johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 83,968
- 141,975
Kwa namna upepo wa siasa za Tanzania bara unavyokwenda ni wazi vyama vya upinzani vina nafasi finyu ya kushinda mwaka 2020. Hii inatokana na ukweli kwamba vyama hivyo vimekosa ajenda na hoja.
Ile hoja iliyokuwa inawabeba katika umri wake wote wa zaidi ya miaka 25 yaani mapambano dhidi ya ufisadi sasa imebebwa kikamilifu na CCM na kuwaacha wapinzani kubakia kama walalamikaji tu.
Hadi sasa hakuna jimbo lolote huku bara ambalo upinzani una uhakika wa kushinda na chama kikuu cha upinzani kwa sasa Chadema ndio kimevurugwa kabisa.
CUF bado wana ngome yao Pemba ambayo haitashindwa kutoa angalao wabunge watano na hivyo kulibakiza bunge letu katika hali ya mfumo wa vyama vingi.
Niishie hapo!
Ile hoja iliyokuwa inawabeba katika umri wake wote wa zaidi ya miaka 25 yaani mapambano dhidi ya ufisadi sasa imebebwa kikamilifu na CCM na kuwaacha wapinzani kubakia kama walalamikaji tu.
Hadi sasa hakuna jimbo lolote huku bara ambalo upinzani una uhakika wa kushinda na chama kikuu cha upinzani kwa sasa Chadema ndio kimevurugwa kabisa.
CUF bado wana ngome yao Pemba ambayo haitashindwa kutoa angalao wabunge watano na hivyo kulibakiza bunge letu katika hali ya mfumo wa vyama vingi.
Niishie hapo!