KUOA MWANAMKE MUUZA BAR/PUB

KUOA MWANAMKE MUUZA BAR/PUB

Unasubiri barua ya mwenyekiti wa kijiji hili kuthibitisha kuwa mkeo hakupendi?
Waite wazazi wake na yeye akiwepo wambie ukweli na msimamo wako iwapo hatabadili tabia.
Halafu kuwa mkali hili ijulikane humo ndani mwanaume ni nani.
Kaza sura
Kaza sauti.
 
Unasubiri barua ya mwenyekiti wa kijiji hili kuthibitisha kuwa mkeo hakupendi?
Waite wazazi wake na yeye akiwepo wambie ukweli na msimamo wako iwapo hatabadili tabia.
Halafu kuwa mkali hili ijulikane humo ndani mwanaume ni nani.
Kaza sura
Kaza sauti.
Kwanini mnapenda kusumbua wazazi kwa vitu vidogo na vya kipuuzi kama hivi? Seriously hili nalo ni la kuita wazazi? Wao ndio wameoa?

Mtakuja lini kuelewa na kukubali kuwa ndoa ni makubaliano na kiapo cha watu wawili? Hatima ya ndoa ni uamuzi wa wanandoa wenyewe. Period!
 
Unaweza kumtafutia shughuli nyingine ambayo naye ataridhia kuifanya?
Mke amefungua pub bila kunishirikisha na anauza mwenyewe kama bar maid nyumba imewaka moto Sababu mke amekua jeuri na kiburi,so aggressive hakuna unachouliza ukajibiwa kistaarabu. Kila mteja anayeenda pale akiomba namba anapewa tu bila shida yupo bize muda wote ni pub pub na `wateja wake" kama anavyowaita hajali familia wala ndoa tena nyumba,chumba chakulala kimekua km stoo kitanda ndio usiseme hajali na imefikia hatua naambiwa nisifike hata kwenye biashara yake sababu namfukuzia wateja wake.
Tupo kwenye ndoa yakikatoliki mwaka wa 4 sasa na tuna watoto wawili wadogo 4yrs na 2yrs.

Ushauri, nifanye nini?
 
Sina mengi ya kukuchosha ila kwa kauli hizo na hulka ya wateja wake;
1. Jiandae kudharaulika zaidi
2. Jiandae kuchapiwa
3. Jiandae kupata magonjwa ya zinaa na hata yasiyo ya zinaa
- Utapata stress muda wote, moyo na pressure.
4. Ipo siku atakuaibisha tu,iwe home au kwenye biashara zake.

Zaidi ya yote, jiandae kutengana naye. Najua hutavumilia manyanyaso hayo na zipo siku utanyimwa hata tendo la ndoa.
 
Hata kama isingekuwa pub, kufungua biashara bila kukuambia ni kosa lakini mbaya zaidi biashara yenyewe ni pub na mwenendo wake ndio kama ulivyoeleza... Let mi tell one thing big bro, Hatupo duniani ili kudharauliwa na kunyanyasika ukiona mtu anakudharau na haonyeshi dalili yoyote ya kubadilika kwanini uendelee kuwa nae? Maisha yako ni bora zaidi. Fanya maamuzi, kuna wanawake wengi wanakusubiri uishi nao kwa furaha kama huyo ameshindwa
 
Pole sana, lakini nikulize kitu mpaka mkeo anafungua pub wewe ulikuwa wapi? Au ndiyo yale haujulikani saangapi unakuwa mke au baba, maana kama ulikuwa upo naye kwakila kitu halafu yeye akafanya alioyafanya! Maana wanaume wengi mkioa wake zenu mnaona kama mfugo ndani mnawapuuza mtu mpaka afungue biashara upo tu
 
Kwani Ndoa ya Kikatoliki Si Ndie Yenye Kipengele Cha Kuto Achana?.

Dah! Pole Sana Mkuu.
 
Back
Top Bottom