Kuna vitu naviona angani usiku huu baada ya umeme kukatika

smarte_r

JF-Expert Member
Nov 8, 2013
4,537
11,869
Nipo masikani kwangu usiku huu kwenye kitongoji fulani hapa Dar.

Umeme wa TANESCO umekatika kutokana na mgao. nje ya nyumba yangu kuna upepo mzuri wa asili na ukimya mwingi, yaani hata zile kelele za mziki kutoka bar na grocery za jirani hazisikiki.

Nikiwa hapa nje kulishangaa anga kutokana na maajabu yake ya kiuumbaji, ghafla nimeona nyota tatu angani mashariki mwa Dar zikitembea kwa kasi sana kuelekea magharibi mwa nchi.

Nimetafakari sana. sasa sijui ndio dalili ya mwana wa adamu kurudi duniani kwa mujibu wa maandiko ya dini?, Au labda anga letu limetembelewa na viumbe kutoka sayari za mbali(aliens )?.

Vipi wenzangu hamjaona chochote huko angani?
 
Kweli uumbaji unapendeza, mataa taa na makelele huwa yanaficha this good vibe I'm having right now. Sema bar yetu jirani inapiga ngoma za kizaramo sijui kimakonde, sio mbaya, good choice
watu wanaoishi ktk vijiji ambavyo umeme wa tanesco haujafika, wana siri nyingi sana kutokana na yale wanayoyashudia angani mida ya usiku.

kwa huku mijini hivi vitu huwezi kuviona wakati umeme upo. ni mida ya usiku tu umeme unapokatika.
 
Hizo ni ndege tuu mkuu, usipige jani la zaidi ya uwezo wako ndugu...
ndege gani hazina mngurumo ndg?. kumbuka kuna ukimya mwingi sana baada ya umeme kukatika. sijasikia mngurumo wowote.
 
Ama kwa hakika kizazi kilichozaliwa kwenye umeme tuu kuna vingi mmevikosa...

Tuliozaliwa kwenye giza, dinner ilikuwa lazima iliwe kabla jua halijazama, au kama ni kipindi cha mwezi basi mnatumia mwanga wa mbalamwezi.

Mkishamaliza mnakaa hapo nje kupiga stori 2 , 3. Vijana mnaweza kuzama porini kuwinda vitoweo, mnakuwa na tochi yenye mwanga mkaliii, mkimpiga mnyama na mwanga anaduwaa tuu mnamsogelea mnammaliza kiulainiii.

Hapo ni kijiji kizima hakina umeme, hivyo hayo mambo unayoyasema wewe tumeyaona sana huko angani. Kuna tuvitu kama nyota ila vinatembea, basi jua hizo ni satelaiti za anga za mbali. Kuna vimondo ambavyo hudondoka ila vinaishia angani, yani unaona kama nyota inadondoka ardhini ila inazima kabla haijatua chini.

Watoto mliozaliwa 2000 haya maisha hamuwezi elewa, washukuruni tanesco wamewasaidia kuwapa experience😀
 
Back
Top Bottom