubiri barua ya mwenyekiti wa kijiji hili kuthibitisha kuwa mkeo hakupendi?
Waite wazazi wake na yeye akiwepo wambie ukweli na msimamo wako iwapo hatabadili tabia.
Halafu kuwa mkali hili ijulikane humo ndani mwanaume ni nani.
Kaza sura
Kaza sauti.
Njia ndefu hiyo....
 
Mkuu una moyo wa chuma cha pua maana kama ningekuwa mimi hata uzi nisianzisha na badala yake angekuwa kwao saizi na mimi naanzisha maisha nje uwepo wake



Anyway ubora na ubovu wa msingi anaujua mjenz mwenyew
 
Kuna mawili
1) Alikuvumilia wewe sana kwanza sasa amechoka dharau zako kaamua kukaza buti.
2) Utakuwa mume bwege na mke ndio ana sauti kwenye ndoa yenu.

Tafakari kabla ya athari


Ndukiiiii 🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️
 
Pole sana, lakini nikulize kitu mpaka mkeo anafungua pub wewe ulikuwa wapi? Au ndiyo yale haujulikani saangapi unakuwa mke au baba, maana kama ulikuwa upo naye kwakila kitu halafu yeye akafanya alioyafanya! Maana wanaume wengi mkioa wake zenu mnaona kama mfugo ndani mnawapuuza mtu mpaka afungue biashara upo tu

Kuna watu wana siri ndani ya ndoa hata shetani anawashangaa. Kuna watu waume/wake wamejenga na wala wenzi wao hawajui, and they're just close...

Binadamu ni kiumbe wa ajabu sana kutokea duniani...!
 
Pole, kwani, vile mtu mmoja tu kasema wewe mwanaume na wewe mwanamke sasa mmekuwa mke na mume uliamini kuwa huyo amekuwa "photocopy" ya akili yako?!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Mke amefungua pub bila kunishirikisha na anauza mwenyewe kama bar maid nyumba imewaka moto Sababu mke amekua jeuri na kiburi,so aggressive hakuna unachouliza ukajibiwa kistaarabu. Kila mteja anayeenda pale akiomba namba anapewa tu bila shida yupo bize muda wote ni pub pub na `wateja wake" kama anavyowaita hajali familia wala ndoa tena nyumba,chumba chakulala kimekua km stoo kitanda ndio usiseme hajali na imefikia hatua naambiwa nisifike hata kwenye biashara yake sababu namfukuzia wateja wake.
Tupo kwenye ndoa yakikatoliki mwaka wa 4 sasa na tuna watoto wawili wadogo 4yrs na 2yrs.

Ushauri, nifanye nini?


Piga chini, chukua watoto wako mwache yeye ale maisha ya ubaa maid na wateja wake. Achana na masuala ya dini, haitakusaidia chochote maishani hizi dini za watu wa nje (Uislam na Ukristu) ni janga kwetu waafrika na ndizo zinazotuharibu akili (rudia ya Rose Muhando). Mungu hajakataza wewe uishi kwa furaha, sasa kwanini dini ikuzuie usimuache huyo mke uishi kwa raha na amani na hao watoto wako?
 
Kifo tu ndicho kitakachowatenganisha
 
Kabisa!!!
Kuna watu wana siri ndani ya ndoa hata shetani anawashangaa. Kuna watu waume/wake wamejenga na wala wenzi wao hawajui, and they're just close...

Binadamu ni kiumbe wa ajabu sana kutokea duniani...!
 
Tungesikiliza upande wa pili wa kesi yako ingependeza zaidi. .... nipe anuwani ya hiyo bar nikamsikilize naye anasemaje.
 
Nenda na wewe uwe mteja wake.kunywa kwa kulipia halafu unamuacchia na tip.pia muombe na mamba yake ya simu.

Mambo yatabadilika tuu.maana mapenzi ameshayahamishia kwa wateja.dawa na wewe ni kuwa mteja wake
 
Back
Top Bottom