Kunguru kunidonyoa kichwani

Kunguru kunidonyoa kichwani

Habarini! hivi hili swala la kunguru kukudonyoa kichwani Lina maana gani? Mara ya kwanza kunitokea nikafikiri kwa vile nilivaa shati jeusi, lakini Leo pia imenitokea Cha kushangaza ni Mimi tu wengine hawadonyolewi
Anadonoa akili yako kidogo kidogo anenda kuiuza apate hela. Una akili nyingi sana mkuu?
 
Mkuu me nahisi kitu,
Unaweza kudhani unakichwa cha binadamu kumbe unatembea na dumple la takataka bila wewe kujua. Kwanini wewe tu? Mkuu huna kichwa cha binadamu. Me nahisi hivyo
 
Je una ki'patch' cha nywele zenye mvi nyeupe kichwani? Ikiwa ni hivyo inabidi uwe unavaa kama kofia au ukipake rangi nyeusi
 
Habarini! hivi hili swala la kunguru kukudonyoa kichwani Lina maana gani? Mara ya kwanza kunitokea nikafikiri kwa vile nilivaa shati jeusi, lakini Leo pia imenitokea Cha kushangaza ni Mimi tu wengine hawadonyolewi
Kasome biblia mwanzo habari za Yusuphu alipofungwa gerezani akakutana na wale wafungwa watatu walioota ndoto na yusuphu akawatafsiria! Mmoja aliota ndoto km hii japo we sio ndoto ila anzia hapo utaelewa!
 
Habarini! hivi hili swala la kunguru kukudonyoa kichwani Lina maana gani? Mara ya kwanza kunitokea nikafikiri kwa vile nilivaa shati jeusi, lakini Leo pia imenitokea Cha kushangaza ni Mimi tu wengine hawadonyolewi
Utakuwa umewahi kuharibu kiota chao au kuua kunguru, kunguru wakikujua wanafahamishana na wako makini sana kukutambua na huitana wakikuona hata ukijaribu kujibadilisha kimavazi, ukitaka wakuogope beba manati.
Kachome sindano ya pepopunda (tetenasi) vinginevyo unaweza ukafa kimzahamzaha.
 
Je ulishawahi kuua kunguru au kumpiga kinda wa kunguru

Ova
Utotoni niliwahi kukamata kitoto cha Kunguru, aisee wale Jamaa pamoja na kukaachia katoto kao ila waliniwekea Bifu karibia wiki nzima, kila nikikatiza maeneo yao walikuwa wananivagaa na kunipa ambush hasa maeneo ya kichwani.. Ikabidi nibadilishe njia Kwa muda..
 
Utotoni niliwahi kukamata kitoto cha Kunguru, aisee wale Jamaa pamoja na kukaachia katoto kao ila waliniwekea Bifu karibia wiki nzima, kila nikikatiza maeneo yao walikuwa wananivagaa na kunipa ambush hasa maeneo ya kichwani.. Ikabidi nibadilishe njia Kwa muda..
Vita vyao haviishi 😂

Ova
 
kichwan apo pamekaa vizuri kweli maana anaweza donoa akazan ni msosi kumbe sio ni kichwa cha mtu nyoa kibara uone kama atadonoa inawezekana nywele zimekaa kama chakula cha kunguru
Hahahaha
 
Back
Top Bottom