Video ya IS yasemekana kuonyesha mauaji ya wakristo wa Nigeria
Kundi la Islamic State limechapisha video ambayo inasadikiwa kuonyesha raia 20 waumini wa Kikristo wakiuawa katika jimbo la Borno kaskazini mashariki mwa Nigeria.
Akizungumza kwa lugha ya Kihausa, mmoja wa wanamgambo walofunika nyuso zao alionyesha kisu akisema ilikuwa ni kulipiza kisasi mauaji ya viongozi wa kundi hilo Mashariki ya Kati mapema mwaka huu.
BBC haijaweza kuthibitisha maudhui ya video hiyo au mahali ambapo picha hiyo ilipigwa.
Ilichapishwa kwenye chombo cha habari kilichounganishwa na IS na inaonyesha makundi matatu ya mateka wakiwa wamevalia mavazi ya kiraia.
Mamlaka bado haijatoa maoni kuhusu video hiyo.
Wanamgambo wa IS, wanaoendesha harakati zao katika eneo la Ziwa Chad kwa jina la Islamic State West Africa Province (Iswap), pamoja na kundi jingine la wanamgambo wa Kiislamu, Boko Haram, hivi karibuni wamepata hasara kubwa kutokana na mashambulizi ya jeshi la mataifa mbalimbali.
Kampeni hizo za kijeshi siku za nyuma kwa kawaida zimekuwa zikifuatiwa na video za propaganda kutoka kwa makundi yenye itikadi kali.
Chanzo BBC.
Kundi la Islamic State limechapisha video ambayo inasadikiwa kuonyesha raia 20 waumini wa Kikristo wakiuawa katika jimbo la Borno kaskazini mashariki mwa Nigeria.
Akizungumza kwa lugha ya Kihausa, mmoja wa wanamgambo walofunika nyuso zao alionyesha kisu akisema ilikuwa ni kulipiza kisasi mauaji ya viongozi wa kundi hilo Mashariki ya Kati mapema mwaka huu.
BBC haijaweza kuthibitisha maudhui ya video hiyo au mahali ambapo picha hiyo ilipigwa.
Ilichapishwa kwenye chombo cha habari kilichounganishwa na IS na inaonyesha makundi matatu ya mateka wakiwa wamevalia mavazi ya kiraia.
Mamlaka bado haijatoa maoni kuhusu video hiyo.
Wanamgambo wa IS, wanaoendesha harakati zao katika eneo la Ziwa Chad kwa jina la Islamic State West Africa Province (Iswap), pamoja na kundi jingine la wanamgambo wa Kiislamu, Boko Haram, hivi karibuni wamepata hasara kubwa kutokana na mashambulizi ya jeshi la mataifa mbalimbali.
Kampeni hizo za kijeshi siku za nyuma kwa kawaida zimekuwa zikifuatiwa na video za propaganda kutoka kwa makundi yenye itikadi kali.
Chanzo BBC.